Wapenzi na wadau wa vitabu nisaidieni hili

Trubetzkoy

JF-Expert Member
Oct 31, 2018
298
542
Habari za wakati huu mabibi na mabwana!

Leo ikiwa ni siku ya kumi tangu tulipouanza
mwaka 2022 naomba msaada wa mawazo yenu ambayo kwa namna ya pekee naweza kuyatumia kama njia ya kuelekea kufanikisha malengo niliyojiwekea kwa mwaka huu wa 2022.

Mimi ni mwandishi mchanga/chipukizi. Nina uwezo na kipaji cha kutunga na kuandika vitabu pamoja na makala zinazohusu masuala mbalimbali ya kijamii. Uwezo na kipaji changu vimedhihirika tangu nikiwa chuoni 2016--2019.

Ndoto zangu zikiwa ni kuwa mwandishi nguli huku role model wangu akiwa ni Late Prof Euphrase Kezilahabi, nimeona ni vema nijieleze humu ili nipate mawazo yenu huku nikiamini kuwa hili ni jukwaa ambalo msaada wa aina yoyote unaweza kupatikana.

Lengo la uzi huu ni kuomba kufahamishwa juu ya hatua ninazopaswa kuzichukua pindi nimalizapo kuandika muswada wa kitabu ikiwa ni pamoja na namna ya kupata muhariri, wachapishaji mpaka kufikia hatua ya kuingiza kitabu sokoni.

Naomba nipewe elimu ili kipaji changu kisipotee.

Nawasilisha.
 
In the age of self publishing all you need is marketing..., Na katika karne hii ya watu wasiopenda kusoma vitabu na urahisi wa publishing ni lazima utafute / u-cultivate soko lake mwenyewe kwahio andika weka out there fanya market watu wakuelewe ukipata following ya kutosha umetoboa...

Cha maana usiandike tu ili upate pesa kwahio kama unapenda kazi yako wewe andika tu hata usipouza sana (publishing ebook can be free) hakuna neno ili mradi you are doing what you like...
 
In the age of self publishing all you need is marketing..., Na katika karne hii ya watu wasiopenda kusoma vitabu na urahisi wa publishing ni lazima utafute / u-cultivate soko lake mwenyewe kwahio andika weka out there fanya market watu wakuelewe ukipata following ya kutosha umetoboa...

Cha maana usiandike tu ili upate pesa kwahio kama unapenda kazi yako wewe andika tu hata usipouza sana (publishing ebook can be free) hakuna neno ili mradi you are doing what you like...
Asante kwa mawazo mazuri
 
Back
Top Bottom