Wapenzi lakini hatujawahi kuonana

Wapenzi lakini hatujawahi kuonana

Liss Liss

Member
Joined
Nov 20, 2015
Posts
37
Reaction score
2
Habarini wandugu na poleni na majukumu ya kila siku, 2014 mwishoni nlitumiwa sms ya salamu ya kawaida tu na namba ilikuwa ngeni. Nikapiga simu akapokea mdada baada ya salamu akaniuliza wewe nani nikamwambia umentumia sms akadai kama ni hivo basi atakua alikosea namba.

Tukaendelea kuwasilina tukazoeana sana kupitia simu. Mwezi wa tatu hivi 2015 nikamu approach tukawa wapenzi yaani vizuri tu japo hatujawahi kuonana yaani sometime hadi tuna gombana tunapatana kama tumewahi kuonana hivi, miezi michache iliyopita nimehamia mji ambao yeye yupo nilimwambia akafurahi sana tatizo linakuja sasa nikimwambia tuonane anakwepa kwa visingizio kibao mara nyingine husema anakuja halafu kimya had leo hii hatuja onana.

Nashindwa kuelewa kwa nini hataki tuonane anataka mawasiliano ya simu tu.

Naomba ushauri wenu
 
Hamna mapenzi hapo mkuu achana nae huyoo..
 
Atakuwa mke/mume wa mtu huyo! Hivyo anaogopa kuunguza nyumba yake...na bila shaka yeye/ mwenzake atakuwa ni mwenyeji sana wa huo mji, hivyo anaogopa kuonekana na mwingine!
 
Huwa unamtumia pesa kwa mobile money?


Nasikia siku hizi wapo wadada kibao pale Sinza wanapanga vyumba guest house na mchana kutwa wanajaribu bahati zao kwa kubeep numba yoyote. Halafu nasikia siku za nyumba kabla ya JPM walikuwa wanapata sana....

Ndiyo mambo ya kukamata fursa!
 
Duh huu umalaya mkubwa sana, yaani unakua malaya hadi unatongoza sauti ya mtu kwenye simu?? Kama hataki munane please please relax and move on, akikutafuta mwambie ushahama, kama ulikua na guts za kumtongoza huyo utapata mwingine tu sio lazima ubakie nae huyo
 
hii ishawahi kunitokea baaaaaadaeeeeee niligundua "mwenzangu" alijipa maujiko ambayo kiuhasilia hakuwa nayo.
 
Back
Top Bottom