Wapenda choir

Wapenda choir

Starwars91

Member
Joined
Jul 12, 2020
Posts
52
Reaction score
47
Mimi ni mkatoliki. Kuna kwaya huwa inanikosha sana hapa Tanzania. Ni kwaya ya mtakatifu kizito parokia ya mtakatifu mwenye heri anuarite iliyoko makuburi Dar es salaam. Kwa kweli ni kwaya ambayo inaimba vizuri sana. Ikiongozwa na mwandishi machachari Wa nyimbo za ki injili za kikatoliki bwana Bernard Mukasa. Jaman kwa wale wakatoliki nahisi wanaifahamu hiii kwaya. Hata wale wasio wakatoliki wanaweza kuwa washawahi kusikia nyimbo zao nzuri na tamu sana. Nyimbo yao bora zaidi ambayo imeweza kupenya mpaka nje ya mipaka ya Tanzania inaitwa "mimina" wanazo pia nyingine nzuri nyingi tu. "Nyota ya mashariki", " wewe ni mungu" , "nusu kwa nusu", " Mungu ni upendo" , "mwanzi uliopondeka" ya kwake Bernard mukasa mwenyewe. Kwa kweli inapendeza sana. Ingawaje ninapenda waimbaji hawa, lakin nyimbo zangu mbili bora za kikatoliki ni "bwana unibadili" ilioimbwa na kwaya ya mtakatifu maria Goreti chuo kikuu cha ushirika moshi na "mbingu zilifunguka" ilioimbwa na kwaya ya parokia ya korogwe ilioko Tanga. Kongole kwa waimbaji hawa. Wapenzi mnaweza kuziangalia katika YouTube. Jumapili njema kwenu watanzania wote.
 
Naomba kuunga mkono hoja chief ninajamaa zangu wapo kwenye iyo kwaya ya makuburi jamaa wapo vizuri alafu iyo kwaya kwa ujumla wapo njema kifedha wanawadhamini wengi hasa wachaga
 
Mimi ni mkatoliki. Kuna kwaya huwa inanikosha sana hapa Tanzania. Ni kwaya ya mtakatifu kizito parokia ya mtakatifu mwenye heri anuarite iliyoko makuburi Dar es salaam. Kwa kweli ni kwaya ambayo inaimba vizuri sana. Ikiongozwa na mwandishi machachari Wa nyimbo za ki injili za kikatoliki bwana Bernard Mukasa. Jaman kwa wale wakatoliki nahisi wanaifahamu hiii kwaya. Hata wale wasio wakatoliki wanaweza kuwa washawahi kusikia nyimbo zao nzuri na tamu sana. Nyimbo yao bora zaidi ambayo imeweza kupenya mpaka nje ya mipaka ya Tanzania inaitwa "mimina" wanazo pia nyingine nzuri nyingi tu. "Nyota ya mashariki", " wewe ni mungu" , "nusu kwa nusu", " Mungu ni upendo" , "mwanzi uliopondeka" ya kwake Bernard mukasa mwenyewe. Kwa kweli inapendeza sana. Ingawaje ninapenda waimbaji hawa, lakin nyimbo zangu mbili bora za kikatoliki ni "bwana unibadili" ilioimbwa na kwaya ya mtakatifu maria Goreti chuo kikuu cha ushirika moshi na "mbingu zilifunguka" ilioimbwa na kwaya ya parokia ya korogwe ilioko Tanga. Kongole kwa waimbaji hawa. Wapenzi mnaweza kuziangalia katika YouTube. Jumapili njema kwenu watanzania wote.

Maria goreti kwa kweli ule wimbo walisimama Sana.
 
Wimbo wa Mwanadamu Kumbuka U Mavumbi Wewe. Wimbo huo ni wa Kikatoliki. Wapi wapatikanika kwa kununua / kudaunilodi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom