Wapambana Rushwa wanapopewa wanaochunguzwa kuwaongoza

Mfumo wa mafunzo ubadilishwe na uwe wa kiujuzi na kinkakati katika kutokomeza rushwa na kuwe na uhuru kama ilivyo ktk nchi nyingine siyo ubabe ndani na nje ya taasisi.

Niwazi bado mafunzo yao siyo yabkimkakati kwani ni semina tu ya miezi 3 kwa mtu mwenye shahada yoyote ile iwe kilimo,uchumi,maktaba,sayansi ya jamii,n.k ambapo hujifunza partial marshal art kwaajili ya self defence na baadhi ya sheria na walimu wakiwa maboss wao au watangulizi wao na baadhi ya wakufunzi waalikwa kutoka polisi,mahakama,nk na ndito maana wanatoka nje ya majukumu yao.

Ndani ya hito course wanajifunza za pcca,cpa,tea,eoca na pc juu tu siyo kwa undani kwa hiyo miezi mitatu pasipo kujifunza masomo mengine yahusuyo RUSHWA na UCHUNGUZI.

Baada ya hapo eti watu wanakuwa wamehitimu tayari kupambana rushwa,kweli?

Haya baada ya miaka kama kumi kazini wanaenda semina ya senior ambao sasa hawa ndiyo wanachaguliwa kuwa dbcs,agrbcs,rbcs,directors,nk kwa fadhira za DG siyo kwa sababu ya elimu ya rushwa na ubobezi ktk maswala ya uchunguzi.

Haya hao watu unawaingiza mtaani na shahada zao na hiyo BIC wakachunguze na kupambana na rushwa kwa kupokea taarifa tu na siyo ujuzi.

Je huyo mtu atatenda miujiza ndani ya taasisi au nje ya taasisi katika kupambana na rushwa au utamlinganisha na polisi aliyepitia mafunzo na hatua mbalimbali ya uingozi?

Tukubali kubadilika takukuru hamna weredi na fairness zaidi ya ubabe na kuogopwa kwa fikira tu humo ndani kuna viongozi viraza kweli ambao wapo kulinda maslahi yao kwa kumpotosha kila DG ajae kwa kumlisha matango pori na kuwachongea subornates wenye vipaji pamoja na mwenda zake kuwaondoa baadhi yao na kuwapeleka taasisi nyinginezo mmoja wao akiwa aliyekuwa AgDPP.

Polisi wakisimamiwa wanaweza kabisa kutokomeza rushwa siyo kwa hii takukuru kupambana na rushwa siyo degree/master/phd, majengo,idadi kubwa ya watumishi,upendeleo na magari bali WEREDI

Viongozi wa takukuru wengi wanalipiana fedha za serikali kusomea elimu za juu vyuoni i.e pgraduate,masters,degree,phd badala ya kuwaandaa watu wa kada ya chini kwa kuwapa elimu nzuri zenye msingi ktk maswala ya kupambana na rushwa kwa kuanzia chini hadi juu.

Hivi kweli mtu mwenye shahada ya maktaba na hizo semina za bic na uandamizi anapewa mkoa au wilaya eti atokomeze rushwa bila nyongeza yoyote ya ujuzi wa uchunguzi wa maswala ya rushwa kunaweza kuleta tija?

TUTAFAKARI!!!!
Nyundo2017

Kwa kweli umeliweka kwa kina jambo hili. TAKUKURU inakosa mashiko na misingi ya kitaaluma ya mapambano ya Rushwa.

Wako pia wafagia ofisi na wahudumu. Wakipata degree wanakuwa wachunguzi automatically bila taalumu nyingine.

Nakumbuka Kuna wakati walikuwa na mkakati wa kujenga chuo chao cha mafunzo. Sijui likiishia wapi wazo hili
 
Hivi ukitaja rushwa nchi hii katika vyombo vya ulinzi akili yako inkutuma JWTZ au POLICE?

We unafikiri huyo police aliyeteuliwa mpaka SASA hajawahi pokea rushwa? Au hajawahi ona rushwa ikitembea waziwazi Huku akijua na kuinyamazia Kimya!

Nilitegemea Huku kujaa thread za watu wakipinga hiyo Taasisi ya TAKUKURU kukabiziwi police ili wajitathmni zaid na said,

Binafsi ktk Maisha yangu Kwa kusikia,kuona,kushiriki Jambo lolote linalowahusisha askari iwe Kwa kukamatwa ndugu,mtaani,Barabarani matrafik n.k sijawahi sikia askari akipinga rushwa zaidi ya kutoa maelekezo rushwa zao watazipataje ama zipelekwe Kwa Nani ili isiwe direct.
Kwa Hyo sikubaliani nao hao watu kitengo hicho
bado unaishi gizani sana.

nanyinyi kwa mitazamo hii ndio mnavunja mionyo wachache walioamua kuzifanya kazi hizo kwa haki,mko negative masaa 24.
unadhani polisi hakuna walokole na swala tano wanaomuogopa Mungu??

jikiteni katika kujadili namna ya kuwaboreshea maslahi ili tuwahukumu kwa haki,huko bandarini,takukuru,tra kuna mishahara na watu wanapiga mikunjo sio kizembe,hao polisi mnawalilia kisa buku mbili mbili zà barabarani mnazowapa huku mnawasimanga!!!!
 
Kwa Polisi ni OK. Polisi kisheria ndio wenye dhamana ya kushughulikia (kupeleleza) jinai zote na rushwa ikiwemo. Refer kesi ya R Vs Jerry Murro ambapo upande wa utetezi uliibua hoja kuwa, kama Jerry Murro aliomba rushwa kwa nini aliyeombwa rushwa hakwenda PCCB na akaenda Polisi? Hapa utetezi ulitaka kujenga hoja kuwa, inawezekana kuna mchezo ulikuwa umechezwa na Polisi na mtoa taarifa dhidi ya Jerry. Lakini mahakama ikaeleza kuwa, Polisi haizuiwi kwa vyovyote vile kudili na jinai yoyote ile, iwe jinai hiyo ina mamlaka yake tofauti kama ilivyo rushwa au lah.

Kwa hiyo, kwa kuwa PCCB ni chombo cha kupeleleza jinai, basi Polisi ni sahihi kabisa kupewa kukiongoza chombo hicho. Kwa JWTZ haikuwa poa sana, maana wao kitaaluma sio wapelelezi kabisa.
anajua nini huyo anahemka tu.
 
Mbunifu kwenye medani zakivita anapelekwa kwenye kupambana na rushwa ilihali kule hutumii bunduki na amri ,mtoaji ,mpokeaji wote hawa wanaakili sana,ndimana tunakuta rushwa inaendelea na ukuaji badala to decline

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app
 
Kwa rushwa zote hizo ambazo polisi wanajihusisha nazo, leo hii ndo mmoja wao anapewa mamlaka ya kusimamia taasisi ya kupambana na rushwa? ama kweli...
kama rushwa ni taasis zote zina rushwa.
ni different levels tu.
however si wote .. wapo wale wenye clean records.
 
Kwa JWTZ was ok,ila Kwa police a big no
Kwa Taarifa yako, CP Salum.Hamduni anakuwa Polisi wa Tatu kuiongoza PCCB ,alianza DCP Valentino Mlowola, Akaja CP Diwani Athumani, na Sasa CP Salum Nassor Hamduni.
Yule Brigadier wa Jeshi hakuwa anatosha kabisa pale, No wonder Most of the time akawa anavaa Sare za Jeshi, Combat kutaka ku hide Weaknesses zake
 
Kwa JWTZ was ok,ila Kwa police a big no
Sikiliza wewe police ndio wataalam unaongea ujinga tupu,police ni law enforcement agence ambayo anasimamia sheria zote za nchi kwa taarifa yako hiyo PCCB ilikuwa ndani ya police wakatenganisha ni ma nguli wa criminal investigation kwenye nyanja zote na wana power kubwa katika kuzuia na kupambana na uhalifu ikiwemo kutoa nakupokea rushwa huyo afande atafanya kazi za PCCB na inapobidi nguvu ya police anatoa maelekezo kwa maofisa wa chini sababu yeye ni COMMISIONER OF POLICE.
 
Sikiliza wewe police ndio wataalam unaongea ujinga tupu,police ni law enforcement agence ambayo anasimamia sheria zote za nchi kwa taarifa yako hiyo PCCB ilikuwa ndani ya police wakatenganisha ni ma nguli wa criminal investigation kwenye nyanja zote na wana power kubwa katika kuzuia na kupambana na uhalifu ikiwemo kutoa nakupokea rushwa huyo afande atafanya kazi za PCCB na inapobidi nguvu ya police anatoa maelekezo kwa maofisa wa chini sababu yeye ni COMMISIONER OF POLICE.
Ujinga Tu,Kwa akili zako fupi unajua Kwa nn ilitenganishwa na police?
 
Kwa Taarifa yako, CP Salum.Hamduni anakuwa Polisi wa Tatu kuiongoza PCCB ,alianza DCP Valentino Mlowola, Akaja CP Diwani Athumani, na Sasa CP Salum Nassor Hamduni.
Yule Brigadier wa Jeshi hakuwa anatosha kabisa pale, No wonder Most of the time akawa anavaa Sare za Jeshi, Combat kutaka ku hide Weaknesses zake
Hivi police unamtemganishaje na Rushwa?
Akili zenu fupi Sana,ndo mana watu wenye IQ kubwa hawaezi weka police Kua wapambana na Rushwa zaidi ya wao wenyewe kuhitaji kupigwa msasa na kupitia mara Kwa mara na Pccb.

Rudisheni akili zenu Sawa Sawa, police Kua Pccb ni Sawa na kesi ya ngedere hakimu nyani.
Hata Huyo Diwani Athumani watu waliongea ndo akang'ofolewa .

Discipline ya jeshi dunia nzima si ya kutiliwa Shaka,hebu geukia upande wa pili wa hao police ndo utajua ufinyu WA akili yako ya kimhemuko
 
bado unaishi gizani sana.

nanyinyi kwa mitazamo hii ndio mnavunja mionyo wachache walioamua kuzifanya kazi hizo kwa haki,mko negative masaa 24.
unadhani polisi hakuna walokole na swala tano wanaomuogopa Mungu??

jikiteni katika kujadili namna ya kuwaboreshea maslahi ili tuwahukumu kwa haki,huko bandarini,takukuru,tra kuna mishahara na watu wanapiga mikunjo sio kizembe,hao polisi mnawalilia kisa buku mbili mbili zà barabarani mnazowapa huku mnawasimanga!!!!
No wonder police 90% ni ngao ya watawala kujifichia maovu Yao na kuwatumia katika kuwaziba midomo wote wanaopingana na unyonyaji na wizi WA viongozi.
Suala la msingi ni police ana legacy gani ya kuchunguza rushwa Hali ya Kua wao ndo wananuka rushwa kila idara?
 
No wonder police 90% ni ngao ya watawala kujifichia maovu Yao na kuwatumia katika kuwaziba midomo wote wanaopingana na unyonyaji na wizi WA viongozi.
Suala la msingi ni police ana legacy gani ya kuchunguza rushwa Hali ya Kua wao ndo wananuka rushwa kila idara?
sasa rushwa ni paka,nani atamfunga kengere??

kama taasisi hamuiamini,watumishi hamuwaamini.
 
Hivi police unamtemganishaje na Rushwa?
Akili zenu fupi Sana,ndo mana watu wenye IQ kubwa hawaezi weka police Kua wapambana na Rushwa zaidi ya wao wenyewe kuhitaji kupigwa msasa na kupitia mara Kwa mara na Pccb.

Rudisheni akili zenu Sawa Sawa, police Kua Pccb ni Sawa na kesi ya ngedere hakimu nyani.
Hata Huyo Diwani Athumani watu waliongea ndo akang'ofolewa .

Discipline ya jeshi dunia nzima si ya kutiliwa Shaka,hebu geukia upande wa pili wa hao police ndo utajua ufinyu WA akili yako ya kimhemuko
Huna akili. Hivyo tu ndivyo ninavyoweza kusema.
 
Huwezi kupambana na rushwa duniani usiwe askari au kupata mafunzo ya kijeshi na ukafanyakazi kwa tija.

Kama wanyama pori tu wanalindwa na askari sembuse binadamu mla rushwa?

Leo hii mnasema polisi wanakula rushwa ambao wamepitia mafunzo ya kijeshi halafu unawategemea takukuru ambao ni raia tu wakapambane na polisi ambao ni askari kweli?

Kupambana na rushwa ni vita na vita inataka weredi,ujasiri,mbinu,ukakamavu,nk.

Mimi napendekeza takukuru iundwe upya kwa kuchanganya askari kutoka majeshi mbalimbali na vyombo vya ulinzi na usalama wapikwe waive waganye kazi kama task force iliyo na lengo kuu siyo kurukaruka.
 
TAKUKURU haiko professional sema tu hawataki kukubali hakuna kiongozi au mtumishi yeyote wa taasisi hiyo mwenye elimu ya maswala ya kupambana na rushwa aliyebobea zaidi ya basic investigation course ambayo haitambuliki kimataifa.

BIC kila mtu anaweza kuwa nayo i.e JKT,POLISI,MAGEREZA,n.k.

Viongozi wengi waliopo huko ni wapiga ramri tu hawana ujuzi wala maono na ni watu wa mwambafai na kukandamiza haki za watu.
Kwanini hawasomeshi watu sasa?
 
Wadau

Nimeona kwa kipindi kirefu Sasa Taasisi ya TAKUKURU inapewa watu kutoka nje kuiongoza. Nina maswali kadhaa,
1. Taasisi hii ina professional discipline? Au wanajiendea endea tu? Maake inaongozwaje na Kila mtu ?
2. Internally ina succession plans? Kama wanayo hao waliotakiwa kuwa katika nafasi husika huwa wanajisikiaje?

3. Hii Taasisi inawezaje kutunza organization culture? Kama Kila muda inapewa mtu mwenye culture tofauti kuiongoza?

Mwisho kwanini wanaoteuwa wanadhani hii Taasisi inaweza kuongozwa na yeyote?

Leo nimekuwa na maswali kuliko majibu
Nilizani unataka kuuliza "Kwanini hawa wala rushwa wanaaminiwa na kupewa kazi ya kupambana na rushwa?"
 
Back
Top Bottom