Wanyamwezi wa Urambo!

Askari Kanzu

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2011
Posts
4,596
Reaction score
1,236
Urambo enzi hizo (1951)!

Iyo staili ya nywele ya uyo jamaa wa kushoto ilikuwa inaitwa "way" yaani nywele ziachane kama za mzungu vile!

Hata enzi hizo miembe ilikuwa mingi. Waafrica wanachimbua tairi wakati wazungu wameshika mikono. Kama inavyokuwa sasa (historia inajirudia)!
 


Gari hizi wakati huo hazikutumia ignition kuliwasha kama siku hizi, magari haya yalikuwa yanawashwa kwa kutumia mtalimbo (handle) kama baadhi ya engine za kuendeshea vinu vya kusaga zinavyowashwa. Handle ilikuwa mbele, hivyo unapowasha hakikisha umeweka kurungu cha gear (gear transfer) kwenye neutral, vinginevyo likishawaka linakuparamia. Tekinologia hadi kufikia tulipo imetoka mbali na wengine hata hatuju magari wakati wanapata uhuru waliwashaje kumbe ni kwa handle.
 
THis is one of the classics I have seen this year!!! Thanks Candid Scope
 
huo mji nao hauchange! nimetoka huko juzi yaani upo vile vile.......
 
huyo jamaa mwenye ''way'' atakuwa amesoma ndiye ameelimika...kavaa na saa mkononi amesimama kwa poz,mkono mfukoni tabasamu kwa mbali
 
Hapo ni ngoma ya maswezi huko Urambo (1951). Kabla ya ngoma kwanza hao wa-maswezi wanakunywa pombe ya kienyeji kupandisha stimu. Khanga zilikuwepo hata kabla ya Uhuru.
Stesheni ya treni ya Urambo (1951). Asali kwa wingii sehemu hizo!!!
 
Miafrika imezoea kutawaliwa kila siku tutakuwa Watu wa kutawaliwa mpaka mwisho wa dunia. MIAFRIKA BWANA NDIVYO ILIVYO
 


maskini wazee wetu, hapa ktk huu umati sijui ni wangapi mpaka sasa bado wapo duniani

mkoloni alivyoiacha hii reli 1950s na mpaka sasa ipo hivyo hivyo hata hilo jengo, sema uchafu tu sasa hivi ndio umeongezeka
 
Jamani wa kwanza kushoto kapiga mkono dizaini kaubetua ili saa ionekane,ndo ilikuwa za zamani zile. Askari Kanzu big up sana kwa hii kitu
 

Hapo utagundua kuna maeneo Tanzania haipigia hatua. Mwaka jana nilipita hapo stesheni yaani panafanana hivihivi. Hakuna mabadiliko yeyote.

Hata ndani bado mambo yaleyale ya zamani hata compyuta hamna
 
Kuna baadhi ya gari mpaka leo zipo japo zina ignition kama landrover 109 ikigoma kupiga unazungusha handle badala ya kuomba watu wakusukume
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…