juzi alhamis kamati ya fedha ya bunge,ambayo mimi ni mjumbe, ilimwagiza waziri wa fedha kuondoa asilimia 15 kutoka katika bajeti ya matumizi mengineyo na kupeleka pesa yote kujenga barabara.
Hii ilifuatia taarifa tuliyopata kutoka kamati ya miundombinu kuwa hakuna barabara mpya zitakazojengwa maana pesa zilizotengwa ni kidogo. Uamuzi huu wa kamati ya bunge utaongeza bajeti ya miuondombinu kwa zaidi shs 393 bilions.
Uamuzi huu wa kamati ya bunge unaonesha kuwa hata tanzania tunaouwezo wa kupunguza gharama na kupeleka pesa katika vipaumbele muhimu. Mfanowa mauritania ni mzuri sana. Lakini tanzania waziri analipwa dola 1100 tu, theluthi tu ya malipo ya waziri wa mauritania, nchi masikini kuliko tanzania