Wanawake ziiii...

Gor

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
2,791
Reaction score
850
Leo ni siku ya wanawake duniani kabla ya kwenda sana kwanza fikiria "siku ya wanawake." Si nia yangu kuwakandia but hoja yangu ni vita vya kipumbavu wanayopigana na jinsia ya kiume.

Ukiwasikiliza kwa makini utagundua kuwa adui yao mkuu ni mwanamme na si vinginevyo itakuwa vigumu kushinda nature ninacho kiona wanawake wanakwepa asili yao,wanakimbia majukumu yao,asili ya umbile yao itawahukumu na daima hawatashinda vita hiyo maana hawajamjua adui yao ni nani,adui yao ni wao wenyewe kwa tabia zao za asili,maumbile yao na kiasili kinachowafanya wawe jike mwanamme sio adui yao.

Mfano mzuri ni kwamba mtoto wa kike anaye kimbia malezi ya wazazi kisha anakwenda kujiunga na maisha yasio fuatiliwa na wazazi kisha anapata mimba,hivi then ana kuja kulaumu nimebakwa,nimekimbiwa na kutelekezwa!Hapa ndipo palipo na upumbavu mtoto wa kike lazima ajijue yeye ni mtoto wa kike na apambane ni kike kike maana mfumo unaruhusu.

Sasa wanapojiona nao ni dume basi hapo tujue hakuna familia matokeo yake tutapata watoto wengi wa mitaani kisha jamii katili na isiyo na elimu na maskini asili yao ndio aweza kuwa adui yao mkuu mwanamke ndiye mwenye nyonyo ya kumnyonyesha mtoto but anaacha kumnyonyesha mtoto ili ziwa iwe still!,mtoto kadogo anaachiwa house girl amtunze binadamu ni mnyama na wanawake wakitaka kwenda mbele warudi kwenye asili yao kwa Hawa kuwa

Adamu hawataweza.Adui yenu ni kiasili chenu
 
WE WAACHE WADANGANYWE wataisoma kimyakimya, hizi ni sera za kimagharibi ambazo walizianzisha zilipowashinda wakaona wazitupie Afrika na sisi kwa kuwa hatuna desturi za kujiuliza juu ya kile tunacholetewa tumeingia wazimawazima na kuanndamanna eti 50kwa50, hivi ninyi wanawake ndio kusema hata uwezo wenu wa kufikilia pia mmekabidhi wengine?
 
Rais wa Afrika Kusini, kasema jambo nao washaanza kuja juu, kiufupi muda sio mrefu, watakuwa sawa nasi wanaume.

Yaani hawasemwi hata kidogo, ukiwasema tu, HAKI ZA BINADAMU zitakuhusu. Ila ndio Mama zetu hawa. Binafsi nawaheshimu kweli na kuwapenda juu.

Ahsante!
 
Mimi siku hizi wala sina ubishi tena, hata wakati tunacheza mechi na kufungana magoli akitaka kuwa juu namruhusu, natuma mishale kutoka chini kwenda angani
Ha ha ha haaa...umenichekesha sanaa.
 
who run the world? We run this mother earth
 
wanawake wanaiendesha hii dunia ....ila iliumbwa kwa mfumo dume period
 
Wanawake wanapopigania haki zao,wanapigania usawa jinsi raslimali zinavyotumika bila kuzingatia mahusiano ya kijinsia na wala si mgawanyo wa majukumu kwa kuzingatia majukumu ya jinsi ya kiume na ya kike.Mgawanyo wa wa majukumu kwa mujibu wa jinsi hakuna mwanamke anayekataa,mfano kubeba mimba na kujifungua ni majukumu ya jinsi ta kike,lakini kupika,kufagia sio mgawanyo kwa mujibu wa jinsi ya mtu,kwamba kupika ni kazi za wanawake,kwamba wanaume waende shule wanawake wabaki majumbani sio mgawanyo kwa mujibu wa jinsi ya mtu,ni fikra za kimila basi
 
Siyo kwa ubaya:

*Aliumbwa mwanadamu kwa mfano wake yeye (Mungu). Huyo mwanadamu ni Adam, Adam ni mwanume.
* Alishi kwa muda mrefu sana ndani ya bustani ya Eden, na kutawala vyote vilivyo angani, aridhini na majini. Kwa maana dunia ilikuwa inaendeshwa/ kuongozwa na mwanaume.
* Baadae sana akaletwa msaidizi kutoka kwenye ubavu wake yeye Adam, akaitwa Eve. Ambae ni mwanamke.

Wacheni wanawake wafanye wanavyotaka au wanachotaka, wala msishindane nao... lakini dunia hii inaendeshwa ki-mfumo dume daima na milele.
 
adui wa mwanamke ni mwanamke mwenyewe wanawake wakitambua hilo wala hawatapigania mambo ya usawa kwani kama wapiga kura wengi ni wanawake kwanini wang'ang'ania viti vya upendeleo.
Jana nimewasikia wakiongea wanawake wenye mafanikio mnaweza kujiita wenye mafanikio wakati wanawake wengi bado wanaishi maisha duni,wananyanyasika ndio hii inaonyesha ubaguzi wa wao kwa wao kwani tayari wamejenga tabaka kuwa kuna wanawake wenye mafanikio na wasio na mafanikio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…