Wanawake wa makanisa ya kilokole

Wanawake wa makanisa ya kilokole

Nadhani shida inaanza pale mtu anashindwa kutofautisha majukumu yake, mtu ana familia lakini ni kushinda na kulala kanisani, mikesha isiyoisha, kipato chote kinaishia kanisani.

Lazima ndoa iwe na matatizo tu!!!
 
Habarini wadau,

Wale wanaume ambao ni waumini wa Katoliki au Lutheran ambao waliwahi kupata wachumba kutoka haya makanisa ya kilokole,ni changamoto gani mlipata kutoka kwa hawa wapendwa?

Angalizo: Kutotoa Tunda kabla ya Ndoa sio changamoto.
Hawa wanawake wa kilokole inategemea ni mlokole wa aina Gani. Wapo makundi makuu mawili waliozaliwa kwenye ulokole akalelewa akakulia humo au aliyeokaka kwa hiyari yake au kwa yaliyomsibu kama mapepo na matatizo mengineyo ikiwemo ya ndoa na hata kupata mume. Sasa hawa waliokoka ukubwani ndo shida kwanza Balaa lake hawana msimamo kabhisa hawa kukuche kuwe usiku ni kutanga makanisani hadi inafikia hajui anasali wapi maana Ataenda sijui Efata, Atoke Aend FPCT ,atoke afike hadi kwa mashahidi wa Yehove yaan hawajisomi kabhisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanajua kila kitu,wabishi afu mama na baba mchungaji ndie huwapangia ratiba ya kila Siku,,,,,by the way humu hawapo wanaamini ni dhambi [emoji1] [emoji1]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanawaamini manabii wao feki kupita mtu Yeyote. Ukiwa naye elewa utaishi kwa instructions za nabii wake... Pili kila jambo negative or challenge wanakemea wanadhani ni pepo kumbe Vingine ni akili tu za kawaida kuelewa. Tatu wako tayari kujinyima na hata kukopa ili mradi tu ampe nabii wake..pia wanapenda umbea Sana na kuona watu wengine niwadhambi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimebahatika kukutana na mabinti wa kilokole walio wazuri, wema, wacha Mungu kweli na wanaojua thamani yao kama mabinti, kama wanawake na kama wazazi.

Sikatai kuna exception lakini naona wasichana wengi wa kilokole au wenye kumcha Mungu hujitahidi kukaa mbali na dhambi kuliko amabye si mcha Mungu.

Mambo yasiwe mengi, mengi yasiwe mambo
 
Kwanza elewa mademu wengi hua wanaenda kwenye ulokole kutafuta mabwana. Wanaamini kwamba kule ni rahisi kupata mume kwahiyo hawakogi siriaz kiviiile labda wachache sana ndio hufuata maombi. Kwahiyo wanalika tu hawanaga shida..
 
Kwenda kukesha kanisani siku 3 kwa kila wiki huku akimuacha mume mnara unasoma 4G kitandani.
Ila turudi nyuma twende mbele, Lazima wajue kutofautisha majukumu ya kanisani na Majukumu ya Mume familia... Haiwezekani amuache Mme wake kitandani au nyumbani halafu yeye akakeshe wiki nzima...

Najua atasema anaingiliwa kiimani lakini kuna vitu vingine vikiendekezwa inakuwa too much na itakuwa tabia yake usiporekebisha
 
Back
Top Bottom