Judithkaunda
Member
- Aug 21, 2022
- 90
- 228
Hii ndiyo dunia niliyoambiwa kuwa uyaone!
Wakati wengine wakikesha kwenye ibada na kwenye vilinge vya waganga kutafuta ndoa, wengine ndoa zimewashinda wanatamani kuachika.
Lakini wanawake tuache ubinafsi!
Wakati unafikilia kuachana na mumeo unajifikilia mwenyewe tu, "Nikitoka hapa nikapange chumba nifanye kazi niishi maisha yangu mazuri au nitakwenda kuishi kwa bwana angu mwenye uwezo nikale bata (kuenjoy)." Hivi umeshafikilia wakati huo mtoto/watoto wako watakuwa kwenye mazingira gani? Vaa viatu vya mtoto wako halafu fikiria ungekuwa ni wewe ukapewa nafasi ya kuchagua unapotaka kuishi, ungechagua wapi?
▪️Ukaishi kwa bibi na babu.
▪️Ukaishi kwa ndugu.
▪️Ukaishi na mama bila baba.
▪️Ukaishi na baba na mama wa kambo au,
▪️ Uendelee kuishi na baba na mama yako.
Ni wapi ungechagua?
Wote tunajua nyumbani ni nyumbani haijalishi pakoje na mcheza kwao hutunzwa. Nia yangu unielewe kwamba hapo ndipo nyumbani kwao mwanao, hiyo ndiyo sehemu yake ya kujidai.
Tuache kuwaadhibu watoto wetu kwamakosa ya baba zao, ni kweli unaweza kumlea mwenyewe lakini anahitaji uwepo wake haijalishi baba yake yukoje, hata kama mlimpata kwa bahati mbaya, siyo kosa lake usimnyime haki mwanao.
Ni kweli anaweza akawa si mume mzuri lakini akawa baba bora kwa mwanao. Dunia imechafuka na matukio ya kikatili yameongezeka, hata wajomba siku hizi hawaaminiki, hivi utakuwa na amani ukiwa mbali naye?
Kama tatizo ni mume kuwa na wanawake wengine hilo ni tatizo la wanaume wengi, wameumbiwa tamaa lakini haimaanishi hakupendi. Huoni kama ni bahati katika wanawake wote kachagua kukuoa wewe, hata wewe ni shahidi siyo kwamba wewe ni mrembo sana lakini anaijua thamani yako na kwanini uko hapo.
Ndiyo maana pamoja na yeye kukusaliti lakini mkiachana wewe ndiyo umevunja ndoa yako kwasababu maamuzi yanatoka kwako. Wakati wewe unahisi mateso kuwa hapo, huwezi kuamini kuna wenzako wanatamani hiyo nafasi, wanasubili tu utikise kiberiti dada kitakulipukia.
Ni kweli wanaume wazuri wako wengi sana, lakini waoaji ni wachache mno. Tulia dada mlee watoto wenu, kama ni kazi au biashara anzia hapo ulipo. Usivunje mji wako wafikilie wanao.
Wakati wengine wakikesha kwenye ibada na kwenye vilinge vya waganga kutafuta ndoa, wengine ndoa zimewashinda wanatamani kuachika.
Lakini wanawake tuache ubinafsi!
Wakati unafikilia kuachana na mumeo unajifikilia mwenyewe tu, "Nikitoka hapa nikapange chumba nifanye kazi niishi maisha yangu mazuri au nitakwenda kuishi kwa bwana angu mwenye uwezo nikale bata (kuenjoy)." Hivi umeshafikilia wakati huo mtoto/watoto wako watakuwa kwenye mazingira gani? Vaa viatu vya mtoto wako halafu fikiria ungekuwa ni wewe ukapewa nafasi ya kuchagua unapotaka kuishi, ungechagua wapi?
▪️Ukaishi kwa bibi na babu.
▪️Ukaishi kwa ndugu.
▪️Ukaishi na mama bila baba.
▪️Ukaishi na baba na mama wa kambo au,
▪️ Uendelee kuishi na baba na mama yako.
Ni wapi ungechagua?
Wote tunajua nyumbani ni nyumbani haijalishi pakoje na mcheza kwao hutunzwa. Nia yangu unielewe kwamba hapo ndipo nyumbani kwao mwanao, hiyo ndiyo sehemu yake ya kujidai.
Tuache kuwaadhibu watoto wetu kwamakosa ya baba zao, ni kweli unaweza kumlea mwenyewe lakini anahitaji uwepo wake haijalishi baba yake yukoje, hata kama mlimpata kwa bahati mbaya, siyo kosa lake usimnyime haki mwanao.
Ni kweli anaweza akawa si mume mzuri lakini akawa baba bora kwa mwanao. Dunia imechafuka na matukio ya kikatili yameongezeka, hata wajomba siku hizi hawaaminiki, hivi utakuwa na amani ukiwa mbali naye?
Kama tatizo ni mume kuwa na wanawake wengine hilo ni tatizo la wanaume wengi, wameumbiwa tamaa lakini haimaanishi hakupendi. Huoni kama ni bahati katika wanawake wote kachagua kukuoa wewe, hata wewe ni shahidi siyo kwamba wewe ni mrembo sana lakini anaijua thamani yako na kwanini uko hapo.
Ndiyo maana pamoja na yeye kukusaliti lakini mkiachana wewe ndiyo umevunja ndoa yako kwasababu maamuzi yanatoka kwako. Wakati wewe unahisi mateso kuwa hapo, huwezi kuamini kuna wenzako wanatamani hiyo nafasi, wanasubili tu utikise kiberiti dada kitakulipukia.
Ni kweli wanaume wazuri wako wengi sana, lakini waoaji ni wachache mno. Tulia dada mlee watoto wenu, kama ni kazi au biashara anzia hapo ulipo. Usivunje mji wako wafikilie wanao.