Wanawake ni viumbe waongo sana, sijui ni kwa nini hawako wazi…!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,809
15,410
i-always-wanted-to-ask-ep4-600x337.jpg


Haya ni malalamiko ya wanaume kila wakati. Je kuna ukweli wowote kwenye malalamiko hayo?

Huende upo, kutokana na tafiti za hivi karibuni na zile zinazoendelea kufanywa, kuhusu jambo hilo.

Tafiti nyingi hadi sasa zimeonesha kwamba, wanawake wanane katika kila kumi husema uongo ambao, lengo lake ni kulinda uhusiano au kujihami ili wanaume wasiwabughudhi. Siyo kusema uongo tu, bali wanawake tisa katika kila kumi, wanaamini kwamba, uongo huo ambao unafahamika kama, ‘uongo mweupe,' ni muhimu kusemwa.

Moja ya tafiti hizo, ni ule uliofanywa na Midway Games, ambao ulionesha kwamba, ni wanaume sita tu katika kumi wanaosema uongo huo ambao hupatikana miongoni mwa watu walio katika uhusiano, yaani mke na mume au hawara.

Inawezekana kwamba, ni kutokana na maumbile ya wanawake kuwa ni watu wanaogusika na kutumia hisia zaidi, ambapo wamejikuta wakiwa wa sanaa hiyo ya kusema uongo ili kujihami. Kwa kawaida uongo wanaousema ni ule unaohusu uhusiano.

Wanawake husema uongo mwingi kuhusu maisha yao ya kiuhusiano, huwadanganya wanaume au wapenzi wao katika mambo ambayo mtu asingetarajiwa kudanganya, uongo ambao hata hivyo, hauna madhara. Lakini pia imebainika kwamba, wanawake huwa hawakubali moja kwa moja sifa wanazostahili pale wanapopewa sifa hizo. Badala ya kusema asante, wataongeza kusema, ‘ni kawaida tu.'

Kwa kawaida wanawake wana sifa ya kusema uongo ambao huwafanya wanaume kushangaa. Jambo linalosemewa uongo huo, kwa kawaida hata kama lingesemwa katika ukweli, lisingebadili chochote, lakini unakuta limesemewa uongo.

Kwa hiyo kwa kusema uongo, inaweza kuwa ni njia bora zaidi kwa mwanamke katika kujitetea. Bila kujali maumbile, ni kwamba, kwa kiasi fulani mwanamke anatakiwa kusema uongo japo kidogo kuliko mwanaume…….

Copy to: Madame B, Paloma, amu, gfsonwin, cacico, Kipaji Halisi, KakaKiiza, Asprin, figganigga, Ruttashobolwa, ladyfurahia, Nivea, Lisa, Lady doctor, Mrembo by Nature, Swts, Binti.com, kisukari, farkhina FP, na Kipipi, Asnam, snowhite nawapa salaam nyingi sana kutoka Arusha, jana nilipata mapokezi mazuri sana kutoka kwa wadau wa Arusha wing. Walikuwepo kina Arushaone, PakaJimmy, Mzee wa Rula, marejesho, Erickb52, LiverpoolFC, Filipo na wengine ambao siwakumbuki maana walipokuja walishanikuta nimezimika kwa Contensa Rum na Govinder Kumar Brandy.....

Watu wa Arusha Wing ni wabaya sana....
 
na sie wanawake ni wajinga kwanini tukubali kudanganywa hatuchekechi maneno.
Nivea nyie ndio mlianza kutudanganya pale kwenye Bustani ya Eden mpaka tukala tunda la mti wa kati kati ambao Mungu alituasa tusiuguse..
Nyie mmetuletea balaa mpaka sasa tunakula kwa jasho na tunataabika ili kuwashawishi...... LOL
 
Last edited by a moderator:
Ndugu Yao Eve na Dalillah.....huwasishindani nao hawa. Hua nikianza kuuliza jambo Tu nikipata jibu lolote lile hukaaa kimya.
 
BBC walishafanyaga utafiti kabisa wakathibitisha kwa data wanawake ni waongo zaidi kuliko wanaume. Kwa hiyo mkiwa pale coffee bar Mlimani City akawa anamponda saaana Asumani think twice! ha ha ha ....

i-always-wanted-to-ask-ep4-600x337.jpg


Haya ni malalamiko ya wanaume kila wakati. Je kuna ukweli wowote kwenye malalamiko hayo?

Huende upo, kutokana na tafiti za hivi karibuni na zile zinazoendelea kufanywa, kuhusu jambo hilo.

Tafiti nyingi hadi sasa zimeonesha kwamba, wanawake wanane katika kila kumi husema uongo ambao, lengo lake ni kulinda uhusiano au kujihami ili wanaume wasiwabughudhi. Siyo kusema uongo tu, bali wanawake tisa katika kila kumi, wanaamini kwamba, uongo huo ambao unafahamika kama, ‘uongo mweupe,’ ni muhimu kusemwa.

Moja ya tafiti hizo, ni ule uliofanywa na Midway Games, ambao ulionesha kwamba, ni wanaume sita tu katika kumi wanaosema uongo huo ambao hupatikana miongoni mwa watu walio katika uhusiano, yaani mke na mume au hawara.

Inawezekana kwamba, ni kutokana na maumbile ya wanawake kuwa ni watu wanaogusika na kutumia hisia zaidi, ambapo wamejikuta wakiwa wa sanaa hiyo ya kusema uongo ili kujihami. Kwa kawaida uongo wanaousema ni ule unaohusu uhusiano.

Wanawake husema uongo mwingi kuhusu maisha yao ya kiuhusiano, huwadanganya wanaume au wapenzi wao katika mambo ambayo mtu asingetarajiwa kudanganya, uongo ambao hata hivyo, hauna madhara. Lakini pia imebainika kwamba, wanawake huwa hawakubali moja kwa moja sifa wanazostahili pale wanapopewa sifa hizo. Badala ya kusema asante, wataongeza kusema, ‘ni kawaida tu.’

Kwa kawaida wanawake wana sifa ya kusema uongo ambao huwafanya wanaume kushangaa. Jambo linalosemewa uongo huo, kwa kawaida hata kama lingesemwa katika ukweli, lisingebadili chochote, lakini unakuta limesemewa uongo.

Kwa hiyo kwa kusema uongo, inaweza kuwa ni njia bora zaidi kwa mwanamke katika kujitetea. Bila kujali maumbile, ni kwamba, kwa kiasi fulani mwanamke anatakiwa kusema uongo japo kidogo kuliko mwanaume…….

Copy to: Madame B, Paloma, amu, gfsonwin, cacico, Kipaji Halisi, KakaKiiza, Asprin, figganigga, Ruttashobolwa, ladyfurahia, Nivea, Lisa, Lady doctor, Mrembo by Nature, Swts, Binti.com, kisukari, farkhina FP, na Kipipi, Asnam, snowhite nawapa salaam nyingi sana kutoka Arusha, jana nilipata mapokezi mazuri sana kutoka kwa wadau wa Arusha wing. Walikuwepo kina Arushaone, PakaJimmy, Mzee wa Rula, marejesho, Erickb52, LiverpoolFC, Filipo na wengine ambao siwakumbuki maana walipokuja walishanikuta nimezimika kwa Contensa Rum na Govinder Kumar Brandy.....

Watu wa Arusha Wing ni wabaya sana....
 
BBC walishafanyaga utafiti kabisa wakathibitisha kwa data wanawake ni waongo zaidi kuliko wanaume. Kwa hiyo mkiwa pale coffee bar Mlimani City akawa anamponda saaana Asumani think twice! ha ha ha ....
Kweli aisee, umenikumbusha jinsi Madame B, amu na Paloma wanavyonidanganyaga...... LOL

Nimeishia kuchezewa sharubu na uzee huu
 
Last edited by a moderator:

hahahaaa!!walikuzimisha aisee
wish ningekuepo duuuh!!
wanaume mmetuzidi uongo
hata wewe shahidi Mtambuzi!!
 
Last edited by a moderator:
Mtambuzi,
uwongo mzuri ni ule wenye faida na uwongo mbaya ni ule wenye kuleta hasara.
Wanaume zetu hawa,bila uwongo hawafungui wallet ng'oo.
 
Last edited by a moderator:
wanaongooza kwa uongo duniani ni wanaume tena ni matapeli wa kutupwa na ni waongo waliokubuhu na mmojawapo ni wewe mwenyewe Mtambuzi

Na wewe usije ukaacha nikasema, siku zile uliponidanganya pale LEO TUPO HAPA PUB...
Kwa si ni wewe ulioniambia kuwa umempiga chini Mentor kwa sababu ametoka na Lady doctor... Kumbe ulikuwa unanidanganya mwayego kwapani umemtia hapumuwi kijana wa watu wa Kichaga
 
Last edited by a moderator:
Ukweli siku zote unauma na sisi hatutaki kuumia wala kumuumiza mtu has a pale tullipopenda with hope kuwa tulichodanganya hakitajulikana that's y we lie
 
Kweli aisee, umenikumbusha jinsi Madame B, amu na Paloma wanavyonidanganyaga...... LOL

Nimeishia kuchezewa sharubu na uzee huu

Hahaha!
Unatoa siri zako sasa.
Tulitaka tukuchune tu.
Si unajua ulikutana na watoto wa mjini.
Nasi tulitaka tukuoneshe kuwa sie ni akina "Born here here!!!".
 
Last edited by a moderator:
Mtambuzi,
uwongo mzuri ni ule wenye faida na uwongo mbaya ni ule wenye kuleta hasara.
Wanaume zetu hawa,bila uwongo hawafungui wallet ng'oo.
N kweli maana mie sio kufungua bali nimelielekeza kabisa, mpaka leo hata sijui wallet langu nimelitelekezea wapi.....
 
^^
Usinikumbushe VC Mtambuzi niliwahi kudanganywa jambo mpaka leo mwanamke hata aseme nini ntasikiliza tu siku ipite.
^^
 
Last edited by a moderator:
N kweli maana mie sio kufungua bali nimelielekeza kabisa, mpaka leo hata sijui wallet langu nimelitelekezea wapi.....

Wallet yako uliiacha sebleni kwangu.
Ila nimefungua hakuna kitu, njoo ulifate.
Au nitampa amu.
Hahaha! Mtambuzi mpaka usahau wallet kwa mwanamke,basi huyo kaongeza na vya kwa babu Bagamoyo.
Wanaume na wallet utadhani wamezaliwa nazo.
 
Last edited by a moderator:
Last edited by a moderator:
Kweli itakuweka huru,wanaume wasemao ukweli ni watu wa mipango na bajeti na wanafuata maadili ya ki-Mungu huwa ni vigumu kupata mwenza maana idadi kubwa wa wanawake wanapenda kudunganywa sababu shetani anawatawala kwa haraka zaid kulipo wanaume ndiyo maana wengi ni waongo si wasema ukweli.
 
yani mm kwa kinywa changu na mdomo wangu na akili na ufahamu na usomi wangu wote huu nikudanganye wewe, ati nitake radhi bhana naona unataka kuchafua hali ya anga na hewa hii ya cc
Na wewe usije ukaacha nikasema, siku zile uliponidanganya pale LEO TUPO HAPA PUB...
Kwa si ni wewe ulioniambia kuwa umempiga chini Mentor kwa sababu ametoka na Lady doctor... Kumbe ulikuwa unanidanganya mwayego kwapani umemtia hapumuwi kijana wa watu wa Kichaga
 
yani umeanza vizuri kwa point ila mwishoni umeniboa na kunikera sana nyie ndo mnaongoza kwa uongo na utapeli uliokithiri na kubuhu inabidi mwombe Mungu awasemehe na mtubu kwa dhambi ya uongo wenu ambao umefanya hata Taifa kudidimia ona sasa mnataka kumleta Rais Obama hapa wa nini na kazi gani kama sio kutuibia na kutunyang'anya mali zetu, ni mnatuficha kwa mgongo wa chupa huku mkisema hakuna kitu anakuja kusalimia, kumbe mna lo jambo lenu sasa huo si uongo wa kwa wananchi wa tz?[QUOTE=Deiman;6650445]Kweli itakuweka huru,wanaume wasemao ukweli ni watu wa mipango na bajeti na wanafuata maadili ya ki-Mungu huwa ni vigumu kupata mwenza maana idadi kubwa wa wanawake wanapenda kudunganywa sababu shetani anawatawala kwa haraka zaid kulipo wanaume ndiyo maana wengi ni waongo si wasema ukweli.[/QUOTE]
 
Back
Top Bottom