Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,410
Haya ni malalamiko ya wanaume kila wakati. Je kuna ukweli wowote kwenye malalamiko hayo?
Huende upo, kutokana na tafiti za hivi karibuni na zile zinazoendelea kufanywa, kuhusu jambo hilo.
Tafiti nyingi hadi sasa zimeonesha kwamba, wanawake wanane katika kila kumi husema uongo ambao, lengo lake ni kulinda uhusiano au kujihami ili wanaume wasiwabughudhi. Siyo kusema uongo tu, bali wanawake tisa katika kila kumi, wanaamini kwamba, uongo huo ambao unafahamika kama, ‘uongo mweupe,' ni muhimu kusemwa.
Moja ya tafiti hizo, ni ule uliofanywa na Midway Games, ambao ulionesha kwamba, ni wanaume sita tu katika kumi wanaosema uongo huo ambao hupatikana miongoni mwa watu walio katika uhusiano, yaani mke na mume au hawara.
Inawezekana kwamba, ni kutokana na maumbile ya wanawake kuwa ni watu wanaogusika na kutumia hisia zaidi, ambapo wamejikuta wakiwa wa sanaa hiyo ya kusema uongo ili kujihami. Kwa kawaida uongo wanaousema ni ule unaohusu uhusiano.
Wanawake husema uongo mwingi kuhusu maisha yao ya kiuhusiano, huwadanganya wanaume au wapenzi wao katika mambo ambayo mtu asingetarajiwa kudanganya, uongo ambao hata hivyo, hauna madhara. Lakini pia imebainika kwamba, wanawake huwa hawakubali moja kwa moja sifa wanazostahili pale wanapopewa sifa hizo. Badala ya kusema asante, wataongeza kusema, ‘ni kawaida tu.'
Kwa kawaida wanawake wana sifa ya kusema uongo ambao huwafanya wanaume kushangaa. Jambo linalosemewa uongo huo, kwa kawaida hata kama lingesemwa katika ukweli, lisingebadili chochote, lakini unakuta limesemewa uongo.
Kwa hiyo kwa kusema uongo, inaweza kuwa ni njia bora zaidi kwa mwanamke katika kujitetea. Bila kujali maumbile, ni kwamba, kwa kiasi fulani mwanamke anatakiwa kusema uongo japo kidogo kuliko mwanaume…….
Copy to: Madame B, Paloma, amu, gfsonwin, cacico, Kipaji Halisi, KakaKiiza, Asprin, figganigga, Ruttashobolwa, ladyfurahia, Nivea, Lisa, Lady doctor, Mrembo by Nature, Swts, Binti.com, kisukari, farkhina FP, na Kipipi, Asnam, snowhite nawapa salaam nyingi sana kutoka Arusha, jana nilipata mapokezi mazuri sana kutoka kwa wadau wa Arusha wing. Walikuwepo kina Arushaone, PakaJimmy, Mzee wa Rula, marejesho, Erickb52, LiverpoolFC, Filipo na wengine ambao siwakumbuki maana walipokuja walishanikuta nimezimika kwa Contensa Rum na Govinder Kumar Brandy.....
Watu wa Arusha Wing ni wabaya sana....