Amicus Curiae
JF-Expert Member
- Sep 12, 2012
- 5,352
- 7,662
Nimeisikia hii mahali nikaona sio vibaya nikawamegea siri wanaume wenzangu hasa ambao mko/mnaishi kwenye ndoa halisi au ambao mnaishi kwenye misingi ya dhana ya ndoa kwa maana ya 'presumption of marriage' (wale wanasheria mtakua mnanielewa).
Kuna jamaa alikua kwenye ndoa kumbe mke wake akawa anajenga nyumba kisirisiri; yaani alinunua kiwanja kwa siri na kuanza kujenga bila mume wake kujua.
Nyumba ilipoisha mwanamke akamshawishi mumewe wahame kwenye nyumba ya awali waliyokua wanaishi wahamie kwenye nyumba ya mke, wakati huo mume hajui kwamba nyumba ni ya mke.
Mume akaridhia, mwanamke akamtafuta 'mwenye nyumba' wa magumashi kwenye nyumba yake. Mume wake akaongea na huyo mwenye nyumba wa magumashi kuhusu kodi wakakubaliana, mume na mke wakahamia na mume akaanza kulipa kodi kwa mwenye nyumba wa magumashi bila mume wake kujua kwamba anamlipa kodi mke wake!!!
Kilichoendelea baada ya mwanaume kugundua sitakiongelea hapa
.
Ninyi wanawake muwe na huruma jamani...
Kuna jamaa alikua kwenye ndoa kumbe mke wake akawa anajenga nyumba kisirisiri; yaani alinunua kiwanja kwa siri na kuanza kujenga bila mume wake kujua.
Nyumba ilipoisha mwanamke akamshawishi mumewe wahame kwenye nyumba ya awali waliyokua wanaishi wahamie kwenye nyumba ya mke, wakati huo mume hajui kwamba nyumba ni ya mke.
Mume akaridhia, mwanamke akamtafuta 'mwenye nyumba' wa magumashi kwenye nyumba yake. Mume wake akaongea na huyo mwenye nyumba wa magumashi kuhusu kodi wakakubaliana, mume na mke wakahamia na mume akaanza kulipa kodi kwa mwenye nyumba wa magumashi bila mume wake kujua kwamba anamlipa kodi mke wake!!!
Kilichoendelea baada ya mwanaume kugundua sitakiongelea hapa
.Ninyi wanawake muwe na huruma jamani...

