Wanawake: Nahitaji ufafanuzi wenu katika jambo hili……..!

Sijui huwa mnapata muda wa kusoma na kuchanganua kabla ya kutuma post kwa ushabiki. Nilipoongelea suala la kuosha sufuria ni mfano lakini nikauweka katika mazingira ya nyumba ya kupanga uswazi, nakuuliza utajisikia raha mumeo akisugua masufuria nje uani kavaa kaptura anasugua ukoko kwa mchanga nawe mkewe upo tena si mgonjwa? Ukinijibu hapo nitajua naongea na mwanamke gani. Otherwise mie nitajisikia vibaya sana na aibu kubwa siku nitakayomkuta mke wangu yupo darini anahangaika kufix waya za umeme labda awe ndo kazi zake. Au mke yupo busy kusimamia mafundi wanapofyatua matofali, lazima nitamuomba akapumzike nimsaidie hata hivyo nikusahihishe kuwa mke wangu hata bei ya kitasa cha mlango hajui, anachofahamu ni kunipa report kuwa kitasa kimeharibika. Kitasa kipi ni durable ye hajui ni kazi yangu. Kumbuka kama ni nyumba, gypsum nimepiga mwenyewe na fundi yeye alishangaa kwani anadhani najua sheria tu, hata gari kumwaga oil sijawahi kupeleka kwa fundi spanner ninazo ndugu yangu. Am a man by nature not by birth!
\
Bondspot nafaham kuwa wewe ulikuwa unatolea mfano tu na mimi nikaupeleka kama mfano tu kwani yote ni katika hali ya kujenga na kuelimishana tu. Binafsi sidhan kama kuna mama atakaa ndani amwache mumewe aoshe vyombo nje mwanamke wa kiafrika kam hakuna sababu ya msingi kama vile ugonjwa.

pia siyo kweli kwamba mwanamke hawez kusaidia kwenye majukumu mengine hata kama ni ya baba, mfano dhahiri huwa napenda mume wangu anshirikishe hata kwenye majukumu yake mathalan tunajenga basi niende naye kununua ama kuchagua vifaa vya ujenzi na siyo aende peke yake. Hata kuniambia nenda site kasimamie ujenzi pia najiskia fahari kuwa moyo wa mume wangu unaniamin kiasi cha kunituma kwenye jukumu kubwa kama hilo so to me collaboration ni muhimu sana ndani ya familia na wala siyo kuweka mgawanyo wa kazi wa kinyonyaji.
 
Last edited by a moderator:
black-couple-arguing1.jpg

Picha hii haihusiani na habari hii

Hivi inakuwaje?


Baadhi ya wanawake wanapowafanyia waume au wapenzi wao jambo zuri, hufanya hivyo huku wakihesabu na kutarajia wapenzi hao waone, watambue na pengine baadae kuwalipa kwa njia nyingine.

Kwa mfano.

Mke ana kawaida ya kumuwekea mume au mpenzi wake maji ya kuoga bafuni, anamwandalia chakula vizuri, anamnyooshea nguo zake au anazikagua nguo zake kwa umakini na kuzirekebisha pale zinapokuwa na kasoro na mengine yanayofanana na hayo. Badala ya kuchukulia au kujua kwamba huo ni wajibu wake, hufanya hivyo kama deni.

Mume anapomkosea, mke huacha kufanya au kumfanyia mumewe mambo hayo kwa maelezo kwamba, haoni sababu ya kufanya hivyo kwa sababu mumewe hana shukurani…………..

Nimekuwa nikisikia malalamiko mengi kutoka kwa baadhi ya wanaume wenzangu wakilalamikia jambo hili, na wanadai kwamba kwa upande wao hata wanapoudhiwa na wake zao kamwe hawasitishi utaratibu wao wa kuacha kodi ya meza lakini wanawake zao huwasulubu kweli kweli wanapoawakosea.

Hebu fungukeni hapa ili tujue namna nzuri ya kuwa-handle…………………

Mimi ndiyo nanyoosha mguu juu. yote utayasikia kwa jirani, kama hujui kujihudumia imekula kwako. la sivyo uendelee na huyo anayetoa huduma kuliko mm.
 
Wao wanasema wanaume hawaridhiki, but thats not true, sio wote wapo hivyo, wengine hujikuta circumstances zinawalazimisha kuwa hivyo. Just imagine mwanamke anataka eti mwanaume wake atoe masufuria kwenye nyumba ya kupanga pale uani akae kwenye kigoda achukue steel wire aanze kusugua ukoko wa ubwabwa! Kwani umefunzwa wapi we mwanamke? Huna baba? Huna makaka au wajomba ukaona mfano wa jinsi waafrika tunavyoishi katika mazingira yetu? Kwa nini wenzio wasikusaidie? Wanawake mtalalamika sana maana sio kuwa wanaume hawaoni mapungufu yenu sema sie ni watu wenye busara na maamuzi. Ndo maana unaweza kukuta mtu kaamua kuwa mlevi au anashinda ofisini mpaka wkend! Na wengine hujichukulia nyumba ndogo wanaojua mapenzi ni uwajibikaji japo hiyari ni wakati wa kuchagua nani wa kumpenda ila ukishampenda unakuwa duty bound na kuna sanctity to marriage. Sio rahisi kama wanawake wengi humu wanavyofantasize mapenzi. Kuna uwajibikaji pia, kwani mnaenda kitchen partie kwa fashion au kujifunza uwajibikaji kwenye ndoa? No wonder mie ni mmoja ya wanaopinga kitchen parties maana mtu anakuja kuingia kwenye ndoa bila kujua wajibu wake wakati alifanyiwa party ya kumfuna. Au huwa mnafuata zawadi ya vyombo? Kwani wadada wa siku hizi ukiingia nyumba yake hata kijiko hana eti anakula restaurant! Kupika zero, ukimpa unga apike ugali unakuja mbichi, ndo maana hata ukienda hoteli kubwa wanazokimbilia kula unakuta the chef ni mwanaume!


wewe unachuki binafsi na wanawake si bure, mapungufu wote tunayo ndugu yangu hata wewe unayo haijalishi unajielezea vipi hapa kwenye jukwaa..lol
 
Mtambuzi nilielewa swali uliloliuliza lakin pia sikutaka kwenda kwenye jibu direct manake ilitubidi tujue kwanza sababu zinazopelekea hayo kutokea. nasikitika kama nimekuwa mpotoshaji wa maana husika ila ukweli ni kwamba nilitaka kwamba nikupe sababu why so ndipo sasa tuanze kujua nini cha kufanya au tunataka nini.

back to the point, wanawake wote hawapendi maudhi hata kidogo, na kama walivyo ni watu ambao kwao kuwajibika ni kitu wanachokipenda sana. wanapenda basi kama mume ukikosea usijifanye mbabe na kuanza kugomba la omba msamaha yatatue yaishe muish kwa amani uone kama hata fanya wajibu wake.

unapokosea wewe kama baba na ukawajeuri hutak hata kuomba msamaha ni dhahiri unamkwaza huyu mama na utapelekea atafute mahali pa kupunguzia hasira zake na ndipo hapo anapogombana na kazi na hata watu wa nyumbani kwake. tunaamin katika maisha ya amani yasiyokuwa ya kibabe na jeuuri kama ambavyo wanaume wengi wanpenda kufanya.
gfsonwin sijui kama uliwahi kusoma uzi wangu huu hapa chini.........
kama ukiusoma kwa makini naamini hutakuwa na maswali zaidi

https://www.jamiiforums.com/mahusia...e-hawezi-kushindana-na-ubabe-wa-mwanaume.html
 
Last edited by a moderator:
hapa umefunga kazi dada gfsonwin .... huwa napenda sana michango yako coz huwa unaongea kama mama mwenye uzoefu na mwanamke anayejua what she is talking about... hivi mwanamke anaolewaje kama hata hajui kwamba anapaswa kutimiza wajibu fulani ndani ya nyumba in the first place? au 'wajibu' ni kwenda salon?

ahsante sana cartura binafsi napenda sana majukumu yangu ya umama. nad i live for it. to me my family is everything. Sipend sana kazi za kufanyiwa na mtu wa tatu napenda wale chakula nilicho andaa mimi, wavae nguo nilizo fua mimi na hata walalie matandiko niliyosafisha mimi.

kwangu kazi ya beki 3 ni kunisaidia pale ninapohitaji na pia kukaa na watoto mchana lakin kazi zangu za ndani sifanyiwi na nimeshazoea, hivyo na siwez badilika kwa hili. my maid is like ma daughter. mfanyaji wa kazi za ndani ni mimi mwenyewe ingaw zipo ninazo machinelize ili kunipunguzia kuchoka but cooking hii never kufanywa na mtu mwingine kama nipo.
 
Last edited by a moderator:
ahsante sana cartura binafsi napenda sana majukumu yangu ya umama. nad i live for it. to me my family is everything. Sipend sana kazi za kufanyiwa na mtu wa tatu napenda wale chakula nilicho andaa mimi, wavae nguo nilizo fua mimi na hata walalie matandiko niliyosafisha mimi.

kwangu kazi ya beki 3 ni kunisaidia pale ninapohitaji na pia kukaa na watoto mchana lakin kazi zangu za ndani sifanyiwi na nimeshazoea, hivyo na siwez badilika kwa hili. my maid is like ma daughter. mfanyaji wa kazi za ndani ni mimi mwenyewe ingaw zipo ninazo machinelize ili kunipunguzia kuchoka but cooking hii never kufanywa na mtu mwingine kama nipo.

that's great gfsonwin.... hapo lazima nitoe 'like' yangu ya 3 tu penda nisipende teh teh teh..
 
Last edited by a moderator:
Why Yummy?

Juzi nilikwua nasikiliza hizi redio Fanya Mizaha...kuna habari ilitoka gazeti nadhani Mwananchi,kwamba kuna kautafiti kanaonyesha 80% ya operations wakati wa kujifungua zinaombwa na wenye mimba, sababu mojawapo ikiwa ni kwamba 'hawataki kuharibu' maungo yao

Hata ukisoma mahojiano ya yule doctor wa mwanza sikumbuki ni lini kwenye mwananchi ametoa hiyo comment. Wanawake wanajua hilo wengi wanapenda kisu kwani inamhakikishia usalama wake na mtoto kuliko kawaida mtoto au mama anaweza kufa! Nadhani huyo mchangiaji anayesema sina mke wala mtoto siwezi kubishana nae kwanza anaonekana ni mtoto anadhani kila mtu humu anaongea kutaka umaarufu wa ID's! Tunapeana mawazo kama hujui au huamini ni bora uulize kuliko kujifanya unabisha jambo lisilopingika kwani utafiti ushafanyika ya kwa nini siku hizi wanawake wengi huzaa kwa kisu?
 
Last edited by a moderator:
Na mimi si ndo nimemshangaa. Wanadhani kujifungua LDCs ni mchezo, ni matter of life and death. Hivi kweli doctor anakwambia huwezi kujifungua kawaida nitakufanyia operation utasema sitaki. Thubutu. I wish na hawa wanaume wangebebaga mimba!

Hivi mnajua idadi ya vifo vya wajawazito huko vijijini ambao nyie mnasema ni hard working ladies. Temea mate chini; kwanza ana mtoto mmoja you never know uzao ujao utakuja vipi.

My first son nilizaa kawaida; wa pili nikapigwa kisu na si kwa option ila ni kwa kuwa mtoto angefia tumboni. Hence haya mambo ya uzazi mziyajadili kijuu juu tuachieni sie tunao experience the pain.



Yesu wanguuuuuuuuuu............you cannot be serious!!!!!!!!!!!!!! sidhani hata kama una mke wewe,sorry.
 
Sipend sana kazi za kufanyiwa na mtu wa tatu napenda wale chakula nilicho andaa mimi, wavae nguo nilizo fua mimi na hata walalie matandiko niliyosafisha mimi.

hebu nijuze gfsonwin (i know you are very frank), kwa mtazamo wako huu do you consider yourself as a traditional wife , mwanamke wa mwaka 47 au mwanamke aliyepitwa na wakati (as opposed to a modern, educated, professional, trendy, upwardly-mobile wife)? how do you balance muda wa kuweka ma-wig, kope, kucha n.k sambamba na ufanyaji wa majukumu yako kama ulivyoyaainisha pale juu?
 
Last edited by a moderator:
Amesahau na muda wa kumpet pet Mr. Au asije akawa analalia upande mmoja; kutwa jikoni. Lol.


hebu nijuze gfsonwin (i know you are very frank), kwa mtazamo wako huu do you consider yourself as a traditional wife , mwanamke wa mwaka 47 au mwanamke aliyepitwa na wakati (as opposed to a modern, educated, professional, trendy, upwardly-mobile wife)? how do you balance muda wa kuweka ma-wig, kope, kucha n.k sambamba na ufanyaji wa majukumu yako kama ulivyoyaainisha pale juu?
 
ahsante sana cartura binafsi napenda sana majukumu yangu ya umama. nad i live for it. to me my family is everything. Sipend sana kazi za kufanyiwa na mtu wa tatu napenda wale chakula nilicho andaa mimi, wavae nguo nilizo fua mimi na hata walalie matandiko niliyosafisha mimi.

kwangu kazi ya beki 3 ni kunisaidia pale ninapohitaji na pia kukaa na watoto mchana lakin kazi zangu za ndani sifanyiwi na nimeshazoea, hivyo na siwez badilika kwa hili. my maid is like ma daughter. mfanyaji wa kazi za ndani ni mimi mwenyewe ingaw zipo ninazo machinelize ili kunipunguzia kuchoka but cooking hii never kufanywa na mtu mwingine kama nipo.

Now this is a type of a woman i was referring to. Wengine sababu nimewagusa wamekuja na p.o.v.u kwa personal attacks! Hapa tuambiane ukweli wandugu na kama mtu anadhani nina chuki na mwanamke may be amenikosea. Kwenye ukweli tuambiane pia kama nina matatizo na mke wangu siwezi kuja kuyaongea huku zaidi nitaongea nae, sioni sababu ya kumuogopa kama amenuna! Otherwise mkimaliza kununa then pitieni uzi wote mjipatie kaufahamu kidogo kanaweza kusaidia mumeo aliye-busy na kazi au bia kuanza kuwa busy na wewe! Pia jitahidi jioni ukirudi upike chakula cha familia na kuogesha mwanao ili upate kumchunguza kama amefanyiwa kitu kibaya, sio unakuja mtoto kalala then baada ya wiki ndo unagundua mtoto amenajisiwa au anamatatizo fulani. Haya yanatokea kwenye jamii ndugu zangu sio lazima yatokee kwako ndio uje kutafuta ushauri.
 
Last edited by a moderator:
Now this is a type of a woman i was referring to. Wengine sababu nimewagusa wamekuja na p.o.v.u kwa personal attacks! Hapa tuambiane ukweli wandugu na kama mtu anadhani nina chuki na mwanamke may be amenikosea. Kwenye ukweli tuambiane pia kama nina matatizo na mke wangu siwezi kuja kuyaongea huku zaidi nitaongea nae, sioni sababu ya kumuogopa kama amenuna! Otherwise mkimaliza kununa then pitieni uzi wote mjipatie kaufahamu kidogo kanaweza kusaidia mumeo aliye-busy na kazi au bia kuanza kuwa busy na wewe! Pia jitahidi jioni ukirudi upike chakula cha familia na kuogesha mwanao ili upate kumchunguza kama amefanyiwa kitu kibaya, sio unakuja mtoto kalala then baada ya wiki ndo unagundua mtoto amenajisiwa au anamatatizo fulani. Haya yanatokea kwenye jamii ndugu zangu sio lazima yatokee kwako ndio uje kutafuta ushauri.

umeona eeh....! safi sana yaani, siyo mtu anashinda anasugua kucha za miguu tu, ukimuuliza eti hawajibiki kwa lolote (akipenda afanye, asipopenda to hell)...
 
Kwani wewe huwezi muogesha mwanao wa kiume mpaka house girl au mama yake? No wonder mnakesha vilabuni maana mna muda mwingi. Kumbuka mkeo si housewife, you can't eat your cake and have it. Mnarudi home saa mbili au saa moja; aanze kuingia jikoni kuoika watoto wale saa nne au wakiwahi saa tatu. Awaogeshe, asafishe nyumba; akiingia kitandani saa tano; bado unadai akufurahishe; maana hawezi furahi wakati yuko hoi.

Poleni wenye waume design hiyo. Wangu ndio kwanza ananuna nikitoka job na kuingia kwenye kazi za jikoni.



Now this is a type of a woman i was referring to. Wengine sababu nimewagusa wamekuja na p.o.v.u kwa personal attacks! Hapa tuambiane ukweli wandugu na kama mtu anadhani nina chuki na mwanamke may be amenikosea. Kwenye ukweli tuambiane pia kama nina matatizo na mke wangu siwezi kuja kuyaongea huku zaidi nitaongea nae, sioni sababu ya kumuogopa kama amenuna! Otherwise mkimaliza kununa then pitieni uzi wote mjipatie kaufahamu kidogo kanaweza kusaidia mumeo aliye-busy na kazi au bia kuanza kuwa busy na wewe! Pia jitahidi jioni ukirudi upike chakula cha familia na kuogesha mwanao ili upate kumchunguza kama amefanyiwa kitu kibaya, sio unakuja mtoto kalala then baada ya wiki ndo unagundua mtoto amenajisiwa au anamatatizo fulani. Haya yanatokea kwenye jamii ndugu zangu sio lazima yatokee kwako ndio uje kutafuta ushauri.
 
Now this is a type of a woman i was referring to. Wengine sababu nimewagusa wamekuja na p.o.v.u kwa personal attacks! Hapa tuambiane ukweli wandugu na kama mtu anadhani nina chuki na mwanamke may be amenikosea. Kwenye ukweli tuambiane pia kama nina matatizo na mke wangu siwezi kuja kuyaongea huku zaidi nitaongea nae, sioni sababu ya kumuogopa kama amenuna! Otherwise mkimaliza kununa then pitieni uzi wote mjipatie kaufahamu kidogo kanaweza kusaidia mumeo aliye-busy na kazi au bia kuanza kuwa busy na wewe! Pia jitahidi jioni ukirudi upike chakula cha familia na kuogesha mwanao ili upate kumchunguza kama amefanyiwa kitu kibaya, sio unakuja mtoto kalala then baada ya wiki ndo unagundua mtoto amenajisiwa au anamatatizo fulani. Haya yanatokea kwenye jamii ndugu zangu sio lazima yatokee kwako ndio uje kutafuta ushauri.
mkuu bondpost,nikuombe radhi kwa swali hili kama litakukwaza:
Tangia uoe ushawahi kum cheat mkeo?
...........just curious.
 
wanawake tunavyopenda kutumia vya wenzetu, sijui kama utapata majibu sahihi hapa,

kwa kifupi tu wanawake tupo wabinafsi saaaaaaan, changu changu, chako cha wote
 
itafikia mahali watu watakuwa wanatazamana tu usoni ndani ya nyumba - hakuna msosi, hakuna ada ya watoto, hakuna medical expenses, hakuna kupika, hakuna usafi, hakuna kuulizana kwa sababu kila kitu kinafanywa kwa hiari na hakuna anayewajibika ....

thubutu kufanya hayo, utabandikwa kila sehemu mwanaume suruali, hajui hata majukumu yake, yaani sisi tunajua sana majukumu ya wenzetu, ya kwetu hata sijui
 
Nakupinga kwa hilo. Ukiona mwanamke anakuwa baili jua kipato chake ni kidogo na mumewe anazo za kumwaga. Wengi tu tunachangia majukumu ya familia zetu.

Na hata wenye kipato kidogo ni wangapi tunawaona wanauza maandazi na vigenge watoto wao waende shule. Wajameni acheni adithi za mapokeo.


Ni wanaume wangapi walokuwa na mapesa na kufulia; kwa aibu wanajifungia ndani wakati wake zao ambao walikuwa watu wa matanuzi wanaingia kwenye biashara ambazo hamna ambaye angefikiria wanaweza kufanya. Sisi ni shock absorber bana! Afi mtu na njaa hata kama mme katimuliwa kazi.

wanawake tunavyopenda kutumia vya wenzetu, sijui kama utapata majibu sahihi hapa,

kwa kifupi tu wanawake tupo wabinafsi saaaaaaan, changu changu, chako cha wote
 
Back
Top Bottom