Wanawake mtaacha lini ukatili huu mbona umezidi?

nitonye

JF-Expert Member
Dec 18, 2011
7,273
3,750
Hii tabia sijui itaachwa lini maana ni ukatili wa hali ya juu. Leo niko zangu ndani ya daladala mara akapanda mwanamke mwenye mtoto mdogo kwa sababu seat zilikuwa zimejaa akamwomba mwanamke mwenzake ampakatie mtoto. Maskini mama wa watu alikubali ghafla yule mama mwenye mtoto akapotea katika mazingira ya ajabu hatukujua ameshukaje kamuacha mtoto mikononi mwa mtu mwingine. Na hii tabia imekuwa ikiendelea siku hadi siku.
 
Bora huyo kuliko wale wanaowaweka kwenye malboro kisha wanawatupa mitaroni..
 
Ah wanawake wengine sijui wana roho katili kiasi gani, unamuacheje mwanao ulombeba tumboni miezi 9 kwa mtu kisa ugumu wa maisha,mungu asinijaalie fikra mbaya Kama hizo,mie mwanangu ntakufaanae shida raha ntakuanae.
 
wanaume tuache kuwapa mimba na kuwakimbia

Mwenye maamuzi ya kupata au kutopata mimba ni mwanamke kwani yeye ndiye mwenye kujua siku zake za mimba. Kwanini mnaipeleka wakati mnajua mpo kwenye siku za uchavushaji!!!
 
Back
Top Bottom