nitonye
JF-Expert Member
- Dec 18, 2011
- 7,273
- 3,750
Hii tabia sijui itaachwa lini maana ni ukatili wa hali ya juu. Leo niko zangu ndani ya daladala mara akapanda mwanamke mwenye mtoto mdogo kwa sababu seat zilikuwa zimejaa akamwomba mwanamke mwenzake ampakatie mtoto. Maskini mama wa watu alikubali ghafla yule mama mwenye mtoto akapotea katika mazingira ya ajabu hatukujua ameshukaje kamuacha mtoto mikononi mwa mtu mwingine. Na hii tabia imekuwa ikiendelea siku hadi siku.