Mvumilivu2
Senior Member
- Jul 31, 2014
- 107
- 47
Heshima mwenu wakuu,
Story ipo hivi kuna dada mmoja tunaishi nae nyumba mmoja kaolewa kwa ndoa kabisa na wana mtoto wa kike wa miaka miwili.
Huyu dada alichokifanya alienda kwao akaja na mdogo wake wa kike umri miaka 15 anaishi nae chumba chenyewe kimoja.
Juzi kati kaenda tena kakuta mdogo wake mwingine kafunga shule nae kamleta ana miaka 10 wa kike wanalala humo humo ndani sasa kabla ya huyo dogo mwingine kuja huyu dada huwa anatoka saa kumi alfajiri kwenda kuchukua mzigo anamuacha mdogo wake ndani na mumewe wanalala wee hadi saa mbili.
Sasa hivi huyu mume akienda kuoga anavalia huko huko kama yupo kambini vile. Wadada mlio ndani ya ndoa msijisahau ndoa ngumu sana kuipata hata kama tunatokea familia ya chini lakini tufikirie tunapoleta ndugu zetu kukaa nao ili hali hakuna pa kulala madhara ni mengi.
Natamani hata nimshauri ila nahisi ataona kama namuingilia uhuru wake.
Hivi hili limekaaje wadau ni uungwana mtu akiolewa akalete na ndugu wakati hakuna hata pa kulala? Yani nashindwa hata kuishangaa hii familia yani watu watano chumba kimoja mh hapana.
Karibu tulijadili wengine wapate funzo.
Story ipo hivi kuna dada mmoja tunaishi nae nyumba mmoja kaolewa kwa ndoa kabisa na wana mtoto wa kike wa miaka miwili.
Huyu dada alichokifanya alienda kwao akaja na mdogo wake wa kike umri miaka 15 anaishi nae chumba chenyewe kimoja.
Juzi kati kaenda tena kakuta mdogo wake mwingine kafunga shule nae kamleta ana miaka 10 wa kike wanalala humo humo ndani sasa kabla ya huyo dogo mwingine kuja huyu dada huwa anatoka saa kumi alfajiri kwenda kuchukua mzigo anamuacha mdogo wake ndani na mumewe wanalala wee hadi saa mbili.
Sasa hivi huyu mume akienda kuoga anavalia huko huko kama yupo kambini vile. Wadada mlio ndani ya ndoa msijisahau ndoa ngumu sana kuipata hata kama tunatokea familia ya chini lakini tufikirie tunapoleta ndugu zetu kukaa nao ili hali hakuna pa kulala madhara ni mengi.
Natamani hata nimshauri ila nahisi ataona kama namuingilia uhuru wake.
Hivi hili limekaaje wadau ni uungwana mtu akiolewa akalete na ndugu wakati hakuna hata pa kulala? Yani nashindwa hata kuishangaa hii familia yani watu watano chumba kimoja mh hapana.
Karibu tulijadili wengine wapate funzo.