Salamu za weekend wakuu,
Iko hivi, Jana nilipokuwa narudi kutoka kwenye mihangaiko nilikutana na Brother yangu mmoja hivi ambaye kitambo sana tulikuwa tunaishi kama majirani kwa wazazi ambapo tulikuwa tukifahamiana sana.
Sasa jamaa nilimkuta yuko katika hali ya kama kuchanganyikiwa. Ilibidi nisimamishe gari nimfate tukasalimiana then nikamuuliza kulikoni?, anaelekea wapi? Ili ikibidi nimsogeze kwasababu hakuwa na usafiri. Jamaa akaanza kufunguka kwamba alikuwa amesafiri kidogo kikazi sasa aliporudi akawa anaangalia baadhi ya documents zake za Kiwanja ambacho amenunua, Kadi za pikipiki mbili pamoja na kadi ya gari, akadai havioni.
Nikamwuliza kwani kwenu mnaishi wangapi si mko wawili tu yaani wewe na mkeo? akajibu ndio nikamwuliza vp mkeo anasemaje akanijibu amemwuliza nae anadai hajui zilipo ila akanambia kwamba siku chache kabla ya yeye kusafiri walikorofishana kidogo na mkewe akawa amesafiri kwenda kwao na aliporudi tripu hii akawa anadai waachane ndipo yeye akapata safari kazini.
Nilichomshauri mimi ni kwamba awaite wazee 2 au 3 pamoja na huyo mke wake then walizungumzie hili swala amwulize kwamba hizi documents ziko wapi kama anazo azitoe na kama hana washirikiane ili kupata nyingine. Brother alikubali.
Ila kuna mzee flani ambaye ni kaka wa dada yake nilipomtaja tu kwamba na yule asimsahau kwenye moja ya watu atakao waita akadai hawezi kumshirikisha kwasababu kipindi anataka kumwoa huyu msichana dada zake na mke wa dada yake mkubwa walimkataza asioe huyu mwanamke ila yeye alikaidi.
Wakuu mi nimebaki najiuliza inakuwaje mwanamke anachukua documents za muhimu then unazificha.? japokuwa sina uhakika wa moja kwa moja ila picha linaonyesha mke anahusika.
Mwenye ushauri zaidi anaweza kunipatia nimfikishie mhusika ili kuweza kuvipata vitu vyake.
Thanks.