Wanawake jifunzeni kutoka kwa mama huyu

Mkulima na Mfugaji

JF-Expert Member
Jul 26, 2013
1,013
1,634
BINTI NA MAMA YAKE

Binti : Hivi mama, kwanini uliamua kuolewa na baba?

Mama : Upendo wake ulinivutia sana.

Binti : Upendo tu, hamna kingine kilichokuvutia?

Mama : Hahaha mwanangu, unajua Upendo hufanya uone kila kitu tofauti na wengine waonavyo.

Binti : Kwani wanaume wengine hawakuwahi kukupenda?

Mama : mmmh walikuwepo na walinipenda tena inawezekana walinipenda kuliko hata alivyonipenda baba yako. Ila Upendo wao haukuongea lugha ninayoielewa.

Binti : Upendo na lugha tena Mbona unanichanganya.

Mama: Kuwa na uwezo wa kuongea hakumaanishi ndio Kuwa na uwezo wa kueleweka. Hivyo kujua kupenda haimaanishi ndio kujua kuonesha huo Upendo kwa unayempenda.

Binti : Kwa hiyo hamjawahi kugombana au kutofautiana hadi ukatamani usingeolewa naye?

Mama : Kwa kweli imeshatokea. Lakini mimi na baba yako ni marafiki na si unajua marafiki kama hamjawahi tofautiana ujue mmoja wenu au wote ni wanafiki.

Binti : Kwani na ninyi mlikuwa mnakula bata enzi zenu.

Mama : hahahaha kila enzi ina enzi. Kila mziki una aina yake ya kucheza. Tofauti yetu na ninyi ni kwamba bata mnaweka mbele kabla ya kutengeneza banda. Yaani namaanisha starehe ni baada ya kazi. Hata Mungu alistarehe baada ya kazi ila ninyi kazi hamtaki mnataka starehe ndio maana hata wanaume mnataka waliokwisha fanikiwa Kuwa na mali na sio wanaowapenda hata kama wanavitu kidogo.

Binti : Mmh mama ndio unatunanga

Mama : Kwani uongo si ulilalamika wewe wakati nimemwachisha dada wa kazi. Unadhani ungekuwa unajua kupika kama sio kukusimamia kidete. Kupika kufua kuosha vyombo hamjui ila kila kumbi za starehe mnazijua. Halafu mnataka muwe na ndoa nzuri.

Binti : Eeh mama basi, Kwani mi nilikuuliza hayo.

Mama : Umenianza mwenyewe sasa tulia hivyo hivyo unisikilize. Kipindi chetu sio kwamba tulikuwa hatutongozwi ila kujiheshimu na kujitunza kulitusaidia sana. Sasa nyie leo ukifuatwa na mkaka yaani kila msichana atajua umefuatwa, unadhani kwa kijana anayejiheshimu akisikia hiyo tabia yako hata kama anakupenda hakufuati ng'oo. Mtaendelea kufuatwa na wanaotaka kuwachezea maana hao hata wakisikia umewasema vibaya wala haiwasumbui watakung'ang'ania mpaka unadhani anakupenda unamkubalia. Kwa Kuwa amekufuatilia muda mrefu unajua anakupenda kweli. Unampa mwili wako anakuchezea na anakuacha. Halafu ooh wanaume wahuni Kumbe vidomodomo vyenu vimewaponza hadi wanaume wa kweli hawaji.

Binti : Eeh mama ndio unanipa risala khoooh

Mama: Ndio si hukuuliza haya ya awali ukakimbilia kwamba kweli nampenda mume wangu. Nampenda na nampenda haswa na tunavyoelewana tangu tunachumba kimoja na kitanda cha kamba na godoro la sufi hadi leo tuna nyumba kadhaa na ninyi mnasoma.

Binti : Mama nakuja naenda kununua vocha.

*Fikicha Akili*

JIFUNZE KUJIFUNZA
 
Back
Top Bottom