Wanawake Arumeru mashariki wampa onyo kali NAssari.

Wanawake Arumeru mashariki wampa onyo kali NAssari.

Hao kina mama ni wa chama gani?Mbona mm nakaa usa River sijasikia
hilo?Hatudanganyiki.

yeye ni mbunge wa baadhi ya watu???kumbuka ukishakuwa kiongozi wa serikali unaongoza watu wote hata wale wanaokupinga.wewe kujenga hoja kuwa ni watu wa chama gani wanaotoa maoni haya ni ulimbukeni tu.Mwalim Nyerere anaita uzuzu
 
Mwanzoni tuliambiwa WAZEE wa kimila (WASHIRI) leo wanawake yani CCM bila kujaribu kugawa watu kijinsia,kikabila,kidini,kivyeo hawawezi kuungwa mkono au ni nini...hao wanawake kama wapo ni SHANGAZI zake SIOI SUMARI bado wana machungu.
 
Walisema "kauli za Mbunge wao siyo za kujenga bali ni kubomoa na kuchochea malumbano makubwa ambapo kwa sasa alipaswa kuwa anaongelea jinsi ya kutatua changamoto mbalimbali zilizomo kwenye jamii".
Source: wavuti - wavuti
 
Hawa wanawake wa "Arumeru" watueleze haya;

1. Kauli na majibu gani hayo wanayo yasema?

2. Walishindwaje kumwambia Mh. Nassari hayo huku
wako naye hao Arusha hadi wakayaseme kwa
"VIONGOZI waliowatembelea"? tena ana kesi hapo hapo
Arusha?

3. Halafu kwanini waongee na wanachama wa CCM
pekee??!



Ushauri: Enyi wanawake wa "ARUMERU" dont make threats that you cant deliver..kama kuingia mitaani ndiyo suluhisho la hayo matatizo yenu ya "kauli" ambazo hata mnashondwa kuzitaja...ingieni tu, hamna hata haja ya kutoa vitisho.!! mambo ya "mipasho" yaacheni huko huko "mnakopashana" mkiwatembelea hao "viongozi sanjari na kuongea na wanachama wa CCM"

hawakuwekewa mipaka ya kutolea maoni ya kero zinazowakabili.


Kaskazini ijitenge - Nassari
 
kaskazini ijitenge - Nassari akiwa arumeru jimboni

Hii kauli ilishatolewa maelezo. Ifike mahali watanzania tukue na kuongea mambo ya msingi. Kama ni kosa lirekebishwe kwa wakati, lakini hatuwezi kupiga hatua kwa kurudia rudia mambo ambayo yameshatolewa ufafanuzi. Ni mufilisi wa hoja ndio anawekeza kwenye mambo yale yale muda wote.
 
Hawa ndio waandishi makanjanja wa vibahasha,sioni habari hapa halafu anasema wanawake wa arumeru wakati ni magamba ya kike ambayo yalimpa kura yule mtoga masikio wao asiyejua hata meru ikoje.....
 
Wavuti nina uhakika hii habari wame copy na ku paste kutoka gazeti la Uhuru, maana hizi propaganda za CCM hazina mashiko wakati wa kampeni ilikuwa Arumeru Mashariki kuna Wazee wa Kishiri sasa hivi wakina Mama wanatoa maoni yao na kulia na wanataka kuandamana... nimesha toast kwenye trash hii news
 
Nimekaa nasoma siona hata hiyo kauli ya Nassary wanaoipinga, waandishi wa habari bana!

Ushabiki wa magazeti,ukiangalia walioongea ni wanawake wa CCM Arumeru ambao hata hivyo hawakumchagua wala kuchangia ushindi wake na wako kwenye kikao cha CCM,sasa ulitegemea waseme nini tofauti na walichosema?
 
Nimekaa nasoma siona hata hiyo kauli ya Nassary wanaoipinga, waandishi wa habari bana!

True. Hii sio habari. Ni umbea tu na sisa za majitaka. Habari haisemi ni kauli gani hizo za Nassari zinazolalamikiwa, wanawake hao ni akina nani, walitoa tamko lini, wapi, na haijaonyesha kama walimuhoji Nassari ku-balance story yao. This is rubbish.
 
Wanawake Arumeru Mashariki wampa onyo Mbunge wao, Nassari la sivyo atajajuta

20/09/2012



Na Queen Lema, ARUSHA -- Wanawake wa eneo la Kisambare, Usariver, wilyani Meru mkoani Arusha wamesema kuwa kamwe hawatavumilia kauli za mbunge wa jimbo hilo, Joshua Nasari badala yake watalazimika kuingia barabarani kumpinga hadharani Mbunge huyo kwani kauli zake hazijengi hoja za kutetea shida za wananchi na badala yake zinachochea malumbano pamoja na migogoro huku wanawake wa Vijijini wakiwa wanakabiliwa na shida mbalimbali

Wanawake hao waliyasema hayo jana Wilyani humo wakati wakizungumza na Viongozi mbalimbali ambao waliwatembelea Kijijini humo sanjari na kuongea na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi.

Walisema kauli za Mbunge wao siyo za kujenga bali ni kubomoa na kuchochea malumbano makubwa ambapo kwa sasa alipaswa kuwa anaongelea jinsi ya kutatua changamoto mbalimbali zilizomo kwenye jamii.

Wakasema Mbunge huyo anapaswa kujua na kutambua kuwa alipewa jimbo hilo kwa hasira kutokana na kukithiri kwa changamoto lukuki ambazo zimo kwenye jamii hasa za Wameru na kwa hali hiyo huu ndio muda muafaka wa Mbunge huyo kuhakikisha kuwa anatatua kero na wala sio kutoa matammko ambayo hayana tija na jamii.

Waliongeza kuwa kauli hizo zimekuwa na madhara makubwa sana hasa kwa vijana kwa kuwa mpaka sasa wapo baadhi yao wanaofanya makosa na kuvuruga amani, kwa visingizo vya Mbunge huyo, “tunachotaka kujua ni kuwa tunatatuliwa kero zetu lakini badala mbunge afikirie suala zima la maendeleo yeye anafikiria kuzima mwenge wakati sisi hatuna shida na mwenge na mwenge unapita lakini shida zetu hasa sisi wakina mama wa Nkoakirika hatujui hata majira ya saa sasa tueleweje kwani tukimbia CCM kutokan a na changamoto lakini hii ya sasa ni kali na kama huyu mbunge ataendelea hivi basi ipo siku matatizo makubwa sana yatatokea” waliongea akina mama hao huku wakilia.

Mbali na hayo, waliongeza kuwa nao viongozi wa siasa watakiwa kukumbuka ahadi mbalimbali ambazo wamezitoa kwa jamii hasa nyakati za kampeni kwani baadhi ya viongozi, hasa wa Mkoa wa Arusha wakishapata nafasi ya kuongoza basi wanakuwa na matamko ambayo hayana tija na badala yake yanasabahbisha baadhi ya vijana kukamatwa ovyo na Polisi.

Awali Katibu wa CCM Wilaya ya Meru, Langaeli Akyoo alikiri kuwa CCM ilikuwa na kasoro hali ambayo iliwafanya wananchama wake kukopesha jimbo la Arumeru Mashariki lakini kwa sasa chama hicho kimejipanga hata kwa Watendaji wa huduma zote za kijamii kuhakikisha kuwa wanatekeleza sera za wananchi.

Bw. Akyoo alisema, hasira ambazo ndio chanzo pekee cha wananchi kutoa kura kwa upinzani kwa sasa zitapunguzwa kwa kiwango cha juu huku jamii hasa za vijijini zenye mahitaji maalumu nazo zikiweza kupatiwa ufumbuzi wa matatizo yao kwani uwezekano wa kuwasaidia bado ni mkubwa sana.



Source:
wavuti - wavuti
Matamko yapi hayo?
 
Haha,haha,hao ni wanawake wa CCM ambao hawataki kubadilika hata siku moja,wamezoea kuhongwa kanga za CCM na vilemba
 
Back
Top Bottom