Mgirik
JF-Expert Member
- Apr 27, 2013
- 13,258
- 13,368
Ilikuwa mwaka 2004 nilipokuwa kidato cha kwanza katika shule ya sekondary Matema beach iliyopo wilayani Kyela. Katika shule hiyo nilipokuwa nasoma nilibahatika kufahamiana na dada mmoja alikuwa anafanya biashara ya kuuza chai na maandazi mbali kidogo na eneo la shule.
Alikuwa ni dada mwenye heshma na nidhamu ya hali ya juu sana na alikuwa mpole sana. Kama ilivyo kwa vijana wengi tunapokuwa kwenye umri huo nilitokea kumpenda na ikabidi nimtongoze. Lakini yule dada alikuwa anasita sana kunikubalia, mimi nikazidi kumganda na baadaye akakubali kuwa wapenzi.
Ikaanza shughuri ya kutaka kufunua utupu, huyu dada alikuwa mbishi sana kuniachia utupu, sikukata tamaa nikazidi kumganda ili anifunulie utupu lakini dada alikuwa mbishi sana.
Sababu yake kuu ilikuwa ni" mdogo wangu ipo siku nitakupa penzi ila nakuomba soma kwanza sitaki nikuchanganye wewe bado mdogo sana mama yako atanilaumu sana siku nikikupa. Mimi nipo kwaajili yako hiyo ndio ilikuwa sababu yake kuu ya kunakatalia utupu.
Alizidi kuwa karibu yangu zaidi na alikuwa ananipa kila ninachokitaka isipo kuwa kunivulia nguo tu. Siku zikaenda na miaka ikapita hatimaye nikamaliza masomo yangu huku dada Sophie akiendelea na biashara yake. Hatimaye nikaondoka na kuja kanda ya mashariki kimasomo.
Kule Mbeya yule dada akaanza kuugua wakazunguka naye katika hospitali mbambali lakini hakupata nafuu. Siku moja nikaenda likizo nikaenda moja kwa moja kwa yule dada kwenda kumpa salam nikamkuta anaumwa lakini alikuwa katiak hali ya kawaida.
Baadaye nikarudi masomon toka kipindi hicho cha mwaka 2008 sikurudi tena mpaka nilivyorudi mwaka huu wiki iliyopita. Ndipo ilipopatwa na mshangao nilipoenda kumsalimia dada Sophie ambapo nimeoneshwa kaburi lake na kuambiwa kuwa amefariki kwa UKIMWI.
Sijaamini kwa kweli. Kumbe yule dada alikuwa na siri nzito sana moyoni mwake, Alinipenda zaidi mpaka aliweza kuniepusha na kiama cha ugonjwa huu.
Nmeoneshwa picha zake ni alikuwa anatisha. Jamani wanaume sio kila mwanamke anayekukataa hakupendi, mwingine anakuokoa na hatari.
Alikuwa ni dada mwenye heshma na nidhamu ya hali ya juu sana na alikuwa mpole sana. Kama ilivyo kwa vijana wengi tunapokuwa kwenye umri huo nilitokea kumpenda na ikabidi nimtongoze. Lakini yule dada alikuwa anasita sana kunikubalia, mimi nikazidi kumganda na baadaye akakubali kuwa wapenzi.
Ikaanza shughuri ya kutaka kufunua utupu, huyu dada alikuwa mbishi sana kuniachia utupu, sikukata tamaa nikazidi kumganda ili anifunulie utupu lakini dada alikuwa mbishi sana.
Sababu yake kuu ilikuwa ni" mdogo wangu ipo siku nitakupa penzi ila nakuomba soma kwanza sitaki nikuchanganye wewe bado mdogo sana mama yako atanilaumu sana siku nikikupa. Mimi nipo kwaajili yako hiyo ndio ilikuwa sababu yake kuu ya kunakatalia utupu.
Alizidi kuwa karibu yangu zaidi na alikuwa ananipa kila ninachokitaka isipo kuwa kunivulia nguo tu. Siku zikaenda na miaka ikapita hatimaye nikamaliza masomo yangu huku dada Sophie akiendelea na biashara yake. Hatimaye nikaondoka na kuja kanda ya mashariki kimasomo.
Kule Mbeya yule dada akaanza kuugua wakazunguka naye katika hospitali mbambali lakini hakupata nafuu. Siku moja nikaenda likizo nikaenda moja kwa moja kwa yule dada kwenda kumpa salam nikamkuta anaumwa lakini alikuwa katiak hali ya kawaida.
Baadaye nikarudi masomon toka kipindi hicho cha mwaka 2008 sikurudi tena mpaka nilivyorudi mwaka huu wiki iliyopita. Ndipo ilipopatwa na mshangao nilipoenda kumsalimia dada Sophie ambapo nimeoneshwa kaburi lake na kuambiwa kuwa amefariki kwa UKIMWI.
Sijaamini kwa kweli. Kumbe yule dada alikuwa na siri nzito sana moyoni mwake, Alinipenda zaidi mpaka aliweza kuniepusha na kiama cha ugonjwa huu.
Nmeoneshwa picha zake ni alikuwa anatisha. Jamani wanaume sio kila mwanamke anayekukataa hakupendi, mwingine anakuokoa na hatari.