Wanaume wenzangu tusiwe hivi....

Wanaume wenzangu tusiwe hivi....

SI unit

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
1,953
Reaction score
767
HABARI ZA USIKU HUU WAUNGWANA..
Nimetoka kwenye mihangaiko yangu muda si mwingi, nasikia timbwili kwa jirani huku mtoto mdogo wa miaka
miwili analia mama, mama.. Mimi ni mwoga sana wa kingilia majambo ya watu hasa wapendanao manake
kibao kinaweza kukugeukia then ukapata aibu na fedheha.. Aaah! Nikasema ngoja niingie kwenye kiota changu
ya ngoswe nimwachie ngoswe.. Ugomvi ukaendelea mpaka njeeeee mambo hadharani, matusi ya nguoni, kila
mmoja anamtuhumu mwenzie m.a.l.a.y.a.... E'bwana eeh!!! Kumbe ugomvi umesababishwa na mwanaume..
Bibie alienda kwa bafu kukoga akawa amesahau soap.....akaacha ndoo ya maji kwa bafu kafata sabuni.. Hapo
ndipo aliposikia sauti ya mahaba ya sweetie wake ikiongea na kajumba kadogo akimlaki kwa maneno 'i miss u since
easter'...lol. Bibie uzalendo ukamshinda, safari ya kuoga ikaishia pale likaanzishwa tifu.. Kumbe yasemekana huyu
bwana mkubwa alikua na ka-small haus pasaka huku akiwa amedanganya kwa bi mkubwa wake kuwa atalala kazini..

MY TAKE
  • Kama tuna vijumba vyetu vidogo wajameni tuviache hukohuko tusivikaribishe vivuruge familia zetu
  • Tuwaonee huruma hawa malaika [watoto] ambao wanapata maumivu kwa mahomvi yetu, tena tunawalisha dozi ya matusi isiyostahili.
  • TUEPUKE KABISA NYUMBA NDOGO otherwise HALALISHA KAMA MFALME MSWATI ILI WAJUANE NA WASIONEANE WIVU
  • etc
.............
ALAMSIKI
 
mi sijaelewa, ni kwamba hiyo small house ilikuja nyumbani kwao au wanaishi nyumba moja?
maana kama wife alikuwa anaenda kuchukua sabuni ndani hiyo waooooo kaisikiaje huko kwa nyumba ndogo?
 
good waongezee dozi nyingine kina baba huruma(hawafungi zipu zao)
 
mi sijaelewa, ni kwamba hiyo small house ilikuja nyumbani kwao au wanaishi nyumba moja?
maana kama wife alikuwa anaenda kuchukua sabuni ndani hiyo waooooo kaisikiaje huko kwa nyumba ndogo?

hahahaha shost amesikia maongezi ya husband wake anamuwaoooo small house,hiyo small house alilala nayo kipindi cha pasaka kwa kisingizio cha kulala kazini hapo upooooo
 
hahahaha shost amesikia maongezi ya husband wake anamuwaoooo small house,hiyo small house alilala nayo kipindi cha pasaka kwa kisingizio cha kulala kazini hapo upooooo
shosti, ilikuwa inamuwao kwenye simu?
 
shosti, ilikuwa inamuwao kwenye simu?

Hehehe mtani unataka hadi tuchore mchoro jamani...
Ukiwa na smolo hauzi lazima uwe na maneno ya mikogo na mbwembwe nyingi yote kujikosha tu...
Hiyo waoooo kama ilikuwepo basi ni kuchagiza maongezi ili kumtia kimuhemuhe tu huyo bi mdogo ajione yeye ndio Kwini Elizabeti wa II.
 
Tanzania bila nyumba ndogo haiwezekani kama ilivyo UKIMWI. Hivi kwanini watu hawaridhiki na wake/wapenzi wao????Hadi ucheat ndio uone sawa??mhh hayeni ila mjaribu kuwaonea huruma angalau watoto wenu mliowazaa
 
inavyoonyesha huyo husband ndo alikuwa anamwambia maneno laini small house,kama ujuavyo ukute huyo big house hajasikia maneno adimu kama hayo miaka kadhaa,loh direction ya kuchukua sabuni ikahamia kwenye timbwili.
ha haaa, kama namuona bidada na lubega lake, lol!
sabuuni sabuuniii.
baba usikute alijiachiaaaaaa maana anajua mpaka mamsap amalize kuoga......si unajua tena unapoongea na mupenzi.....
 
ha haaa, kama namuona bidada na lubega lake, lol!
sabuuni sabuuniii.
baba usikute alijiachiaaaaaa maana anajua mpaka mamsap amalize kuoga......si unajua tena unapoongea na mupenzi.....

My dia kuna baadhi ya wanaume ni manyang'au aiseeh ukirudi toka bafuni unapokelewa na tabasamu fake dah
 
Huo ndiyo unaitwa wizi wa kutoshirikisha akili kubwa na ndogo...

Basically, akili ndogo ndiyo ilikuwa kazini...


Babu DC!!
 
Sio kila wakati mbwa akibweka kuna hatari ya kuonekana kwa macho!
 
hilo tabasamu usifikiri lako......
anamalizia kutabasamu aliyokuwa anaambiwa na mupenzi..... mbona kazi tunayo binadamu!

hahahaha umenichekesha sana,anakumbukia alivyofia kiunoni siku ya pasaka we unajua anakufurahia ama kweli Mungu alituweza kutuficha mioyo ya wengine inafikiria nini
 
Back
Top Bottom