Jadda
JF-Expert Member
- May 20, 2019
- 31,547
- 88,538
Hahahaha na hii ndiyo sababu kwanini nilibadili id yangu ya JF labda nikupe hint kidogo ya personality yangu sikia iko hivi ile id niliyokuwa natumia mwanzo ya Edelyn ndo official nick name yangu ambayo karibu watu wote wanaonijua wanaijua ila nakumbuka nilishawahi kusema humu kuwa hakuna mtu wangu yeyote wa karibu ambaye ni member wa JF isipokuwa mmoja tu ambaye ni rafiki yangu tena naye mimi ndo nilimsaidia kujiunga na hata hayuko active sana as in huwa hachangii mada sana humu ila wengine labda kama wapo bila mimi kujuamy previous comment was intentionally made to persuade you to give your view in subtle way about that. Yeah!! of course how we present ourselves in this forum can be a reflection of our manners at least in social sense. I am used to you as argumentative fellow i’d never thought you are even good in vulgar language, that queer side was yet to be seen by me. However i salute your tenacity girl.
Sasa juzi kati hapa kuna ndugu zangu wanaonijua vizuri ndani nje nje ndani kitabia waliojiunga JF hivi karibuni na kukutana na baadhi ya comments zangu humu walinifuata wakaniuliza yule Edelyn wa JF ni wewe nikawaambia ni mimi aise walinishangaa wakaniambia wewe Edelyn huyu huyu tunayekujua sisi au mwingine wewe ulivyo mpole hivyo tangu lini ukajibishana na watu tena kwa majibu ya hovyo kama yale na comments ndefu kama zile nikawaambia ile ni confidence tu ya nyuma ya keyboard wakasema haiwezekani hiyo confidence umeipatia wapi wakati sisi tunakujua hata mtu akikukosea vipi hauwezagi kumjibu vibaya siyo kwa matamshi wala maandishi wakaniuliza na shemeji yetu anajua nikawaambia hajui hayupo JF wakasema tena yule akijua ndo atakataa kata kata kwamba siyo wewe mwenye majibu yale
Yaani hawakuamini na walinishangaa hadi nikaona aibu nikawaza ningejua ningewadanganya tu kwamba siyo mimi ni mtu tu mwingine anatumia id inayofanana na nick name yangu ila ndo hivyo nilishalikoroga tena nahisi walizifuma zile comments nilizokuwa nabishana na wewe na Extrovert sasa nikaona isiwe taabu ngoja nitafute jina ambalo sijawahi kulitumia popote na wala hamna kati yao anayelijua ndo nikapata hili nikawatafuta mods wanibadilishie id wakanibadilishia na najua wale hawawezi kugundua kama ni mimi ndo nimebadili id maana hawako active sana JF
Mimi ndo maana huwa nawashangaa watu humu wanaosemaga eti haya tunayoyaandika humu ndo yanatambulisha uhalisia wetu sijui labda kama wengine huwa wanaandika mawazo yao halisi ila mimi siwezi kufanya hivyo na wala siwezi kusema namjua mtu kutokana tu na anayoyaandika mitandaoni hasa JF tena mengi ninayoyaandika humu huwa sitoi kichwani kwangu bali huwa nayasikia tu kutoka kwa baadhi ya marafiki zangu maana na mimi nina marafiki pasua vichwa wana midomo hao yaani haya ninayoyaandika humu wao huwa wanakuwaga na ujasiri wa kuyatamka kabisa kwa kifupi tu ni kwamba Edelyn wa JF na Edelyn wa real life ni watu wawili tofauti japo ni mtu mmoja you may take it or leave it but that is the truth