Wanaume wengi hupenda baadae

Wanaume wengi hupenda baadae

Alola

JF-Expert Member
Joined
Nov 14, 2013
Posts
476
Reaction score
300
Salaam wanabodi,

Nimeona nitumie fursa hii kuwafunulia dada na mama zetu jambo moja ambalo wengi wao hawalielewi au hawataki kulielewa.

Kwa kawaida wanaume wengi huwa hawaingii mazima (committed) miezi ya kwanza ya mapenzi. Jambo ambalo
hutafsiriwa vibaya na wanawake wengi. Ukweli ni kwamba wanaume wengi huwa wanapenda baadae sana. Kwa mfano unaweza kuona mtoto wa kiume anavyo kua, kuanza kujitegemea, n.k anaanza kukuza sana mapenzi yake na mama kwasababu akianza kufikiria yale malezi yote aliyotendewa anasema 'loh nakupenda sana mama'.

Hii haimaanishi watoto wa kike hawawapendi mama zao lakini ukweli ni kwamba watoto wa kiume wengi huwapenda sana mama zao na watoto wa kike wengi huwapenda sana baba zao. Nadhani ni suala la uwiano wa hasi na chanya. Na mama anawakilisha mwanamke, kwahiyo kuna baadhi ya malezi ambayo mwanaume aliyapata kwa mama yake angependa pia kupewa na mwanamke wake.

Kwenye mapenzi ya mtu na mwenza wake ni kawaida kwa wanawake 'kuzimika haraka kimapenzi' kwa mwanaume lakini huchukua muda sana kwa wanaume wengi kuthamini na kuanza kumpenda mpenzi wake wa kike kwa moyo wote.

Hivyo basi mwanamke usiwe mwenye papara ya kutaka 50/50 mara unapoanza mahusiano na mwanaume. Usimpe vikwazo vya kutaka abadilike kwanza ili muwe wapenzi. Unapaswa kumkubali kama alivyo halafu baadae waweza kumshauri abadilike vile wewe unavyotaka, lakini pia kumbuka katika mapenzi ni lazima kukubali kuishi na baadhi ya tabia za mwenza.

Haitowezekana aishi utakavyo wewe kwa 100%. Na yeye hatakiwi kukushurutisha wewe uishi atakavyo yeye. Ni suala la kukubaliana na kuamua kuishi na tofauti zenu. Kwa hiyo usiseme "ah mtu mwenyewe hajui kuvaa" au "jamaa halipigi simu kutwa nzima..siwezi date na mtu wa hivyo mimi":smile-big:. Mkubali kwanza kama alivyo na hayo mengine yatafuata taratibu.

Tumia jinsia yako uliyopewa na muumba. Kama ni jambo jema na ni mtu muelewa anaweza badilika vile utakavyo. Tumeona mashababi, matajiri, wababe na majambazi katika dunia wakiwa watiifu kwa wanawake zao. Tumia jinsia yako vizuri na kila kitu kitakuwa shwari.

Nawasilisha.
 
Before sijaoa,i was dreaming kuoa mwanamke atakaemfanana mama yangu kitabia,but siku zote huwezi kupata mwenzi ambae ni perfect kama na wewe ulivyo na mapungufu ingawa wengi hatujitambui,soltn ni kuvumiliana na kuchukuliana mapungufu yenu kama changamoto ya maisha,

usione wazazi wetu wanafanya sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya ndoa zao ukadhani mchezo.mfano kesho wazazi wangu nashukuru Mungu wapo wote wanatimiza miaka 50 ya ndoa yao najiuliza how about me?:what::what::what::what:
 
daaa hyo imenitokea sana kuna dem flan hvi mwanzon sikumkubali na nlikua simuelew kabisaa ila baada ya kunisumbua kwa mda mrefu nikajikuta namkubali mbaya hata sjui kwanin
Ndiyo maombi yake yanajibiwa mkuu hehehe.....yaani ukianza kufikiria uvumilivu na mapenzi aliyokupa unaanza kumuona kuwa ni mmoja wa wachache sana ambao usingependa kumuacha aende zake.
 
Ndiyo maombi yake yanajibiwa mkuu hehehe.....yaani ukianza kufikiria uvumilivu na mapenzi aliyokupa unaanza kumuona kuwa ni mmoja wa wachache sana ambao usingependa kumuacha aende zake.
kipind hcho nlikua na dem mwingne nlikua hata simuwaz kabisaaa ila ghafla tu vitu vilibadilika
 
Before sijaoa,i was dreaming kuoa mwanamke atakaemfanana mama yangu kitabia,but siku zote huwezi kupata mwenzi ambae ni perfect kama na wewe ulivyo na mapungufu ingawa wengi hatujitambui,soltn ni kuvumiliana na kuchukuliana mapungufu yenu kama changamoto ya maisha,usione wazazi wetu wanafanya sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya ndoa zao ukadhani mchezo.mfano kesho wazazi wangu nashukuru Mungu wapo wote wanatimiza miaka 50 ya ndoa yao najiuliza how about me?:what::what::what::what:

Hongera kwa wazazi wako mkuu...Haya mambo ya mapenzi hayana kocha. Ni hekima/busara na uvumilivu ndivyo vya kutusaidia. Unaweza kuwa na PhD ya saikolojia ya binadamu lakini bado ukawa na mitihani mizito mno katika mapenzi yako. Kila mtu ana hadithi yake na njia yake atakayoipitia. Hakuna maisha ya mtu mmoja yanayofanana na ya mwingine kwa 100%. Kwahiyo hatuwezi hata iga wazazi wetu hehehe. Kila mtu ana mtihani wake. Tufunge mkanda.
 
Kila Mara huwa nasema wanawake wana nguvu kubwa ya kuweka mahusiano yawe ya furaha kwa nafasi zao. Bahati mbaya wao wanakimbilia kwenye usawa tu. Kadiri wanavyodai usawa ndiyo mahusiano yanavyozidi kuvunjika

Your so junior to know this ukikua utaelewa pole sana mkuu
 
Mleta mada umeleta kitu chenye ukweli kabisa, wanawake huwa wanapenda zaidi hata kama ni siku ya kwanza tu umemtokea, hapo usiku halali na wala chakula hakipiti. Sasa tatizo linakuja pale mwanaume haoneshi hata kama kapenda na kufa kabisa, unakuta yupo normal kabisa hadi unajiuliza huyu mtu jana kanitokea akimaanisha au ndio kunijaribu tu, mwanaume hapigi simu hovyo wala haoneshi papara.

Sikilizia hayo maneno ya lawama kwa binti hadi utakoma. Wakati mwanamke anawaza 1 tu kichwani, lakini mwanaume anawaza 2 au zaidi. Ila dawa yenu ni kuwapotezea tu ukijidai na wewe upo normal tu huoneshi kupenda sana, wenyewe mnachangamka, ila tatizo wanawake wanashindwa kuficha hisia zao.
 
Alola

Unatudanganya kutetea tamaa za wanaume ili watu wakubali mahusiano yasiyo na upendo. Je ikitokea mpk hiyo baadae huyo bwana hampendi mwanamke atamlipaje fidia ya muda aliompotezea?
 
Last edited by a moderator:
Unatudanganya kutetea tamaa za wanaume ili watu wakubali mahusiano yasiyo na upendo. Je ikitokea mpk hiyo baadae huyo bwana hampendi mwanamke atamlipaje fidia ya muda aliompotezea?

ningeshangaa asingetokea mtu kama wewe kuleta maoni kama haya..na unajua nini? ,,kuna neno umeliweka ambalo ndo msingi wa matatizo yenu..."fidia"..mnaingia katika mahusiano mkiwa mnawaza malipo na fidia..sometimes heartbreak ndo fidia iliyo halali kwenu
 
mada ipo sahihi sana ingawa nadhani ina tatizo la choice of words ndio maana wengine wanaipinga..kinachotokea sio kuwa mwanamme mwanzoni anakuwa hapendi ila anapenda baadae..la hasha..from the very beginning mwanamme anapenda, to begin with, asilimia 98 ya mahusiano katika jamii zetu za kiafrika yanaanzishwa na mwanamme, right?

sasa kinachotokea ni kuwa mwanzoni ingawa mwanamme anakuwa kapenda still anakuwa very much reserved to some extent..hii inatokana na kuwa wanawake walio wengi (sijasema wote) huwa wana tabia ya kuleta maringo, nyodo, na kunata pale wanaporealize kuwa jamaa kafa kaoza..so mwanamme anakuwa anaweka kinga flani ingawa moyoni ndo keshazama.

Sababu nyingine ni kuwa by nature wanaume huwa tuna-internalize vitu..zikiwemo feelings...mwanamme anaweza akakaa mwaka bila kumwambia mkewe "nakupenda" lakini utakuta hiyo nakupenda anaitamka kila siku moyoni..sasa kwa mwanamke asiyeelewa kuwa wao wana-externalize na sie tuna-internalize issues atadhani mume hampendi kumbe ni kinyume chake

sasa as time goes on taratibu mwanamme, kwa sababu ya mazoea na kwa kutaka kucope na mkewe ambaye haishi kumwambia anampenda, basi ataanza kureveal feelings zake kwa maneno na kwa matendo..sasa hapo sio kuwa kipindi hicho ndo kaanza kupenda, hapana. ni kuwa hapo ndo kaanza kufunguka.
 
ningeshangaa asingetokea mtu kama wewe kuleta maoni kama haya..na unajua nini? ,,kuna neno umeliweka ambalo ndo msingi wa matatizo yenu..."fidia"..mnaingia katika mahusiano mkiwa mnawaza malipo na fidia..sometimes heartbreak ndo fidia iliyo halali kwenu

Mbona unapagawa hivyo, kwasababu time huwa haifidiwi ndo maana nimeuliza. Unakuwa umeyasimamisha maisha ya mtu, kuna mambo ya maana ambayo angefanya kama usingekuwepo na wengine mmewazalisha kabisa. Mtaendelea kuchunwa mkidhani wanasubiri kupenda
 
Tumewasikia! tutaanza kuyasikilizia mapenzi yenu kichwani kama stim za pombe sio moyoni.
 
Back
Top Bottom