Wanaume wa tabia hii wanasikitisha sana

Wanaume wa tabia hii wanasikitisha sana

Muwazi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2014
Posts
355
Reaction score
81
Wana Jf, ni jambo ambalo naona kama ni kero kwa wanaume wenye tabia kama hii. Unakuta mwanaume ambaye ni baba wa familia mwenye watoto wakubwa wa kiume na kike ambapo wakike baadhi wameolewa na wakiume pia baadhi wameoa. Sasa unakuta mwanaume kama huyu anapanga kuoa mke wa pili jambo ambalo ni hiari kwa kila mtu. Lakini cha ajabu na cha kusikitisha sana ni kwamba baba kama huyu anamuoa mtoto mdogo ambaye ana umri wa miaka 16 ambaye ni rika ya mtoto wake wa wa nne hivi na kimuweka ndani kama mke wake. Hapa nashindwa kuelewa mwanaume kama huyo anakuwa anawaza nini kufanya jambo kama hili. Kwa upande mwingine pia nawalaumu wazazi wa mtoto anayeolewa maana sijui ni tamaa ya mahari ama nini kukubali mtoto wa umri huo kuolewa na baba mzima kama huyo mwenye mke na watoto na wajukuu. Endapo ingekuwa ati mtoto alitoroka na akakataa kuwa yeye anaolewa na huyo licha ya wazazi kukataa basi wasingekuwa lawamani lakini sasa ni jambo ambalo limepangwa na mahari kutolewa kisha kupanga siku ya kwenda kwake na kufuatwa rasmi. Hili nimelishuhudia bila kusimuliwa na mtu yeyote. Nawasilisha kwenu wana Jf.
 
Sawa umesikitika, Ila umechukua hatua gani kuweka mambo sawa?
 
Una watoto wa kike wangapi? Una experience gani kuhusu malezi ya watoto hao wa kike? Tabia za kulaumu tu bila kutoa suluhisho naona ni kama mipasho flani flani hivi
 
Wanaume hawajuagi kitu kimoja...........Sisi wanawake ukitaka asireact sana ni pale utakapomletea mwanamke mzuri zaid ya mkeo/bebi wako, pale sauti itatoka ya kulalamikiwa lakin moyoni atakubali kitu ulichokibeba ni zaid yake...
What hurt us the most unaenda kuchukua katoto kadogo, sura mong'onyo yani pale mwanamke anaumia roho sanaa na kuona umemdhalilisha,Umekosa nini mpaka ukaenda kubeba kituko

Advice....Ukitaka kuchepuka chukua kitu chenye hadhi ya juu kuliko uliyenaye ili usimuumize sana mkeo/darling sweetbeb
 
Ningependa kujua
1. Mzee huyo ni dini gani (pengine diniyake inaruhusu kuongeza mke)
2. Pia ningependa kujua ni kabila gani au amezungukwa na jamii gani...
Kuna kitu kinaitwa "invisible walls"...yani, kwenye maisha kuna walls ambazo hazionekani kwa macho lakini zina-shape tabia zetu na kutulazimisha kukaa "njiakuu" bila hata sisi kujua...maranyingi hizi hutokana na jamii inayotuzunguka au imani zetu/dini...unaweza kukuta huyu mzee dini yake na jamii inayomzunguka inamruhusu kuoa msichana wa miaka 16.
 
Nakushauri uka report hili swala Ustawi wa jamii zilizo karibu nawe.

Ni kinyume na sheria kuoza msichana chini ya umri wa miaka
18.
 
Wana Jf, ni jambo ambalo naona kama ni kero kwa wanaume wenye tabia kama hii. Unakuta mwanaume ambaye ni baba wa familia mwenye watoto wakubwa wa kiume na kike ambapo wakike baadhi wameolewa na wakiume pia baadhi wameoa. Sasa unakuta mwanaume kama huyu anapanga kuoa mke wa pili jambo ambalo ni hiari kwa kila mtu. Lakini cha ajabu na cha kusikitisha sana ni kwamba baba kama huyu anamuoa mtoto mdogo ambaye ana umri wa miaka 16 ambaye ni rika ya mtoto wake wa wa nne hivi na kimuweka ndani kama mke wake. Hapa nashindwa kuelewa mwanaume kama huyo anakuwa anawaza nini kufanya jambo kama hili. Kwa upande mwingine pia nawalaumu wazazi wa mtoto anayeolewa maana sijui ni tamaa ya mahari ama nini kukubali mtoto wa umri huo kuolewa na baba mzima kama huyo mwenye mke na watoto na wajukuu. Endapo ingekuwa ati mtoto alitoroka na akakataa kuwa yeye anaolewa na huyo licha ya wazazi kukataa basi wasingekuwa lawamani lakini sasa ni jambo ambalo limepangwa na mahari kutolewa kisha kupanga siku ya kwenda kwake na kufuatwa rasmi. Hili nimelishuhudia bila kusimuliwa na mtu yeyote. Nawasilisha kwenu wana Jf.

Unawasilisha kwetu tufanye nini. Wewe binafsi umechukua jitihada gani juu ya hilo swala.?
Maana umeshuhudia kwa macho yako bila kuambiwa na mtu nilitegemea ungekuwa mtu wa kwanza kulipoti katika vyombo husika kama Polisi ustawi wa jamii
 
Huyo amefanya kosa sana kiasi kwamba ilifaa ashitakiwe kwenye vyombo husika.
 
Umekesha kwenye kigodoro na kigele gele ukapiga,leo unakuja kufungua thread eti wanakusikitisha!!
Madawati ya jinsia yako kila kona siku hizi,ulienda kuomba msaada mkazuia hili?
 
Ni ubazazi wa kiwango cha juu 😠😠😠😠😠😠😠😠
 
Wanaume hawajuagi kitu kimoja...........Sisi wanawake ukitaka asireact sana ni pale utakapomletea mwanamke mzuri zaid ya mkeo/bebi wako, pale sauti itatoka ya kulalamikiwa lakin moyoni atakubali kitu ulichokibeba ni zaid yake...
What hurt us the most unaenda kuchukua katoto kadogo, sura mong'onyo yani pale mwanamke anaumia roho sanaa na kuona umemdhalilisha,Umekosa nini mpaka ukaenda kubeba kituko

Advice....Ukitaka kuchepuka chukua kitu chenye hadhi ya juu kuliko uliyenaye ili usimuumize sana mkeo/darling sweetbeb

Ha!ha.. Kwa hiyo wewe ukiletewa zaidi yako unaridhika?
 
Wanaume hawajuagi kitu kimoja...........Sisi wanawake ukitaka asireact sana ni pale utakapomletea mwanamke mzuri zaid ya mkeo/bebi wako, pale sauti itatoka ya kulalamikiwa lakin moyoni atakubali kitu ulichokibeba ni zaid yake...
What hurt us the most unaenda kuchukua katoto kadogo, sura mong'onyo yani pale mwanamke anaumia roho sanaa na kuona umemdhalilisha,Umekosa nini mpaka ukaenda kubeba kituko

Advice....Ukitaka kuchepuka chukua kitu chenye hadhi ya juu kuliko uliyenaye ili usimuumize sana mkeo/darling sweetbeb

SiSi wanaume tunachojali sana ni mapenzi ya dhati, kama mtu anakupa roho inapenda, anakupeleka sayari ya mars basi uzuri wake ni bonus tu, cha msingi ni "ufundi". Ndio maana michepuko inakuwaga ya kawaida sana (kiuzuri) ukiifananisha na njia kuu.


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Wanaume hawajuagi kitu kimoja...........Sisi wanawake ukitaka asireact sana ni pale utakapomletea mwanamke mzuri zaid ya mkeo/bebi wako, pale sauti itatoka ya kulalamikiwa lakin moyoni atakubali kitu ulichokibeba ni zaid yake...
What hurt us the most unaenda kuchukua katoto kadogo, sura mong'onyo yani pale mwanamke anaumia roho sanaa na kuona umemdhalilisha,Umekosa nini mpaka ukaenda kubeba kituko

Advice....Ukitaka kuchepuka chukua kitu chenye hadhi ya juu kuliko uliyenaye ili usimuumize sana mkeo/darling sweetbeb

Sikubaliani na wewe hata kidogo! Unapozungumzia mwanamke mzuri kuliko wewe una maanisha kitu gani? Mwanaume kukuchagua wewe kuwa mkewe ni kwamba wewe ni bora kwa nafsi yake kuliko wanawake wengine, kukubali mwanaume kuchepuka na mwanamke mwingine kwa vile ni mzuri kuliko wewe ni kujishusha na kutojua thamani yako.
 
v2 hv c vya kuzungumza bila kufanya scientifc analysis ya jamii husika. Mwsho utaishia kulalama bt nah action u can take xo far...mfikishe hyo babu ustaw wa jamii utasaidiwa. *The barking dogs seldom bite*
 
SiSi wanaume tunachojali sana ni mapenzi ya dhati, kama mtu anakupa roho inapenda, anakupeleka sayari ya mars basi uzuri wake ni bonus tu, cha msingi ni "ufundi". Ndio maana michepuko inakuwaga ya kawaida sana (kiuzuri) ukiifananisha na njia kuu.


Sent from my iPhone using JamiiForums app

Sasa huyo mtoto atakufikisha wapi? Sio kweli msemo wako. Tafuta mwanamke mwenye mawazo ya kiutu uzima.
 
Wanaume hawajuagi kitu kimoja...........Sisi wanawake ukitaka asireact sana ni pale utakapomletea mwanamke mzuri zaid ya mkeo/bebi wako, pale sauti itatoka ya kulalamikiwa lakin moyoni atakubali kitu ulichokibeba ni zaid yake...
What hurt us the most unaenda kuchukua katoto kadogo, sura mong'onyo yani pale mwanamke anaumia roho sanaa na kuona umemdhalilisha,Umekosa nini mpaka ukaenda kubeba kituko

Advice....Ukitaka kuchepuka chukua kitu chenye hadhi ya juu kuliko uliyenaye ili usimuumize sana mkeo/darling sweetbeb

Hapo anakuwa amesalimu amri...nice one!
 
Back
Top Bottom