Wanaume wa Kibongo, utasa na kuelekea mwaka 2014

mkuu kuquote thread ndefu kama hizi mnatuumiza sana sisi tunaotumia device ndogo! plea jamani ni bora mtu u-reply kawaida kuliko kureply with quote.. please wana jf tusikilizane kwa hili!

Yaani wanakera kweli.
 
Nadhani tuwe makini na hizi tafiti pia, au kwa maneno mengine 'hizo sample' ni muhimu kuwa makini nazo.
Kwa ujumla hao waliopimwa kwa sehemu kubwa ni kutoka hospitali za Muhimbili na Tumani. Na ni obvious hao wanaokwenda huko wanatoka 'class' flani. Si rahisi kwa mtu kutoka Vingunguti ndani huko ama Tandika taa nyekundu kuchukua uamuzi wa kupima Muhimbili au Tumaini Hospital.

Lakini hapa si-rule out kwamba watu kutoka maeneo ya Uswazi ni salama sana, lakini ni vyema kuyafikia makundi yote ili kujiridhisha. Na mimi huwa napita sana Uswazi...kuanzia Ukonga Mombasa mpaka Mbagala maji matitu, kwa mtazamo wa macho tu bila utafiti ile idadi ya Watoto nayoiona inahitaji utafiti unaojitegemea.

Kwa ujumla maeneo ya Uswazi ni jambo la kawaida kukuta Kijana wa kiume kuanzia miaka 20 'ameshamzalisha' binti, au ukamkuta binti mwenye umri wa miaka kuanzia 19 ana mtoto. Akipona huyo Mtaani ana sifa kubwa!!
 
Iko shida hpo kuvaa nguo z kubana ni tatizo, sasa hawa masharobaro c watakua janga la taifa mana wanabana vyombo mpka havipumui cz nguo z fashion
 
Ndo uende ukapimwe ili ujue mbivu na mbichi. Mkuu EMT umeeleza kwa kina sasa mwenye macho na asome na kuelewa kisha wachukue hatua. Huu mfumo dume ni ugonjwa sijui utatibika lini . Wanandoa wenye matatizo ya uzazi mara nyingi husukumiwa mama tena mpaka ndugu humwandama mwanamke . Wanaume badilikeni tunapoelekea 2014.

Mfumo dume sasa wadaiwa kuwamaliza wanaume.
 
Kuna tips mbalimbali huwa zinatolewa za watu kuongeza nguvu za kiume ikiwemo aina ya vyakula,mazoezi na mfumo mzima wa maisha kwa ujumla matokeo yake wengi wao hukimbilia kununua dawa kwa kufikiri kwambakuchelewa kumwaga ndio kuwa nguvu kumbe unaweza ukachelewa na still sperms zako zisiwe na nguvu ya kurutubisha yai.,kwa mwenye akili kuna mengi ya kujifunza hapa.
 
Back
Top Bottom