Wanaume tuoneeni huruma dada/mama zenu

Wanaume tuoneeni huruma dada/mama zenu

Mzigua90

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2014
Posts
38,391
Reaction score
88,769
Nikiwa kama mhanga wa mwanamke alieachiwa matunzo ya mtoto bila msaada wa baba naumia sana. Hivi wanaume huwa mnawaza nini mnapotupa adhabu ya kulea watoto peke yetu na wewe baba ukiwa hai na unajiweza? Hata kama hujiwezi basi kumjali mtoto wako japo kwa kuulizia maendeleo yake mtu anashindwa kabisa.

Hivi kina kaka mmejiuliza nyie baba zenu wangewakimbia mngekuwa wapi sasa hivi? Mnajua ni chuki gani mnaweka kwa watoto wenu mliowakataa? Mnajua ni laana gani mnapata kwa Mungu kwa kukataa kutimiza wajibu wenu kama wazazi? Au mnatukomoa kwa sababu mama hawezi kumuacha mtoto wake nyuma hata apate tatizo gani?

Labda wewe na mama wa mtoto hamko sawa lakini ile hasira ya ninyi kutokua sawa baba usimkomeshe mama kwa kuacha kumtunza mwanao ukijua unamkomoa mama, pale unaemkomoa ni mtoto wako ambae ulimtafuta kwa mapenzi/tamaa zako mwenyewe.

Naandika nikiwa na uchungu mwingi sana moyoni. Mwanaume usiemtunza mwanao ona aibu na muogope Mungu wako kwa kitendo unachokifanya.
Jiulize ingekua ni dada yako au mwanao ameachwa na mwanaume alee mtoto peke yake ungejisikiaje?

KARMA IS A BITCH. Ukinifanyia mimi leo wakati unao dada na watoto wa kike jua itakuumiza na wew kwa mmoja kati ya hao kufanyiwa kama unavyofanyia wengine.

Baba mtoto wangu nimeshamlilia Mungu juu yako na nina hakika huyu mtoto ulieniachia nimlee peke yangu atanifuta machozi siku moja na utatamani akutambue kama baba yake utakua umeshachelewa.

Kaka/baba zangu baba Diamond akawe mfano kwenu, Obama aliekataliwa na baba yake mwishoni alikuja kuwa Rais wa Marekani/dunia.
 
Pole sana, wanaume tusikimbie watoto wetu hata kama walikuja bila ridhaa na mipango yetu. Huwezi kuikimbia damu yako hata kama uchumi ni mbaya, ni dhambi na uonevu mkubwa sana kwa mtoto!!

Asante sana. Najiuliza hivi wanaume wa hivyo huwa wanamuogopa Mungu kweli?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mwanamke unatakiwa uwe smart pia, usichukue mimba huku ukiwa unamtegemea mtu asiyeeleweka na sio mume... au kuwa na kazi ya kukupa kipato cha kumtunza mwanao kabla ya kuchukua mimba nje ya ndoa.. japo wanaume wana makosa ila mnaweza kupunguza extent ya watoto kulelewa kwenye umasikini kwa kuwa makini
 
Pole sister! ila kuna kitu watu huwa hawatambui,wanaume huwa si wepesi wa kuongea yanayowasibu kwenye mahusiano ila wanaume wanateswa sana na wanawake japo siungi mkono tabia ya kukimbia familia ila kuna wanawake pasua kichwa aisee,nina jamaa yangu yeye toka ameoa ana miaka mitatu,mke hata wakizinguana kidogo anasepa kwao miezi 6 mpaka karibia mwaka.sasa saa hizi ana ujauzito huyo mdada baada ya kua akibeba unaaribika,alafu makosa yenyewe yanamtoa hom kwake ni makosa ya kawaida tu,kuna muda jamaa huwa anatamani hata amuache kabisa sasa hali hyo ikiendelea si ipo hatar ya jamaa kutelekeza mke na mtoto? sema wengi huwa mnatumia watoto kama mwavuli,ukisha kua na familia inabidi ujifunze kukaa vizuri na mwenzio kwa ajili ya ustawi wa familia,wanaume sio watu wa ku take action kirahisi ila akichukua hua aangalii side effect ya uamuzi anaochukua.Maudhi yakizidi familia huwa haina uzito sana hasa katika kuchukua uamuzi mgumu
 
Mwanamke unatakiwa uwe smart pia, usichukue mimba huku ukiwa unamtegemea mtu asiyeeleweka na sio mume... au kuwa na kazi ya kukupa kipato cha kumtunza mwanao kabla ya kuchukua mimba nje ya ndoa.. japo wanaume wana makosa ila mnaweza kupunguza extent ya watoto kulelewa kwenye umasikini kwa kuwa makini
Mimi nawalaumu wanawake katika hilo tu, they are in control of their bodies, wanajua lini wapo safe, lini wanaweza kujiachia, wanaweza kuamua huyu nimpe coz anafaa, huyu hanifai hivyo he won't test my bits.

Ninachoshindwa kuelewa, kwa nini(pamoja na kuwa na full control ya miili yao), kwa nini mtu anabeba mimba ya mtu asiyeonyesha kuwa nae, kwa nini wanategesha mimba? Hiyo weakness kwa dada zetu inawatafuna, wanapata mzigo wa kulea watoto peke yao...so sad!...

Lakini pamoja na hayo, mwanaume kumuachia mwenzako majukumu ya malezi no dhambi kubwa!!
 
Mwanamke unatakiwa uwe smart pia, usichukue mimba huku ukiwa unamtegemea mtu asiyeeleweka na sio mume... au kuwa na kazi ya kukupa kipato cha kumtunza mwanao kabla ya kuchukua mimba nje ya ndoa.. japo wanaume wana makosa ila mnaweza kupunguza extent ya watoto kulelewa kwenye umasikini kwa kuwa makini
Nikisikiaga hizi kauli namkumbuka binti mmoja aliyempiga kofi daktari baada ya kuambiwa anaujauzito, alikuwa makini sana ila ikatokea, kwahiyo ndugu haya mambo hutokea tu hata kwa walio ndoani, cha msingi ni mkumbuke tu hizo damu zenu muwe part of their lives no mata what!! Hebu ufikirie tu ingekuwa ni wewe umetelekezwa hivyo ungejisikiaje?
 
Hii ishu ikishatokea cha msingi ni sapoti kutoka kwa familia yako, ni hiko tu ndiyo kitafanya makosa yaliyotokea usiyajutie sana.

Mwanaume anayesusa mtoto huku wewe uko sawa kwa kila kitu ni utoto umemshika anajiona kuna vitu hajamalizia.
 
Mwanamke unatakiwa uwe smart pia, usichukue mimba huku ukiwa unamtegemea mtu asiyeeleweka na sio mume... au kuwa na kazi ya kukupa kipato cha kumtunza mwanao kabla ya kuchukua mimba nje ya ndoa.. japo wanaume wana makosa ila mnaweza kupunguza extent ya watoto kulelewa kwenye umasikini kwa kuwa makini
kweli kabisa mkuu mwenyewe najikusanya kabisa kabla sijapiga tukio akitoa fine ni kama bonus tu ila mwanaume sio wa kutegemea kabisa baba yao shetani
 
shosti ila na wewe kumbuka ulikosea kuzaa na mume wa mtu so kubali makosa komaaa na matokeo
huwezi kuokota embe kwenye mnazi .ulitaka kukimbia na hauna break????????
 
Dah!! Dada Umeandika kwa Hisia sana
Angalia Usijiue Ukiona Umeelemewa sana Tafadhali Tuwasiliane Naweza Saidia

Jamani Waloekaji Tukumbuke kufua Na kuanika pia ikibidi. Tusikimbie Majukumu.
 
Makosa yanaweza kuwa ya mwanamke,mwanaume au wote wawili lakini athari kubwa inakuja kwa mwanamke na mtoto..So wadada muwe makini..Sio kila mlowekaji ni mfuaji..Wengine wanaloweka tu na kuendelea na shughuli zao..
Happy new year.
 
Nikiwa kama mhanga wa mwanamke alieachiwa matunzo ya mtoto bila msaada wa baba naumia sana.
Hivi wanaume huwa mnawaza nini mnapotupa adhabu ya kulea watoto peke yetu na wewe baba ukiwa hai na unajiweza? Hata kama hujiwezi basi kumjali mtoto wako japo kwa kuulizia maendeleo yake mtu anashindwa kabisa. Hivi kina kaka mmejiuliza nyie baba zenu wangewakimbia mngekuwa wapi sasa hivi? Mnajua ni chuki gani mnaweka kwa watoto wenu mliowakataa? Mnajua ni laana gani mnapata kwa Mungu kwa kukataa kutimiza wajibu wenu kama wazazi? Au mnatukomoa kwa sababu mama hawezi kumuacha mtoto wake nyuma hata apate tatizo gani? Labda wewe na mama wa mtoto hamko sawa lakini ile hasira ya ninyi kutokua sawa baba usimkomeshe mama kwa kuacha kumtunza mwanao ukijua unamkomoa mama, pale unaemkomoa ni mtoto wako ambae ulimtafuta kwa mapenzi/tamaa zako mwenyewe.
Naandika nikiwa na uchungu mwingi sana moyoni. Mwanaume usiemtunza mwanao ona aibu na muogope Mungu wako kwa kitendo unachokifanya.
Jiulize ingekua ni dada yako au mwanao ameachwa na mwanaume alee mtoto peke yake ungejisikiaje?
KARMA IS A BITCH. Ukinifanyia mimi leo wakati unao dada na watoto wa kike jua itakuumiza na wew kwa mmoja kati ya hao kufanyiwa kama unavyofanyia wengine.
Baba mtoto wangu nimeshamlilia Mungu juu yako na nina hakika huyu mtoto ulieniachia nimlee peke yangu atanifuta machozi siku moja na utatamani akutambue kama baba yake utakua umeshachelewa.
Kaka/baba zangu baba Diamond akawe mfano kwenu, Obama aliekataliwa na baba yake mwishoni alikuja kuwa Rais wa marekani/dunia.
ilikuwaje akakuachia watoto, mlioana kwa ndoa? kama jibu ni ndio basi ujilaumu kwa kutotunza ndoa hadi mkaachana. kama haukuoana naye kwa ndoa, jilaumu kwa kuwa malaya kuvua chupi ovyo hadi jamaa kakuzalisha na kukudampu akaenda kuoa ampendaye. ilaani ile siku umevua pichu na sio kuwalaani na kuwachukia wanaume.tatizo wadada mmezidi umalaya na kuchagua chagua, nataka kila mwanaume mnayemtamani awaingilie, na kwa jinsi sisi wanaume tulivyo, mwanamke mrahisi huwa tunamtumia kwa starehe tu ila sio wa kudumu naye kwasababu tunajiuliza amekuwa mrahisi kwangu hivi atakuwa mrahisi au amekuwa mrahisi kwa wangapi. hivyo punguza umalaya uache kulalamika. utamu uliutaka mwenyewe hayo ndo matunda yake uyale sasa.
 
Jieleze vizuri kwa nn amekukimbia, sio unakuja kulaumu hapa, wewe ulifikiri kuwa na mtoto wake ndo iwe kigezo cha kuto kukupiga chini!
wanawake wengi mkishazaa tu, mnaanza kujionyesha tabia zenu halisi, mwanaume anakuvumilia hubadiliki anakupiga chini. Ili ulee mwenyewe. Hata kama una mtoto naye, utiifu wa mapenzi kwa mwenzio ni muhimu. Au ulifikiri mtoto wake kwako umeweka kitegauchumi bila mapenzi?
 
Back
Top Bottom