Wanaume tu wadhaifu kwa wanawake

Wanaume tu wadhaifu kwa wanawake

Retired

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2016
Posts
50,214
Reaction score
96,337
Juzi kati nilisafiri kutoka Dar kuja Tanga. Kando yangu kiti kingine, alikaa baba mtu mzima mtanashati. Kidogo akaja binti/mwanamama wa umri wa kijana---25-30's. Kufika Kibaha Mailimoja, mwanaume akanunua peas manne hivi (unajua ni ghali kidogo-1000 Tsh/each). Jicho langu ndani ya habari, akachukua mawili akampa mwanamama huyo. Akapokea, akaanza kula.

Tunaondoka, Lo! Salale, konda akapangua seat namba. Mwanamama akahamia kiti cha mbele kabisa. Akaletwa mtoto wa miaka kama 10 hivi-mjukuu wa huyo baba let say. Baba akanunua vitu vya kula kula, huyo mtoto/mjukuu wake hakumpa hata kidogo kama alivyofanya kwa mwanamama yule. Na hawakuwasiliana na mwanamama huyo mpaka tunafika Muheza mwanamama akateremka.

Nikajisemea kuwa wanaume tu dhaifu kwa wanawake!
 
tehe tehe tehe kama namuona vile babu wa kitanga!
 
Mzee anaendekeza chini hahaha kaona mtoto atamsaidia nini
 
Wivu tu, baada ya kuona mwenzio kabahatika, mate yakakutoka, kila move ukawa unakodolea macho tu
 
Konda alimpokonya tonge mdomoni, konda Mungu anakuona ujue
 
Safi sana

hii mizee inaoonga wee sisi makapuku tukienda na sound zetu tunatolewa baru kama mbwa koko shenzi type.

nilipokuwa naenda mwanza toka arusha... nafika babati kuchimba dawa kurudi namkuta mbaba kakaa sehemu niliyokuwepo.... nafika akanikonyeza mi nikaelewa mchezo.... sasa kumbe yule mdada alikuwa mwanafunzi anaenda shule..... sasa na upole wangu nikakubali.... sehemu yake alikuwa kakaaa muhindi ahhhh ile safari niliichukua sana sitaki ijirudie
 
Idhaifu unategemeana na kiwango. Ndio maana kuna wala mazoba kabisa... ambao kila kitu wakiambiwa na mwanamke ni ndio... na kuna wenye kujielewa...
 
Hakuna udhaifu hapo Mkuu.. Nature of men.. Huwa wanainvest kwenye maslahi...,
 
Mimi sina udhaifu na wanawake.

Najielewa na kujitambua mno hadi huwa naogopa.
 
ulifatilia yote A-Z..? je kama huyo mzee alimpa huyo unaemuita mjukuu wake na alikataa(kumbuka kuna kukataa kwa ishara pia)
 
Back
Top Bottom