Wanaume na wazazi wenye watoto wa kiume, hii imeshawahi kuwatokea?

Wanaume na wazazi wenye watoto wa kiume, hii imeshawahi kuwatokea?

Binti wa zamani

Platinum Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
11,763
Reaction score
27,149
Ulivyokua kijana na kipindi cha balehe (teen age), mahusiano yako na baba yako yalikuwaje?

Nina watoto wa kiume wapo kipindi cha balehe na hawaivi kabisa na baba yao, japo hapo zamani walikua wana ukaribu sana. Ugomvi hauishi, kila kitu kidogo lazima watoto wapate mihemuko au wapate hasira na baba yao naye anakasirika (they trigger each other kupita kiasi). Watoto pia hawana uoga kuongea mbele ya baba kama wakiambiwa kitu na hawana utayari (japo huwa hawavunji heshima au kutukana).

Hii hali ni mpya (kwa miaka kadhaa sasa) tokea waingie kwenye balehe (teen years). Wazazi ambao mmeshalea male teens (vijana wa kume wakiwa kwenye balehe) uzoefu wenu ulikuwaje na je baada ya balehe, ukaribu na mahusiano huwa yanarudi tena kama zamani?

Na wanaume wa JF, vipi na wakati unakua mahusiano yako na wazazi yalikuwaje?

Asanteni na Jumapili njema!

Father and son.jpg
 
Hiyo hali haiepukiki ila ukubwa wake unatagemeana na mizizi iliyowekwa kipindi cha utoto wao na baba yao.

Mtoto ukimchekea sana utotoni akahisi ni marafiki basi katika balehe yake lazima atakupanda kichwani akihisi mnawezana.

Mtoto hapaswi kumuogopa mzazi ila kunapaswa kuwe na uelewa kuwa japo mzazi haogopewi ila nafasi yake ya uzazi haina mjadala, kwamba anachoamua mzazi ndio cha mwisho na hakihojiwi.

Haipaswi mtoto kuwa na nafasi yeyote ya kukaidi, kuhoji ama kujibizana na mzazi as long as bado anaishi katika himaya ya mzazi na bado anategemea mzazi.

Pia watoto wanapaswa kutambua kuwa wazazi wote wawili ni kitu kimoja sio kwamba mmoja ni 'fair' na mwingine ni mkuda.
Nyumba nyingi utakuta mzazi mmoja anajifanya mwema sana hasa mama na kumrushia uhaini wote baba. Hii inajenga taswira mbaya kwa baba mbele ya watoto.

Inapaswa itambulike kwa watoto wote kuwa maamuzi ya wazazi wote ni mamoja na kuwa ikitokea hukumu/agizo/maamuzi ni la wazazi wote.
Inapaswa wazazi waepuke kubishana juu ya maamuzi ya watoto wao mbele ya watoto. Hata kama hamkubaliani kuhusu jambo, inapaswa mfanyie pembeni mabishano sio mbele ya watoto.

Kubwa na la muhimu zaidi, mtoto hatakiwi kuwa na uhuru wa kuongea ujinga wowote juu mzazi mmoja kwenda kwa mzazi mwingine pasi na uwepo wa mzazi huyo. Yani haijalishi mtoto kakerwa kiasi gani, hatakiwi kuwa na ujasiri wa kwenda kuongea shiti juu ya baba mbele ya mama na mama nae aka support.

Nguvu ya ulezi bora inapatikana kwa umoja wa wazazi wote wawili.
Sio baba anatoa hukumu/adhabu, mama anamuita mtoto pembeni na kumbembeleza.
 
Back
Top Bottom