Its Pancho
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 14,196
- 22,596
Jumatatu asubuhi mida ya breakfast nilitoroka kwenye ka mishe kangu kidogo nikaenda kufungua kinywa kidogo pale Dodoma kuna mgahawa upo karibu na TRA kwa wanaopajua.
Ok twende mbele,au basi mbele kote kwanini huko?
Well mdogo mdogo. Nikacheki meza ambayo ni empty lakini nikakosa,kutokana na kwamba almost meza zote unakuta kuna mtu mmoja au wawili pengine mpaka watatu. Hivyo nikaangaza macho mpaka mwisho wa kona kabisa.
Nikaenda moja kwa moja kukaa kwani niliona pananifaa zaidi. Mezani hapo alikaa dada mmoja mnene kiasi,miwani yake ya macho,shati la mikono mirefu la blue bahari, suruali ya kitambaa ya blue huku akiwa kachomekea vilifanya karibu watu wengine wote wamtazame kwa kuibia ibia kama mimi. Sikujali nikaenda hapo alipo.
"Dada samahani naweza kukaa kama hutojali" nikaona ni uungwana kuuliza kwani hata nisingeuliza bado ni sawa kwani nakula bure bwana eeh?
Yeye: "hapana"( akajibu kiufupi) sikujali nikakaa kisha nikaagiza nikaanza kukifyeka huku yeye pia yuko bize anakula.
Dakika si nyingi akamaliza kula na kuamka kwenda kunawa nikataka niseme kitu ikabidi nimuwahi
Mimi: "dada, Dadaa samahani naomba nikuulize kidogo"akasimama kisha akageuka halafu akaniangalia kisha akaendelea na safari yake baadhi ya watu wakabaki wananiangalia kwa macho ya "uachage kushobokea watu bwege wewe"
Mtu mzima nikajizoa zoa weee yakaisha.
Well twende mbele sasa,maana nikirudi mtasema kufanya nini sasa? Au basi katikati ndo panafaa sana..😆😆
Week moja mbele siku ya jumapili tu hapa mtaa ninaoishi ndani kuna nyumba tatu na zipo ndani ya uzio.
Moja ninakaa mimi na mbili hazina watu natafutaga sana wapangaji.
Najua wanajf mtamaindi kusikia namiliki nyumba tatu,maana wabongo kwa kukunja hamjambo 😂😂..
Vuuup dalali huyu hapa kaniletea mteja anataka nyumba,nikaona afadhali sasa nyumba ipate mtu angalau hela iende kwenye mafuta si mnajua yamepanda?
Kuuliza mteja mwenyewe ni nani, guess what?
Ni yule yule dada niliekaa naye kwenye mgahawa pale karibu na kazini na akaniletea nyodo huenda alidhani nilitaka kumtongoza.
Aliponiona akaanza
Yeye: "ooh kumbe huyu kaka ndo mwenye nyumba? Namjua huyu afadhali kodi angalau atakuwa ananipa muda kidogo, eeh sa masiku mkaka?"akawa mchangamfu ghafla sana mimi nimenyuti tu nasikiliza.
Nikamwambia short and clear kodi bei yake na wala sipunguzi,alipe au akatafuta nyumba kwengine..
Nadhani alijua nitajirahisisha kama siku ile,labda uzuri wake nitababaika.
Lakini wazee ni pesa ndo inazungumziwa hapo si mnaona?
Kodi alilipa ,na kwa sasa ni mpangaji wangu na tunaishia kusalimiana tu pasipo mazoea mengine yasiyo na msingi..
Muda mwengine ni bora kutulia na kufuata mambo yako kuliko kujirahisisha hovyo hovyo na kujidhalilisha..!
Hata humu jamvini pia vidume vikware nawasihi acheni kuwa na tamaa na wanawake penda unapopendwa, sikiliza unaposikilizwa, zingatia unapozingatiwa.
FUNZO: ukiona pisi kali tumia kondom hata kama umeoa..😂😂
Ok twende mbele,au basi mbele kote kwanini huko?
Well mdogo mdogo. Nikacheki meza ambayo ni empty lakini nikakosa,kutokana na kwamba almost meza zote unakuta kuna mtu mmoja au wawili pengine mpaka watatu. Hivyo nikaangaza macho mpaka mwisho wa kona kabisa.
Nikaenda moja kwa moja kukaa kwani niliona pananifaa zaidi. Mezani hapo alikaa dada mmoja mnene kiasi,miwani yake ya macho,shati la mikono mirefu la blue bahari, suruali ya kitambaa ya blue huku akiwa kachomekea vilifanya karibu watu wengine wote wamtazame kwa kuibia ibia kama mimi. Sikujali nikaenda hapo alipo.
"Dada samahani naweza kukaa kama hutojali" nikaona ni uungwana kuuliza kwani hata nisingeuliza bado ni sawa kwani nakula bure bwana eeh?
Yeye: "hapana"( akajibu kiufupi) sikujali nikakaa kisha nikaagiza nikaanza kukifyeka huku yeye pia yuko bize anakula.
Dakika si nyingi akamaliza kula na kuamka kwenda kunawa nikataka niseme kitu ikabidi nimuwahi
Mimi: "dada, Dadaa samahani naomba nikuulize kidogo"akasimama kisha akageuka halafu akaniangalia kisha akaendelea na safari yake baadhi ya watu wakabaki wananiangalia kwa macho ya "uachage kushobokea watu bwege wewe"
Mtu mzima nikajizoa zoa weee yakaisha.
Well twende mbele sasa,maana nikirudi mtasema kufanya nini sasa? Au basi katikati ndo panafaa sana..😆😆
Week moja mbele siku ya jumapili tu hapa mtaa ninaoishi ndani kuna nyumba tatu na zipo ndani ya uzio.
Moja ninakaa mimi na mbili hazina watu natafutaga sana wapangaji.
Najua wanajf mtamaindi kusikia namiliki nyumba tatu,maana wabongo kwa kukunja hamjambo 😂😂..
Vuuup dalali huyu hapa kaniletea mteja anataka nyumba,nikaona afadhali sasa nyumba ipate mtu angalau hela iende kwenye mafuta si mnajua yamepanda?
Kuuliza mteja mwenyewe ni nani, guess what?
Ni yule yule dada niliekaa naye kwenye mgahawa pale karibu na kazini na akaniletea nyodo huenda alidhani nilitaka kumtongoza.
Aliponiona akaanza
Yeye: "ooh kumbe huyu kaka ndo mwenye nyumba? Namjua huyu afadhali kodi angalau atakuwa ananipa muda kidogo, eeh sa masiku mkaka?"akawa mchangamfu ghafla sana mimi nimenyuti tu nasikiliza.
Nikamwambia short and clear kodi bei yake na wala sipunguzi,alipe au akatafuta nyumba kwengine..
Nadhani alijua nitajirahisisha kama siku ile,labda uzuri wake nitababaika.
Lakini wazee ni pesa ndo inazungumziwa hapo si mnaona?
Kodi alilipa ,na kwa sasa ni mpangaji wangu na tunaishia kusalimiana tu pasipo mazoea mengine yasiyo na msingi..
Muda mwengine ni bora kutulia na kufuata mambo yako kuliko kujirahisisha hovyo hovyo na kujidhalilisha..!
Hata humu jamvini pia vidume vikware nawasihi acheni kuwa na tamaa na wanawake penda unapopendwa, sikiliza unaposikilizwa, zingatia unapozingatiwa.
FUNZO: ukiona pisi kali tumia kondom hata kama umeoa..😂😂