mtoto wa mfugaj
Senior Member
- Jul 18, 2011
- 136
- 29
Kuna tabia imezuka sikuhizi na kadiri muda unavyoenda inajipatia umaarufu kwa baadhi ya vijana wa kiume,tabia yenyewe ni wanaume kuvaa nguo zinazobana na kushika kisawasawa maungo yao hasa ni suruali aina ya model,kama hiyo haitoshi suruali hushushwa chini hivyo kuacha boxer ikionekana,on top of that juu wanavaa tshirt fupi ambayo kila baada ya mda anakua anaipandisha pandisha.hizi ni pozi za kike kabisa,mambo ya kuvaa skin jeans,kuonyesha chupi na kuvaa tshirt fupi na kuanza kuzipandisha pandisha haifai,kama dhumuni la watu wa aina hiyo ni kuvutia mabinti jueni hiyo mbinu imefeli maana baada ya kuwavutia mnajidhalilisha na mnawakera.kijana unatakiwa uwe msafi na mwenye kujali hivyo ndivyo utawavutia hao warembo.nimemaliza.pamoja tunajenga nchi.