Emc2
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 16,808
- 16,836
Nimekuwa na muda mrefu sana ninafuatilia mambo ya siasa na nimegundua ni mchezo mchafu sana.
Mchezo huu unahatarisha maisha si ya wanasiasa bali ya wananchi wasio na hatia.
Nimekua nikifikiria hivi hawa wanasiasa wanapata faida gani wanapozunguka huku na huku majukwaani wakinadi sera zao, hivi kweli ni wazalendo na wanachokiongea ndio hicho? Mwisho wa siku nimeona kuwa sio wazalendo na wala sio watu wanaojinadi kuwa ni wakombozi.
Kunavyama hapa nchini zaidi ya 5 kila mmoja lengo lake ni kutawala nchi. Huku nyuma ya pazia wako na ajenda yao ya siri na kuwahadaa watz kuwa wao ni wakombozi. Wakitumia shida na changamoto za maisha kama kigezo cha wao kupewa nafasi ya utawala.
Mambo ya muhimu ya maendeleo hawayapigii kampeni wanakaa kimya.
Mfano tu mmoja tunazoezi la sensa kitaifa, wanasiasa wamekaa kimya hakuna hata mmoja anaye ongelea hilo. Zaidi tu kueneza propaganda mbalimbali ambazo hazimsaidii mtanzania.
Haya ni maoni yangu kuwa wanasiasa wanataka kutumia watanzania kwa manufaa yao.
Naomba tu wawe wawazi kuhusu mali wanazo miliki. Na sisi watanzania tusipelekwe pelekwe na mtu yeyote tutumie akili zetu na kufikilia.
Mchezo huu unahatarisha maisha si ya wanasiasa bali ya wananchi wasio na hatia.
Nimekua nikifikiria hivi hawa wanasiasa wanapata faida gani wanapozunguka huku na huku majukwaani wakinadi sera zao, hivi kweli ni wazalendo na wanachokiongea ndio hicho? Mwisho wa siku nimeona kuwa sio wazalendo na wala sio watu wanaojinadi kuwa ni wakombozi.
Kunavyama hapa nchini zaidi ya 5 kila mmoja lengo lake ni kutawala nchi. Huku nyuma ya pazia wako na ajenda yao ya siri na kuwahadaa watz kuwa wao ni wakombozi. Wakitumia shida na changamoto za maisha kama kigezo cha wao kupewa nafasi ya utawala.
Mambo ya muhimu ya maendeleo hawayapigii kampeni wanakaa kimya.
Mfano tu mmoja tunazoezi la sensa kitaifa, wanasiasa wamekaa kimya hakuna hata mmoja anaye ongelea hilo. Zaidi tu kueneza propaganda mbalimbali ambazo hazimsaidii mtanzania.
Haya ni maoni yangu kuwa wanasiasa wanataka kutumia watanzania kwa manufaa yao.
Naomba tu wawe wawazi kuhusu mali wanazo miliki. Na sisi watanzania tusipelekwe pelekwe na mtu yeyote tutumie akili zetu na kufikilia.