Wakuu.
Tanzania tumezidiwa na nguvu ya siasa. Siasa kutoka ku-control kila ueledi ni Laana ya ajabu.
Naweza kusema hivyo baada ya sakata la kutoelezeka kwa matumizi ya shilingi trillion 1.5 kama ripoti ya Ukaguzi ya CAG kwa mwaka wa fedha 2016/17.
Katika ukurasa wa 34 wa ripoti ya CAG kwa mwaka wa fedha wa 2016/17 anasema,
"Kati ya Shilingi bilioni 25,307.48 zilizokusanywa, Shilingi bilioni 23,792.30 zilitolewa kwa ajili ya mishahara ya watumishi, matumizi mengine, matumizi ya maendeleo na fedha kwa ajili ya kulipa madeni yatokanayo na amana za Serikali pamoja na riba. Kielelezo cha hapo chini kinaonesha fedha za matumizi katika mwaka wa fedha 2016/17"
Kwa maelezo hayo ni kwamba kuna bakaa “baki” ya shilingi trillion 1.5 ambazo hazijulikani zimetumika wapi.
Katika ukaguzi kuna kitu kinaitwa “Audit Query” ambapo mkaguzi husema upungufu/udhaifu aliouona.
CAG (kama Mkaguzi) si polisi au mahakama kwamba atoe hitimisho kwamba fedha hizi zimeibwa.
Hata sharia ya kazi yake inasema madhaifu yaliyopo ktk ripoti yashughulikiwe na bunge, na hoja ikishindwa kufungwa huko basi inaweza kuamuliwa mahakamani. Kiufupi bunge hutoa maelekezo kwa serikali kwa sababu serikali ndiye mkaguliwa.
Hapa nitaeleza visa 10 vya namna Wakaguzi na Wahasibu walivyowahi kutumika kudanganya ripoti na baadae kuja kusababisha anguko la makampuni au uchumi wan chi kutikiswa.
1. WORLDCOM SCANDAL (2002)
Ni kampuni ya nini?
Mawasiliano
Nini kilitokea?
Kudanganya mtaji (assets) kwa zaidi ya dola billion 11, kulikopelekea wafanyakazi 30,000 kufukuzwa kazi na hasara kwa kampuni kiasi cha dola billion 180.
Wasuka dili/Wahusika wakuu
Mtendaji Mkuu (CEO) Bernie Ebbers
Dili ilisukwaje?
Alishusha matumizi kwa kuongeza mtaji badala ya gharama, na kupandisha mapato kwa mauzo feki.
Namna ilivyogundulika
Idara ya Mkaguzi wa ndani wa WORLDCOM aligundua ubadhirifu wa dola billion 3.8
Hapa ukaguzi zaidi ukaagizwa. Kampuni ilitangazwa Bankruptcy (mufilisi)
Adhabu
Mkuu wa Idara ya Fedha (CFO) alifukuzwa kazi, Mdhibiti (controller) aliachia ngazi, Kampuni ikashindwa kujiendesha na kutangazwa mufilisi.
Mkurugenzi Ebbers alifungwa miaka 25 jela kwa ubadhirifu uhujumu na kuwapa nyaraka bandia wakaguzi.
2. TYCO SCANDAL (2002)
Ni kampuni ya nini?
Kampuni ya Ulaya (iliyokuwa New Jersey) ya mifumo ya ulinzi
Nini kilitokea?
Mkurugenzi Mkuu (CEO) na Mkuu wa Idara ya fedha (CFO) waliiba dola million 150, na kudanganya kwa kuongeza mapato katika vitabu kwa dola million 500.
Wasuka dili/Wahusika wakuu
CEO Dennis Kozlowski na CFO Mstaafu Mark Swartz.
Dili ilisukwaje?
Walijilipa mikopo na marupurupu ya kiutendaji. Pia walijilipa kama wasambazaji wa bidhaa kwa kampuni.
Namna ilivyogundulika
Uchunguzi uliofanywa na Kamisheni ya dhamana ya Dhamana na Mitaji ya Marekani (SEC) iligundua kukiukwa kwa kanuni za kihasibu na mikopo mikubwa kwa Kozlowski.
Adhabu
Kozlowski na Swartz walifungwa miaka 25. Kampuni Tyco iliamriwa kulipa fidia kwa wawekezaji dola biliion 2.92
……………………………………List itaendelea hadi visa vyote kumi (10)……………………..
Hoja
Kwanza, ni uwendawazimu kumshamshulia Mkaguzi (CAG)
Pili, wote mnaona namna ambavyo namba hupikwa ili kuwapa wahusika matumaini hewa. Hapa ndio jukumu la Mkaguzi hutakiwa ili kung’amua ukweli wa hizo namba.
Rais, Mawaziri, Makatibu wakuu, na Wakurugenzi na maafisa wengine wa serikali ni wakaguliwa wa namna walivyotumia mali hizo za wananchi (kodi)
Katika sekta ya umma, CAG ndiye mlinzi/mhakiki wa mali za umma na thamani ya uwekezaji wa umma.
Kunapokuwa na mkanganyiko wowote ktk ukaguzi wa CAG, ni bunge ndio chombo cha kuhoji na sio Mawaziri/Rais ambao hawa ndio wakaguliwa.
Tukija kuendelea na makala hii utakuja kugundua namna ambavyo si afya kiuchumi kuchukia kazi ya Mkaguzi mfano CAG.
Kasomeni historia ya “Auditing” ambayo ilitokana na Principal-Agency business relationship”.
Tanzania tumezidiwa na nguvu ya siasa. Siasa kutoka ku-control kila ueledi ni Laana ya ajabu.
Naweza kusema hivyo baada ya sakata la kutoelezeka kwa matumizi ya shilingi trillion 1.5 kama ripoti ya Ukaguzi ya CAG kwa mwaka wa fedha 2016/17.
Katika ukurasa wa 34 wa ripoti ya CAG kwa mwaka wa fedha wa 2016/17 anasema,
"Kati ya Shilingi bilioni 25,307.48 zilizokusanywa, Shilingi bilioni 23,792.30 zilitolewa kwa ajili ya mishahara ya watumishi, matumizi mengine, matumizi ya maendeleo na fedha kwa ajili ya kulipa madeni yatokanayo na amana za Serikali pamoja na riba. Kielelezo cha hapo chini kinaonesha fedha za matumizi katika mwaka wa fedha 2016/17"
Kwa maelezo hayo ni kwamba kuna bakaa “baki” ya shilingi trillion 1.5 ambazo hazijulikani zimetumika wapi.
Katika ukaguzi kuna kitu kinaitwa “Audit Query” ambapo mkaguzi husema upungufu/udhaifu aliouona.
CAG (kama Mkaguzi) si polisi au mahakama kwamba atoe hitimisho kwamba fedha hizi zimeibwa.
Hata sharia ya kazi yake inasema madhaifu yaliyopo ktk ripoti yashughulikiwe na bunge, na hoja ikishindwa kufungwa huko basi inaweza kuamuliwa mahakamani. Kiufupi bunge hutoa maelekezo kwa serikali kwa sababu serikali ndiye mkaguliwa.
Hapa nitaeleza visa 10 vya namna Wakaguzi na Wahasibu walivyowahi kutumika kudanganya ripoti na baadae kuja kusababisha anguko la makampuni au uchumi wan chi kutikiswa.
1. WORLDCOM SCANDAL (2002)
Ni kampuni ya nini?
Mawasiliano
Nini kilitokea?
Kudanganya mtaji (assets) kwa zaidi ya dola billion 11, kulikopelekea wafanyakazi 30,000 kufukuzwa kazi na hasara kwa kampuni kiasi cha dola billion 180.
Wasuka dili/Wahusika wakuu
Mtendaji Mkuu (CEO) Bernie Ebbers
Dili ilisukwaje?
Alishusha matumizi kwa kuongeza mtaji badala ya gharama, na kupandisha mapato kwa mauzo feki.
Namna ilivyogundulika
Idara ya Mkaguzi wa ndani wa WORLDCOM aligundua ubadhirifu wa dola billion 3.8
Hapa ukaguzi zaidi ukaagizwa. Kampuni ilitangazwa Bankruptcy (mufilisi)
Adhabu
Mkuu wa Idara ya Fedha (CFO) alifukuzwa kazi, Mdhibiti (controller) aliachia ngazi, Kampuni ikashindwa kujiendesha na kutangazwa mufilisi.
Mkurugenzi Ebbers alifungwa miaka 25 jela kwa ubadhirifu uhujumu na kuwapa nyaraka bandia wakaguzi.
2. TYCO SCANDAL (2002)
Ni kampuni ya nini?
Kampuni ya Ulaya (iliyokuwa New Jersey) ya mifumo ya ulinzi
Nini kilitokea?
Mkurugenzi Mkuu (CEO) na Mkuu wa Idara ya fedha (CFO) waliiba dola million 150, na kudanganya kwa kuongeza mapato katika vitabu kwa dola million 500.
Wasuka dili/Wahusika wakuu
CEO Dennis Kozlowski na CFO Mstaafu Mark Swartz.
Dili ilisukwaje?
Walijilipa mikopo na marupurupu ya kiutendaji. Pia walijilipa kama wasambazaji wa bidhaa kwa kampuni.
Namna ilivyogundulika
Uchunguzi uliofanywa na Kamisheni ya dhamana ya Dhamana na Mitaji ya Marekani (SEC) iligundua kukiukwa kwa kanuni za kihasibu na mikopo mikubwa kwa Kozlowski.
Adhabu
Kozlowski na Swartz walifungwa miaka 25. Kampuni Tyco iliamriwa kulipa fidia kwa wawekezaji dola biliion 2.92
……………………………………List itaendelea hadi visa vyote kumi (10)……………………..
Hoja
Kwanza, ni uwendawazimu kumshamshulia Mkaguzi (CAG)
Pili, wote mnaona namna ambavyo namba hupikwa ili kuwapa wahusika matumaini hewa. Hapa ndio jukumu la Mkaguzi hutakiwa ili kung’amua ukweli wa hizo namba.
Rais, Mawaziri, Makatibu wakuu, na Wakurugenzi na maafisa wengine wa serikali ni wakaguliwa wa namna walivyotumia mali hizo za wananchi (kodi)
Katika sekta ya umma, CAG ndiye mlinzi/mhakiki wa mali za umma na thamani ya uwekezaji wa umma.
Kunapokuwa na mkanganyiko wowote ktk ukaguzi wa CAG, ni bunge ndio chombo cha kuhoji na sio Mawaziri/Rais ambao hawa ndio wakaguliwa.
Tukija kuendelea na makala hii utakuja kugundua namna ambavyo si afya kiuchumi kuchukia kazi ya Mkaguzi mfano CAG.
Kasomeni historia ya “Auditing” ambayo ilitokana na Principal-Agency business relationship”.