wanaovunja viti uwanja mpya .......

Ni watanzania ,ujinga ndio unawasambua.Kama sio watanzania sasa inamaana uwanja mzima unakuwa umejaa wageni? kama kuna mtanzania anaona mtu anavunja kiti kwanini wasimpeleke kwenye vyombo husika?
 
yeah umeangalia tbc ukadhani hivyo...... au malizia kabisa kama ni watanzania wanaweza wakawa wana CDM.... LOL

On a serious note, we need to condemn anyone anayeharibu mali ya taifa si uwanja wa taifa pekee... patriotism si kubeba bendera pekee bali ni pamoja na kulinda mali za nchi, watu wa nchi na amani ya nchi hii... ambayo, kwa bahati mbaya, we are not good at

TUAMKE SASA, TULINDE NCHI YETU, MALI ZETU NA AMANI YETU

ANAYEVUNJA AKAMATWE NA ALIPISHWE GHARAMA YA UHARIBIFU
 
Ni watanzania ,ujinga ndio unawasambua.Kama sio watanzania sasa inamaana uwanja mzima unakuwa umejaa wageni? kama kuna mtanzania anaona mtu anavunja kiti kwanini wasimpeleke kwenye vyombo husika?
ATAKUA ANATANIA MKUU... we account for over 90% ya attendance there:redfaces:
 
nina wasiwasi wanaovunja viti uwanja mpya wa taifa si watanzania
uzuri wa hii sredi yako ni fupi na haichokeshi kusoma. ubaya wake ni kwamba haina mantiki wala ushahidi. weka ushahidi kabla hatujakuvua uanachama wa greti thinka.
 
uzuri wa hii sredi yako ni fupi na haichokeshi kusoma. ubaya wake ni kwamba haina mantiki wala ushahidi. weka ushahidi kabla hatujakuvua uanachama wa greti thinka.
thanks mkuu

naona kaangalia tbc kakurupuka ili awe wa kwanza kuposti suala la vindalism ya viti na mali za uwanja wa taifa
 
someni kabla ya kuanza kushambulia ndiyo maana nimetanguliza neno 'wasiwasi ' kwa sababu kwa mtanzania kufanya vitendo kama hivyo atakuwa punguani ni sawa na mtu kuharibu mali yake aliyoitafuta kwa muda mrefu kwani ni ukweli usiopingika kuwa uwanja ule ni mali ya watz wote sasa wao kuharibu mali zao ni kukosa mzalendo makusudi au bahati mbaya?
 
someni kabla ya kuanza kushambulia ndiyo maana nimetanguliza neno 'wasiwasi ' kwa sababu kwa mtanzania kufanya vitendo kama hivyo atakuwa punguani ni sawa na mtu kuharibu mali yake aliyoitafuta kwa muda mrefu kwani ni ukweli usiopingika kuwa uwanja ule ni mali ya watz wote sasa wao kuharibu mali zao ni kukosa mzalendo makusudi au bahati mbaya?
kwanza labda nikuulize wewe ni mtanzania?, maana hizi tabia ulizoandika kwenye hii post ndio tabia za watanzania hasaaaa! sasa sjui kwanini unawanyang'anya watanzania tabia zao. nazani ulitakiwa kutuambia watanzania tujirekebishe na sio kuzichakachua tabia zetu.
 
Mambo ya kuingia uwanjani bule hayo. Waliovunja inawezekana hata TV hawaangalii, Mitandao kama hii ndio hawajui kama ipo, Labda kesho watachungulia vichwa vya habari vya magazeti, Ila ni vile vya mbele, habari za michezo hawazioni. Wanasubilia tena next time itokee bure wakavuje tena, maana hawajui utaratibu.
 
mi Mtanganyika labda ndiyo maana nawaona nyie mko tofauti
hehehe punguza hasira greti thinka, hasira zinaweza kupelekea ugonjwa wa dayabetic. acha nikubaliane na wewe basi ili tusuluhishe,

nadhani itakuwa wa ivori kosti ndio wanaovunja viti vya uwanja mpya, wabongo hawawezi kabisa kufanya hivi bana.
 
someni kabla ya kuanza kushambulia ndiyo maana nimetanguliza neno 'wasiwasi ' kwa sababu kwa mtanzania kufanya vitendo kama hivyo atakuwa punguani ni sawa na mtu kuharibu mali yake aliyoitafuta kwa muda mrefu kwani ni ukweli usiopingika kuwa uwanja ule ni mali ya watz wote sasa wao kuharibu mali zao ni kukosa mzalendo makusudi au bahati mbaya?
mkuu, nimekusoma sana na nikarudia na nikauona huo "wasiwasi" WAKO... na dnio maana kwenye post yangu namba tatu nikaendeleza wasiwasi wako kwa kutoa rai kwamba tulinde vilivyo vyetu

labda ungetumia dk chache pia walichoandika wenzako usirejea na kulalama
 
Mambo ya kuingia uwanjani bule hayo. Waliovunja inawezekana hata TV hawaangalii, Mitandao kama hii ndio hawajui kama ipo, Labda kesho watachungulia vichwa vya habari vya magazeti, Ila ni vile vya mbele, habari za michezo hawazioni. Wanasubilia tena next time itokee bure wakavuje tena, maana hawajui utaratibu.
Wakati akiwa amesimama juu ya kiti jirani yake anakosekana hata wa kumwambia siyo mambo hayo shuka mpk kinang'oka?
 
Naomba kwa heshima tu niwaulize wachangiaji wenzangu mmeshawahi kwenda uwanja wa taifa na kuvikalia vile viti?, nauliza kwa nia nzuri tu ili nitoe mawazo yangu. Mawazo yangu vile viti haviendani na Quality ya ule uwanja, kila kitu katika ule uwanja ni superb isipokuwa vile viti. Kwanza ni rahisi kuvunjika pili vipo karibu hivyo wakati wa kutoka ndipo inapokuwa taabu, kama mstari uliopo mtu akizembea mbele utaona watu wanataka kurukia mstari mwingine na huwezi fanya hivyo isipokuwa ukanyage kiti, ndipo kinavunjika. Nafikiri itafutwe mbinu ya kuvibadili la sivyo wimbo utakuwa huo huo kila siku, viwekwe aidha vigumu kama vilivyokuwa kweney mabasi ya uda ya zamani au viwekwe vya kujikunja kama katika majumba ya cinema. Ili mtu akinyanyuka tu kinajikunja hivyo hataweza kukikanyaga na hakitaweza kuvunjika, bila hivyo tutatafuta mchawi kila siku.
 
Mambo ya kuingia uwanjani bule hayo.
Kuna wale waliolipia mechi za mwanzoni uwanja ulivyofunguliwa rasmi,wao walipanga foleni kabisa chooni wanakojoa kwenye ma-sink ya kuoshea mikono.

Ustaarabu hauna maskini wala tajiri hawa wote ni wakupewa adhabu tu.
 
Viti vinavyunjwa kwa ujinga na ushabiki wa kipuuzi kabisa uwanjani. Kwa mfano, mtu anaingia uwanjani kachelewa kidogo. Ile kukaa tu, rafiki yake anampigia mbinja, "mshkaji eeh njoo tukae hapa kuna nafasi". May be jamaa yupo juu kidogo mathalani row ya tano hivi.
Basi hilo njemba badala ya kumfuata mwenzake kwa kutoka kwenye hiyo row ili aende kwenye ngazi hadi afike kwenye row ya tano alipo rafiki yake, utakuta linakanyaga viti hadi mahali hapo. Na hii tabia ipo sana. Kiti/viti kinaweza kisivunjike hapo, lakini tayari kinaanza kupata damage taratibu. Tujifunze ustaarabu jamani. Napia wale wengine tukemee tabia kama hii.
 
hehehe punguza hasira greti thinka, hasira zinaweza kupelekea ugonjwa wa dayabetic. acha nikubaliane na wewe basi ili tusuluhishe,

nadhani itakuwa wa ivori kosti ndio wanaovunja viti vya uwanja mpya, wabongo hawawezi kabisa kufanya hivi bana.
Nakasirika si unajua kodi nalipa halafu wengine wanacheza na fedha zetu , mambo kama haya ndiyo huwa fursa mafisadi kubuni mbinu za kutuibia sasa hv itatangazwa tenda ya waangalizi wa samani uwanjani wakati wa mechi ikiendelea msigune sasa mnategemea uharibifu uendelee mpk lini?
 
Ni ulimbukeni wa sisi waTZ! Kwenye fainali ya Tusker Cup,kuna dogo mmoja alikamatwa anakojoa kwny sinki la kunawia mikono! Sasa mtu wa namna hii kung'oa kiti si anaona kawaida tu! Eti anaikomoa TFF na serikali. Haelewi kama anajikomoa yeye,kwani pesa yake (kwa njia ya kodi) ndio itakayotumika kurekebisha uharibifu uliojitokeza!
 
Wengine wanajisikia vizuri wakivunja na kuchukua vipisi kama kumbu kumbu majumbani??????
 
Back
Top Bottom