Hehehe, mkuu hiyo ni ajira ya mtu, app moja inaweza chukua muda mrefu sana, hadi miezi kadhaa, unataka mtu akufanyie bei gani? laki moja mbili?
Wanaotengeneza website kama blog ile sio complex skill wanatumia templates tu kitendo cha kubadilisha data, au wordpress na yenyewe vilevile tu. Ukitaka custom website na complex features hakuna mtu nayemjua wa kufanya chini ya Tshs.2Million.
Apps in most cases lazima uanze from scratch, kuandika code sio kitu rahisi kama watu wengi wanavyofikiria, hauendi tu na kuiambia computer app iko hivi na yenyewe ikafanya, kuna mambo mengi sana ya kujifunza, ni skill ambayo imetuchukua wengine miaka kuimaster.
App ya bei chini kabisa nilowahi fanya ni 500K na hiyo ilinichukua kama masaa manne kuikamilisha. Ila kawaida siendi chini ya 2M kwa simple apps na 10M+ kwa complex applications, miaka niliyopoteza kusoma inabidi ijilipe, mwisho wa siku app itakutengenezea wewe mamilioni kwa nini niifanye kwa laki moja mbili au less? hehehe! Wapo lakini developer uchwara wanaweza kukufanyia hata kwa 50K lakini jiandae kupata quality sawa na bei hiyo.
Em angalia hii picha ujifunze kitu
View attachment 517300