Wanaosema Gwajima hana msaada jimboni wanakaa wapi?

Nov 21, 2023
10
24
Siku ya Jumamosi ya tarehe 21 iliandikwa historia ya kunyesha mvua isiyo ya kawaida iliyosababisha maafa makubwa sana. Pamoja na maeneo mengine, jimbo la Kawe liliguswa vibaya sana na mvua hizi.

Madaraja mengi yalikatika, nyumba ziliondoka na kukabaki misingi tu. Magari na samani nyingi zilisombwa na maji. Tangu siku ile jana mbunge Gwajima amekuwa bega kwa bega na watu wake kuhakikisha anakuwa nao huku akipambana kurudisha tumaini tena kwenye maisha yao.

Gwajima ameonekana sana kwenye site za madaraja na barabara huku greda alilonunua likipambana na tope usiku na mchana kusaidia wananchi. Madaraja mengi yamerudishwa katika hali yake na mawasiliano ya barabara yamerudi kuimarika vyema.

Kama vyombo vya habari havioni jambo hili sisi wananchi tutatumia midomo yetu kumwambia mbunge asante kwa moyo wako wa ukarimu. Jitihada zako tangu ulipoamua kugombea mpaka leo zinaonekana.

Mtu akija jimboni na aweke akili yake sawasawa. Ukituletea masentensi ya ovyo eti mbunge hajatusaidia tutakufundisha hii ndio Kawe ya Gwajima. Mitaro ya Mbweni, mitaro ya Msasani, vivuko na barabara alizotengeneza unaweza kudhani Gwajima wako 1000 kumbe jamaa ni mmoko lakini shughuli ni ya kubafu aroooo.
 
Unaandika kutoka Birmingham Alabama au uko hapa hapa Kawe mkuu?

WanaKawe, kuna mtu huku anawabipu njooni!😁😁 😁


IMG_20240116_170605_391.jpg
IMG_20240116_170605_310.jpg
IMG_20240116_170604_835.jpg
 
Kweli tena
Kweli tena weka number ya simu hapo .....utakumbukwa kwenye usanii na kutengeneza comedy
Gwajima ni msanii tu!! Hilo greda lake halitatatua matatizo ya barabara za jimbo la Kawe haşa zile za kule Tegeta kwasababu greda linakwangua na mvua zikinyesha barabara inakuwa tope haipitiki!!

Kuna barabara moja hapo Nyaishozi kwenda Nyamachabezi hiyo barabara inatakiwa itengenezewe drainage system lakini wao wanatifua tifua na kuziba madimbwi lakini mvua zikinyesha hali inarudi vile vile miaka yote!! Viongozi wamekosa maarifa!
 
Siku ya Jumamosi ya tarehe 21 iliandikwa historia ya kunyesha mvua isiyo ya kawaida iliyosababisha maafa makubwa sana. Pamoja na maeneo mengine, jimbo la Kawe liliguswa vibaya sana na mvua hizi.
o na barabara alizotengeneza unaweza kudhani Gwajima wako 1000 kumbe jamaa ni mmoko lakini shughuli ni ya kubafu aroooo.
Hapo Japan unaendeleaje na mafunzo ya uvuvi mkuu?
 
Jimbo la kawe bado tuna matumaini ma Gwajima, kwa muda mfupi wa miaka yake 4 shoo yake si ya kitoto. Maana tulikuwa na miaka 15 ya kupotezewa muda na hayo yote ambayo Gwajima amepambana na kutoboa ni matobo na udhaifu wa aliyekuweko.

Gwajima akipewa miaka mingine buku kawe yote inabadirika.

Mpe muda amalizie madhaifu ya miaka 15 mizima, ili kazi yake jimbo la kawe ianze.

Sisi tupo kawe na kazi inaendelea

Gwajiboy anatosha!
 
Siku ya Jumamosi ya tarehe 21 iliandikwa historia ya kunyesha mvua isiyo ya kawaida iliyosababisha maafa makubwa sana. Pamoja na maeneo mengine, jimbo la Kawe liliguswa vibaya sana na mvua hizi.

Madaraja mengi yalikatika, nyumba ziliondoka na kukabaki misingi tu. Magari na samani nyingi zilisombwa na maji. Tangu siku ile jana mbunge Gwajima amekuwa bega kwa bega na watu wake kuhakikisha anakuwa nao huku akipambana kurudisha tumaini tena kwenye maisha yao.

Gwajima ameonekana sana kwenye site za madaraja na barabara huku greda alilonunua likipambana na tope usiku na mchana kusaidia wananchi. Madaraja mengi yameirudishwa katika hali yake na mawasiliano ya barabara yamerudi kuimarika vyema.

Kama vyombo vya habari havioni jambo hili sisi wananchi tutatumia midomo yetu kumwambia mbunge asante kwa moyo wako wa ukarimu. Jitihada zako tangu ulipoamua kugombea mpaka leo zinaonekana.

Mtu akija jimboni na aweke akili yake sawasawa. Ukituletea masentensi ya ovyo eti mbunge hajatusaidia tutakufundisha hii ndio Kawe ya Gwajima. Mitaro ya Mbweni, mitaro ya Msasani, vivuko na barabara alizotengeneza unaweza kudhani Gwajima wako 1000 kumbe jamaa ni mmoko lakini shughuli ni ya kubafu aroooo.
Muongo wewe, sijui unazungumzia jumamose ipi ya tarehe 21, pengine mwaka jana. 2023.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom