Wanaopinga uwepo wa Mungu ni wakaidi

Wanaopinga uwepo wa Mungu ni wakaidi

Hauwezi kumjua mungu bila DINI.
Ndo maana kulikuwa na mitume na manabii waliotumwa kuleta neno la kumjua mungu.
Ndo maana kuna watu waliowapinga hao mitume na manabii waliadhibiwa kwa adhabu Kali ya Mungu
Ambao wote wametokea mashariki ya kati? (Mungu amekua mbinafsi kiasi hiko)
Ambapo biashara ya utumwa imesaidi 95% kuenea kwa dini!!! (Hili jambo kweli Mungu ameliona ni busara?)


Wanaopinga Mungu hayupo wana hoja na mnazishindwa hoja zao
 
Neno mungu umelitumia kwenye mkitadha gani?

Kumbuka kuna maneno kama haya

1.mungu
2. Mungu
3. MUNGU

TAFADHALI NIJULISHE MAANA UJUMBE WAKO NI MZURI SANA
Niambie tofauti ya hayo meneno matatu, halafu nitakwambia muktadha niliotumia katika hiyo.
 
Kuna vitu ukifikiria hupati majibu kabisa mfano kumu judge Mungu
Lakini kwa akili ya kawaida tu utabaini kuwa hii sio hoja ya kuthibitisha kuwa mungu hayupo.

Na hata katika Quran kumetajwa miungu mingine, hata firauni alijiita mungu na kuna huyu mama naye aliyeibuka hivi karibuni hapa kwetu naye nasikia anajiita mungu.

Hivyo uwepo wa miungu mingi haulazimu kutokupo kwa mungu wa kweli.
 
Sio Quran tu, vitabu vingi vimeeleza uwepo wa wapinga Mungu lakini bado huvikubali kuwa ni vitabu vya kweli

Nini kinachofanya kitabu chako kiwe special kuliko vingine?

Kuthibitisha Mungu yupo ndio kwamba umeshindwa kabisa?
Utoafauti wa Quran na vitabu vingine upo wazi, au uspecial gani hasa unaoutaka?

Kuhusu kuthibitisha kuwa mungu yupo, sidhani kama unahitajia hilo, maana ulishapinga.

Au umebadili msimamo?
 
Utoafauti wa Quran na vitabu vingine upo wazi, au uspecial gani hasa unaoutaka?

Kuhusu kuthibitisha kuwa mungu yupo, sidhani kama unahitajia hilo, maana ulishapinga.

Au umebadili msimamo?
Kwanini kitabu chako kiwe cha kweli kuliko vingine?

Hakuna sehemu umethibitisha zaidi ya assumption kitu ambacho kinaweza fanywa na muumini wa dini nyingine ambayo inapingana na ukapinga aina hiyo ya ushahidi
 
Kwanini kitabu chako kiwe cha kweli kuliko vingine?

Hakuna sehemu umethibitisha zaidi ya assumption kitu ambacho kinaweza fanywa na muumini wa dini nyingine ambayo inapingana na ukapinga aina hiyo ya ushahidi
Kwani wewe ulianza kupinga Quran kabla ya kuijua na kujua yaliyomo ndani yake?

Kama ulifanya hivyo huoni kama huo ni ujinga?

Na kama unayajua yaliyomo na umeshayapinga, hivyo jibu langu litabadilisha nini?

au unataka mjadala usio na tija?
 
Kwani wewe ulianza kupinga Quran kabla ya kuijua na kujua yaliyomo ndani yake?

Kama ulifanya hivyo huoni kama huo ni ujinga?

Na kama unayajua yaliyomo na umeshayapinga, hivyo jibu langu litabadilisha nini?

au unataka mjadala usio na tija?
Kuna maelfu ya dini ambazo zinapingana na dini yako ambazo unaziita dini za uwongo, unataka kuniambia ulipata wasaa wa kusoma vitabu vyao halafu ndipo ukapinga kuwa ni dini za uongo?
 
Kuna Miungu ipatayo zaidi ya 5,000 inayoabudiwa hapa duniani

Wasioamini Mungu hawakubaliani na hiyo Miungu yote

Ila wewe unakubaliana na Mungu mmoja na kupinga Miungu 4,999

For the same reason umekuwa mkaidi kwa hiyo miungu na huwezi kuthibitisho hiyo miungu uliyoipinga kuwa haipo

Umesema wasioamini Mungu wanapinga mafundisho ya dini, well kauli hii itakuwa valid pale muislamu atapotuambia ni kiasi gani anakubalina na habari za roho mtakatifu, Mungu katika utatu, Yesu kuwa ndio njia ya pekee na uzima, Yesu kubatizwa nk. ambazo zimeelezwa kwenye dini ya kikristo

Kama nyinyi kwa nyinyi mnaoamini Mungu mnapinga mafundisho ya dini zingine, kwanini jambo hilo hilo likifanywa na mtu asiyeamini Mungu lichukuliwe katika uzito mkubwa?

Nimeona umenukuu aya za Quran hapo kua ndio uthibitisho wa kile ulichokiita muujiza, lakini kuna madai mangapi ya kimuujiza kwenye biblia unayapinga?

Kwanini uyapinge wakati yameitwa ni miujiza? So kumbe kitu kuitwa miujiza sio kigezo cha kyafanya yawe kweli au kukubaika, kwa fact hiyo kumbe hata wewe inawezekana hayo madai yako yakawa ya kizushi vile vile otherwise uje na vivid evidence inayopimika
The real meaning of the philosophy
 
Wanaokana mungu huwa wanahoja mbalimbali katika kupinga uwepo wa mungu, pia huwa wanakosoa mafunzo ya dini ili kutilia mkazo zaidi katika hilo.

Lakini ukweli ni kwamba, sio kama hoja zao zinathibitisha kutokuwepo kwa mungu, hapana.
Bali hoja zao zinathibitisha kuwa wao ni wapingaji, hivyo hakuna andiko wala muujiza utakao wafanya waamini, sembuse hizi hoja ambazo huwa wanarumbana na watu Kila kukicha.

Na hivi ndivyo walivyo tangu enzi na enzi, hoja zao ni zilezile, na hata katika Quran, imeelezwa jinsi hawa watu walivyowakaidi.

Walipoonyeshwa miujiza waliita uchawi, maneno ya Mwenyezi Mungu waliyaita hadhithi za kutunga, mitume waliwaita wachawi, machizi n.k.(rejea; Quran 6:7,10:2,15:6, 46:17, 44:14, 40:56).

Na katika kudhihirisha zaidi ukaidi wao, walifikia hadi kusema kumwambia Mwenyezi Mungu, eti kama kweli hii (yaani yale aliyokujanayo mtume) ni haki kutoka kwako basi tuteremshie mawe kutoka mbinguni, au ututeremshie adhabu yenye kuumiza.(rejea; Quran 8:32).

Hii inaonyesha ni kiasi gani hawa watu ni wakaidi maana wangetaka kujua, wangeomba kuongozwa ila kwakuwa ni wakaidi wakaomba kuangamizwa.

Atakwambia thibitisha kama mungu yupo.

Sasa kama dalili alizoziweka mungu mwenyewe kuthibitisha uwepo wake hazijakukinaisha kuamini, unadhani hoja gani itakayokukinaisha.

Muktadha wa kupinga kwao ni kwamba mungu hayupo, hivyo hoja za kuthibitisha uwepo wake zote ni batili, lakini hata kama mungu yupo na hizi ndizo dalili alizoziweka kuthibitisha uwepo wake, basi ndio tayari wameshazipinga, maana hawakubalianinazo, hivyo ni wapingaji.

Kwahiyo tatizo sio ubora wa dawa ya sikio katika kutibu, bali tatizo ni kuwa hili ni sikio la kufa, hivyo halisikii dawa.
Dini ukiipeleka kwenye falsafa na sayansi inabaki uchi Sana. Usishangae ukachakazwa na wanafalsafa mzee
 
Sasa Kama Mungu alijua kutakua nawakana mungu, Sasa hao wakana Mungu wanakosa gani?
Na katika kudhihirisha zaidi ukaidi wao, walifikia hadi kusema kumwambia Mwenyezi Mungu, eti kama kweli hii (yaani yale aliyokujanayo mtume) ni haki kutoka kwako basi tuteremshie mawe kutoka mbinguni, au ututeremshie adhabu yenye kuumiza.(rejea; Quran 8:32).

Hii inaonyesha ni kiasi gani hawa watu ni wakaidi maana wangetaka kujua, wangeomba kuongozwa ila kwakuwa ni wakaidi wakaomba kuangamizwa.

Mwenyezimungu hamdhulumu yeyote.
 
Kuna maelfu ya dini ambazo zinapingana na dini yako ambazo unaziita dini za uwongo, unataka kuniambia ulipata wasaa wa kusoma vitabu vyao halafu ndipo ukapinga kuwa ni dini za uongo?
Certainly, Allah’s only Way is Islam.1 Those who were given the Scripture did not dispute ˹among themselves˺ out of mutual envy until knowledge came to them.2 Whoever denies Allah’s signs, then surely Allah is swift in reckoning.(3:19)
 
Wapingaji wa uwepo wa Mungu hawakuanza leo na watazidi kuendelea kuwepo...!!

Wapingaji wa Mungu walikuwepo kipindi cha Mussa!! Na ndio waliomwambia Mussa kuwa ili tukuamini basi mwambie Mungu wako ajitokeze tumuone live...Mussa aliwachukua na kupanda nao mlimani na huko walipigwa na radi nzito kutoka kwa Mungu na wote wakafariki kutokana na ukaidi wao ila Mussa alimuomba Mungu awafufue...walivyofufuliwa ndio wakaamini kuwa kweli Mungu yupo
 
Back
Top Bottom