Msonjo
JF-Expert Member
- Oct 13, 2019
- 1,378
- 2,394
Wanaokana mungu huwa wanahoja mbalimbali katika kupinga uwepo wa mungu, pia huwa wanakosoa mafunzo ya dini ili kutilia mkazo zaidi katika hilo.
Lakini ukweli ni kwamba, sio kama hoja zao zinathibitisha kutokuwepo kwa mungu, hapana.
Bali hoja zao zinathibitisha kuwa wao ni wapingaji, hivyo hakuna andiko wala muujiza utakao wafanya waamini, sembuse hizi hoja ambazo huwa wanarumbana na watu Kila kukicha.
Na hivi ndivyo walivyo tangu enzi na enzi, hoja zao ni zilezile, na hata katika Quran, imeelezwa jinsi hawa watu walivyowakaidi.
Walipoonyeshwa miujiza waliita uchawi, maneno ya mwenyezimungu waliyaita hadhithi za kutunga, mitume waliwaita wachawi, machizi n.k.
(rejea; Quran 6:7,10:2,15:6, 46:17, 44:14, 40:56...)
Na katika kudhihirisha zaidi ukaidi wao, walifikia hadi kusema kumwambia mwenyezimungu, eti kama kweli hii (yaani yale aliyokujanayo mtume) ni haki kutoka kwako basi tuteremshie mawe kutoka mbinguni, au ututeremshie adhabu yenye kuumiza.(rejea; Quran 8:32)
Hii inaonyesha ni kiasi gani hawa watu ni wakaidi maana wangetaka kujua, wangeomba kuongozwa ila kwakuwa ni wakaidi wakaomba kuangamizwa.
Atakwambia thibitisha kama mungu yupo.
Sasa kama dalili alizoziweka mungu mwenyewe kuthibitisha uwepo wake hazijakukinaisha kuamini, unadhani hoja gani itakayokukinaisha.
Muktadha wa kupinga kwao ni kwamba mungu hayupo, hivyo hoja za kuthibitisha uwepo wake zote ni batili, lakini hata kama mungu yupo na hizi ndizo dalili alizoziweka kuthibitisha uwepo wake, basi ndio tayari wameshazipinga, maana hawakubalianinazo, hivyo ni wapingaji.
Kwahiyo tatizo sio ubora wa dawa ya sikio katika kutibu, bali tatizo ni kuwa hili ni sikio la kufa, hivyo halisikii dawa.
Lakini ukweli ni kwamba, sio kama hoja zao zinathibitisha kutokuwepo kwa mungu, hapana.
Bali hoja zao zinathibitisha kuwa wao ni wapingaji, hivyo hakuna andiko wala muujiza utakao wafanya waamini, sembuse hizi hoja ambazo huwa wanarumbana na watu Kila kukicha.
Na hivi ndivyo walivyo tangu enzi na enzi, hoja zao ni zilezile, na hata katika Quran, imeelezwa jinsi hawa watu walivyowakaidi.
Walipoonyeshwa miujiza waliita uchawi, maneno ya mwenyezimungu waliyaita hadhithi za kutunga, mitume waliwaita wachawi, machizi n.k.
(rejea; Quran 6:7,10:2,15:6, 46:17, 44:14, 40:56...)
Na katika kudhihirisha zaidi ukaidi wao, walifikia hadi kusema kumwambia mwenyezimungu, eti kama kweli hii (yaani yale aliyokujanayo mtume) ni haki kutoka kwako basi tuteremshie mawe kutoka mbinguni, au ututeremshie adhabu yenye kuumiza.(rejea; Quran 8:32)
Hii inaonyesha ni kiasi gani hawa watu ni wakaidi maana wangetaka kujua, wangeomba kuongozwa ila kwakuwa ni wakaidi wakaomba kuangamizwa.
Atakwambia thibitisha kama mungu yupo.
Sasa kama dalili alizoziweka mungu mwenyewe kuthibitisha uwepo wake hazijakukinaisha kuamini, unadhani hoja gani itakayokukinaisha.
Muktadha wa kupinga kwao ni kwamba mungu hayupo, hivyo hoja za kuthibitisha uwepo wake zote ni batili, lakini hata kama mungu yupo na hizi ndizo dalili alizoziweka kuthibitisha uwepo wake, basi ndio tayari wameshazipinga, maana hawakubalianinazo, hivyo ni wapingaji.
Kwahiyo tatizo sio ubora wa dawa ya sikio katika kutibu, bali tatizo ni kuwa hili ni sikio la kufa, hivyo halisikii dawa.