Wanaopinga uwepo wa Mungu ni Wakaidi (3)

Wanaopinga uwepo wa Mungu ni Wakaidi (3)

Msonjo

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2019
Posts
1,378
Reaction score
2,394
Leo natoa na salamu.

Kutokea pale nilipoishia.

Kwa mwenyeakili atagundua kuwa huu ulimwengu na vyote vilivyomo, havikujiumba vyenyewe bali kuna alieviumba ndio maana vipo katika mpangilio uliopangika sawa sawa.

Swali nani aliyeuumba na akauweka katika mpangilio huu?

Aliyeumba ulimwengu na kutuumba sisi wanaadamu hakutuacha hivihivi, bali alituma wajumbe(mitume) ambao ndio waliokuja na habari za uwepo wake na kuwa yeye ndiye aliyeuumba huu ulimwengu na vyote vilivyomo.

Hivyo uwepo wa huu ulimwengu na vilivyomo, na mpangilio wake, na uwepo wetu sisi wanaadamu na kukili kwetu kuwa hatujajiumbwa wenyewe, wala kuumba huu ulimwengu, basi hizi zikawa ni ishara za uwepo wa mwenyezimungu kwa wale wenyeakili.

Lakini mitume walikuwa ni wanaadamu na walikuwa wakifahamika na watu wao na pia hawakudai tu kuwa wao ni mitume wa mwenyezimungu, bali walithibitisha utume wao kwa kuonyesha miujiza -mambo ambayo sio ya kawaida-, na pia walikujanayo(vitabu) yalikuwa yanasadikisha wanayoyasema.

Na hii inaafikiana na sababu za kumuamini mtu.

Unaweza kumuamini mtu kwa sababu unamjua vizuri, hivyo unajua hawezi kudanganya katika anayoyasema au utamuamini baada ya kuthibitishia(ushahidi) au baada ya kuyasadikisha yale anayoyasema.

Maana unaweza usimuamini msemaji, na wala usiamini ushahidi alioutoa, lakini baada ya kuyasikia aliyoyasema ukayaona ni yakweli, hivyo ukamsadikisha.

Tukiacha khabari za mitume kwa ujumla wao, katika umma huu, tuna mtume Muhammad -swallallahu allaihi wasallam-, kuna mtu atasema hamjui!!!?

Kwa hakika katika binadamu ambaye historia ya maisha yake ipo exposed ni mtume Muhammad -swallallahu allaihi wasallam-, kuanzia anazaliwa, alivyoishi, kufa kwake, maneno aliyokuwa anayasema, mpaka alivyokuwa akikutana na wakeze, mpaka jinsi alivyokuwa akipiga mswaki!!!
huu ni uwazi ulioje?

Na huu ni mlango ambao upo wazi kwa kila mmoja, huyu ndiye mtume wa mwenyezimungu, na maisha yake yapo wazi, maneno yake yapo wazi(hadiith) na ujumbe aliokuja nao kutoka kwa Allah upo baina ya mikono yetu(Quran).

Lakini wanaompinga huwa hawaoni kuwa kunamazingatio kwenye historia ya maisha yake, kuwa imekamilika, bali wao wanatafuta sehemu wanazoweza kukosoa ili waendelee kupotosha watu na kueneza chuki.

Hivyo asiyemuamini na akampinga basi anampinga kwa kujua, maana anamjua na anayajua aliyokujanayo(Quran).
Vinginevyo atakuwa anampinga kwa ujinga(na huu ni ujinga ulioje)!!!?

Lakini hata kama mtu atawaamini mitume, ni wazi atakuwa na maswali, atajiuliza kwanini mwenyezimungu alituumba? kwanini maisha yapo hivi? mungu yupo wapi? mbona aliweka mfumo huu, na hakujidhihirisha? na maswali kibao kuhusu mwenyezimungu.

Lakini kwa akili ya kawaida tu, utagundua kuwa majibu sahihi ya hayo maswali, yatatoka kwa mtume ambaye yeye ndiye aliyekuja na habari za Mungu, na kwa aliyemuamini ni wajibu kuyaamini, maana ni katika muktadha wa kumuani kwake.

Hivyo muumini atauliza maswali yenye tija,lakini asiyemuamini atauliza maswali ya hovyo, na mbaya zaidi atajijibu mwenyewe, ili kujustify kutokuamini kwake.

Sasa wakana mungu wanajifanya hawana Imani, kisha wamempinga mtume(Muhammad swallallahu allaihi wasallam), na wameipinga Quran, kisha wakasema mungu hayupo, halafu wakamkosoa.

Pia wanamaswali mengi kuhusu mungu, halafu wanajijibu wenyewe!!!

Halafu wanamwambia thibitisha kama mungu yupo!!!?

Nadhani nakaribia kuwafikia.

Sehemu zilizotangulia

Wanaopinga uwepo wa Mungu ni wakaidi

 
Thread zako mbili zote hujathibitisha Mungu yupo

Na hii yatatu lakini mambo ni yale yale

Huo ni zaidi ya ukaidi
Swali lako hilo bado ninalo kichwani, hivyo usihofu litajibiwa, ndio maana bado naendelea kulinukuu.

Kila jambo na wakati wake.
 
Thread zako mbili zote hujathibitisha Mungu yupo

Na hii yatatu lakini mambo ni yale yale

Huo ni zaidi ya ukaidi
Kwa sasa jikite kwenye mada
 
Swali lako hilo bado ninalo kichwani, hivyo usihofu litajibiwa, ndio maana bado naendelea kulinukuu.

Kila jambo na wakati wake.
Lengo la hii mada ni nini?
 
kwani hii ni mada yako ya kwanza yenye kichwa hiki?
Ok, ngoja nikusaidie kuelewa

Ni kweli hii mada haithibitishi kuwa mungu yupo, lakini ni katika sababu zilizo nifanya niamini kuwa mungu yupo.

Kwa sababu naamini huu ndio mfumo aliouweka mwenyezimungu(kwa hekma zake) ili wajawake wamtambue na kumuabudu.

Sasa wewe huoni kama huu mfumo upo sahihi, ndio maana ukaupinga.

Lakini mimi sitaki unipesababu ya kwanini unaupinga.

Mimi nachotaka ni wewe uonyeshe mfumo ambao ni sahihi, ambao ungekufanya uamini kuwa mungu yupo na ukamuabudu? yaani ulitaka iweje?

Sasa kwakuwa huwezi kufanya hivyo ndio maana mimi naitumia kama hoja na kukuita mkaidi.

Sijui utakuwa umenielewa kidogo.

Kama unaweza karibu.
 
Ok, ngoja nikusaidie kuelewa

Ni kweli hii mada haithibitishi kuwa mungu yupo, lakini ni katika sababu zilizo nifanya niamini kuwa mungu yupo.

Kwa sababu naamini huu ndio mfumo aliouweka mwenyezimungu(kwa hekma zake) ili wajawake wamtambue na kumuabudu.

Sasa wewe huoni kama huu mfumo upo sahihi, ndio maana ukaupinga.

Lakini mimi sitaki unipesababu ya kwanini unaupinga.

Mimi nachotaka ni wewe uonyeshe mfumo ambao ni sahihi, ambao ungekufanya uamini kuwa mungu yupo na ukamuabudu? yaani ulitaka iweje?

Sasa kwakuwa huwezi kufanya hivyo ndio maana mimi naitumia kama hoja na kukuita mkaidi.

Sijui utakuwa umenielewa kidogo.

Kama unaweza karibu.
1649923895880.png


Unasema una amini at the same time unasema hauoni mfumo huu upo sahihi. nikueleweje?

Imani ingekuwa njia thabiti ya kujua ukwei wa jambo, basi kungekuwa na dini moja yenye imani moja

Uwepo wa imani tofauti zinazopingana ni ushahidi kwamba imani sio mfumo sahihi
 
Leo natoa na salamu.

Kutokea pale nilipoishia.

Kwa mwenyeakili atagundua kuwa huu ulimwengu na vyote vilivyomo, havikujiumba vyenyewe bali kuna alieviumba ndio maana vipo katika mpangilio uliopangika sawa sawa.

Swali nani aliyeuumba na akauweka katika mpangilio huu?

Aliyeumba ulimwengu na kutuumba sisi wanaadamu hakutuacha hivihivi, bali alituma wajumbe(mitume) ambao ndio waliokuja na habari za uwepo wake na kuwa yeye ndiye aliyeuumba huu ulimwengu na vyote vilivyomo.

Hivyo uwepo wa huu ulimwengu na vilivyomo, na mpangilio wake, na uwepo wetu sisi wanaadamu na kukili kwetu kuwa hatujajiumbwa wenyewe, wala kuumba huu ulimwengu, basi hizi zikawa ni ishara za uwepo wa mwenyezimungu kwa wale wenyeakili.

Lakini mitume walikuwa ni wanaadamu na walikuwa wakifahamika na watu wao na pia hawakudai tu kuwa wao ni mitume wa mwenyezimungu, bali walithibitisha utume wao kwa kuonyesha miujiza -mambo ambayo sio ya kawaida-, na pia walikujanayo(vitabu) yalikuwa yanasadikisha wanayoyasema.

Na hii inaafikiana na sababu za kumuamini mtu.

Unaweza kumuamini mtu kwa sababu unamjua vizuri, hivyo unajua hawezi kudanganya katika anayoyasema au utamuamini baada ya kuthibitishia(ushahidi) au baada ya kuyasadikisha yale anayoyasema.

Maana unaweza usimuamini msemaji, na wala usiamini ushahidi alioutoa, lakini baada ya kuyasikia aliyoyasema ukayaona ni yakweli, hivyo ukamsadikisha.

Tukiacha khabari za mitume kwa ujumla wao, katika umma huu, tuna mtume Muhammad -swallallahu allaihi wasallam-, kuna mtu atasema hamjui!!!?

Kwa hakika katika binadamu ambaye historia ya maisha yake ipo exposed ni mtume Muhammad -swallallahu allaihi wasallam-, kuanzia anazaliwa, alivyoishi, kufa kwake, maneno aliyokuwa anayasema, mpaka alivyokuwa akikutana na wakeze, mpaka jinsi alivyokuwa akipiga mswaki!!!
huu ni uwazi ulioje?

Na huu ni mlango ambao upo wazi kwa kila mmoja, huyu ndiye mtume wa mwenyezimungu, na maisha yake yapo wazi, maneno yake yapo wazi(hadiith) na ujumbe aliokuja nao kutoka kwa Allah upo baina ya mikono yetu(Quran).

Lakini wanaompinga huwa hawaoni kuwa kunamazingatio kwenye historia ya maisha yake, kuwa imekamilika, bali wao wanatafuta sehemu wanazoweza kukosoa ili waendelee kupotosha watu na kueneza chuki.

Hivyo asiyemuamini na akampinga basi anampinga kwa kujua, maana anamjua na anayajua aliyokujanayo(Quran).
Vinginevyo atakuwa anampinga kwa ujinga(na huu ni ujinga ulioje)!!!?

Lakini hata kama mtu atawaamini mitume, ni wazi atakuwa na maswali, atajiuliza kwanini mwenyezimungu alituumba? kwanini maisha yapo hivi? mungu yupo wapi? mbona aliweka mfumo huu, na hakujidhihirisha? na maswali kibao kuhusu mwenyezimungu.

Lakini kwa akili ya kawaida tu, utagundua kuwa majibu sahihi ya hayo maswali, yatatoka kwa mtume ambaye yeye ndiye aliyekuja na habari za Mungu, na kwa aliyemuamini ni wajibu kuyaamini, maana ni katika muktadha wa kumuani kwake.

Hivyo muumini atauliza maswali yenye tija,lakini asiyemuamini atauliza maswali ya hovyo, na mbaya zaidi atajijibu mwenyewe, ili kujustify kutokuamini kwake.

Sasa wakana mungu wanajifanya hawana Imani, kisha wamempinga mtume(Muhammad swallallahu allaihi wasallam), na wameipinga Quran, kisha wakasema mungu hayupo, halafu wakamkosoa.

Pia wanamaswali mengi kuhusu mungu, halafu wanajijibu wenyewe!!!

Halafu wanamwambia thibitisha kama mungu yupo!!!?

Nadhani nakaribia kuwafikia.

Sehemu zilizotangulia

Wanaopinga uwepo wa Mungu ni wakaidi

Kwani aliyeviumba lazima awe mmoja? Magari yote, pipiki zote, baskeli zote zilitengenezwa na mtu mmoja? Hebu acheni kujitengenezea Mungu ambae hayupo
 
Kwani aliyeviumba lazima awe mmoja? Magari yote, pipiki zote, baskeli zote zilitengenezwa na mtu mmoja? Hebu acheni kujitengenezea Mungu ambae hayupo
Hebu onyesha ni jambo gani linakufanya uone huu ulimwengu na vilivyomo havikuumbwa na mungu mmoja?

Na utoe na mifano wa kila mungu na alivyoviumba?
 
Hebu onyesha ni jambo gani linakufanya uone huu ulimwengu na vilivyomo havikuumbwa na mungu mmoja?

Na utoe na mifano wa kila mungu na alivyoviumba?
we umejuaje kama vimeumbwa na mmoja na umejuaje kama huyo mmoja ni mungu na si kingine
 
Hebu onyesha ni jambo gani linakufanya uone huu ulimwengu na vilivyomo havikuumbwa na mungu mmoja?

Na utoe na mifano wa kila mungu na alivyoviumba?
Wewe una huo ushahidi wa Mungu mmoja tofauti na yale maandiko ya mchongo?

Angekuwa Mungu mmoja angewapa waislam sheria tofauti na wakristo, wayahudi sheria tofauti na waislam, wabudha sheria tofauti na wakristo? Huyo Mungu ni mmoja?

Haya sasa mtwambie ni Mungu gani aliyeviumba hivyo? Ni Allah, Yehova, Krishna au nani? Maana hawa wote wana sifa tofauti na sheria tofauti.

Ukisoma simulizi za kale za kihistoria (nimesema za kihistoria, sio za kiimani, maana historia inasikulia yaliyopata kutokea, na imani inalazikisha kuamini tu bila kuhoji hata kama huna uhakika. Kwa hiyo vitabu vya historia ni source ya kutumainiwa kuliko vitabu vya imani) utaona kuna viumbe walitoka nje ya dunia na ndio waliounda viumbe wote.
 
Thread zako mbili zote hujathibitisha Mungu yupo

Na hii yatatu lakini mambo ni yale yale

Huo ni zaidi ya ukaidi
Kwa hiyo chanzo cha uimbaji ni nini kama si Mungu?
 
Wewe una huo ushahidi wa Mungu mmoja tofauti na yale maandiko ya mchongo?

Angekuwa Mungu mmoja angewapa waislam sheria tofauti na wakristo, wayahudi sheria tofauti na waislam, wabudha sheria tofauti na wakristo? Huyo Mungu ni mmoja?

Haya sasa mtwambie ni Mungu gani aliyeviumba hivyo? Ni Allah, Yehova, Krishna au nani? Maana hawa wote wana sifa tofauti na sheria tofauti.

Ukisoma simulizi za kale za kihistoria (nimesema za kihistoria, sio za kiimani, maana historia inasikulia yaliyopata kutokea, na imani inalazikisha kuamini tu bila kuhoji hata kama huna uhakika. Kwa hiyo vitabu vya historia ni source ya kutumainiwa kuliko vitabu vya imani) utaona kuna viumbe walitoka nje ya dunia na ndio waliounda viumbe wote.
Kwann haiamini uwepo wa Mungu?
 
Chanzo cha uimbaji ni mziki
Una mishipa mingapi ya damu na fahamu katika mwili wako?

Na hiyo idadi utakayoitaja uliamuwa wewe mwenyewe uwe nayo au yupo aliyeamua uwe nayo

Kama uliamuwa wewe mwenyewe weka uthibisho

Na kama sio wewe tuambie ni nani aliyeweka hiyo idadi ya mishipa ya damu na fahamu katika mwili wako weka uthibitisho tumjue
 
Back
Top Bottom