Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 18,658
- 22,255
Mkeo kakutoroka? Inaelekea una msingi wa mawazo.1. Wauzaji na watumiaji wa Dawa za Kulevya
2. Waliofukuzwa kazi kwa ishu ya vyeti feki
3. Waliokuwa wanajilipa pesa kupitia dili za watumishi hewa
4. Wezi wa mifugo kabla ya wazo wa kupiga alama ya utambuzi kwenye minada
5. Walanguzi wa korosho kwa kangomba huku wakiwaibia wakulima
6. Watoto/wake/wame ambao baba/mama/zao wametumbuliwa kwa kashfa mbalimbali
7. Waliony'anyang'wa mashamba makubwa baada ya miaka mingi ya kuyakalia bila kuyalima huku wananchi wakiteseka kukosa ardhi
8. Waliojinufaisha kwa migogoro ya wakulima na wafugaji
9. Walioishi kwa magendo ya bandarini huku wakiliibia taifa
10. Wakwepa kodi hasa wafanyabiashara wa hali ya kati
11. Waliolipwa pesa baada ya uthaminishaji na wakakataa kuhama wakijua ni vya bure
12. Wanasiasa wapingaji na waropokaji maana kila jambo kabla hawajalisema Serikali inalitatua
13. Wezi wa madini, wanyama na mbolea za Serikali
14. Wanaokereka na mashine za kukusanyia mapato
15. Wanasiasa waliokata tamaa ya ushindi 2020 huku wasijue hatma yao