Wanaomaliza vyuo vikuu kipindi hiki cha awamu ya tano mpaka nawaonea huruma. Ajira zote zimezimwa kana kwamba nchi imesimama

Kazi ya serikali sio kuajiri. Huko vyuoni mnaposoma huwa mnaambiwa mkimaliza mtaajiriwa?
Hizi akili huwa mnazitoa wapi?hatutaki serikali iajiri per se,kwenye taasisi zake,tunataka iweke sera bora,Sekta binafsi ichangamke,izalishe ajira kibao,Kama wasomi wa vyuo wa korea,japan,china,wanazungumzia ajira,sembuse sie wa ulimwengu wa tatu,hata USA,ajira nyingi zimetengenezwa na sekta binafsi,iliyosaidiwa na sera bora za uchumi zinazosimamiwa na Serikali,
Hatutaki kwenda TRA,Bandari,TBS,TBC,tunataka tukiingia kwenye kilimo,mazao yapate soko,sio serikali ishindane na sisi kwa kuanzisha wakala anayesaga na kukoboa nafaka,
Viwanda vya magari South Afrika,sio mali ya serikali,mashamba makubwa ya kisasa sio ya serikali,ni watu binafsi,
Ukienda Zanzibar,wazungu wote wanaoanzisha mahotel,wengi wao,hawajawahi kuajiliwa serikalini,walifika hapo walipo kutokana na mpango madhubuti ya serikali,

Kampuni inayotengeneza bidhaa ya samsung,kule korea,ni ya mtu binafsi,hatuitaji serikali ijenge nyumba,ilime,serikali hii haiwezi kufanya biashara,iangalie TTCL,hoi,haiwezi hata kushindana na halotel!
 
Nchi sasa hivi inajiendesha Kama haina Rais. Wafanyakazi sekta zote wengine wanastaafu na wengine wanakufa kila siku lakini jamaa hataki kabisa Wala kusikia kuhusu ajira. Yuko radhi wote mfe ilimradi barabara zijengwe.

Elimu sasa hivi haina value tena Kama kipindi cha JK ambapo kuna vipaumbele vya ajira mpaka wazazi walikuwa wanajivunia kuwasomesha watoto maana ukimaliza tu ajira ipo mkono lakini sasa hivi ukimaliza msisitizo unaotolewa na JPM na viongozi wengine ni kujiajiri hawatwambii kama nchi imeahafilisika haiwezi kuajiri tena.

Kila kitu kimekuwa kugumu hata ukijaribu kuanza kufungua genge TRA wanamwagika unafirisiwa within no time. Uliamua kwenda kulima mazo ya biashara hakuna soko yote serikali imeyavuruga kwa uongozi huuvmbovu kuwahi kutokea.

Vijana salini Sana ndo kilichobakia ili mungu ampende zaidi.

Mungu awafanyie wepesi kwa mitihani yao!!

Serikali inabidi iwe na sera za kuinua vijana na sio kununua midege ambayo haina tija yeyote!! Fedha za midege wangepewa vijana wakavamia mapori wakawekeza kwenye kilimo ungefikiri wangehangaika?
 
Maajabu ya dunia nchi kama Tanzania Medical doctors/Pharmacists/Nurses na degree zao wanakaa mtaani hawana ajira huku ratio ya healthcare workers to patients ikiwa bado kubwa sana..

Hili tu linatosha kuonyesha how bad things are..
Wanasoma hadi kwa mikopo taifa lipate wataalamu. Wakihitimu hakuna ajira. Kwani ajira hazipo? Mwaka jana wakati wa kampeni za uchafuzi acha watangaze ajira! Madaktari 1000 kuajiriwa. Waalimu 13000 kuajiriwa kwenye halmashauri. Nani kaajiriwa? Nimekumbuka, ndiyo, yupo mmoja Abdallah kaandikwa mara 196 kwenye orodha ya mzee wa nyungu!
 
Ww hujielew aisee yani ktk hoja zote hapo unaenda tafuta single point ya jkt hv ratio ya walikosa kipnd cha kikwete na hawa ambao wana miaka mitano ni sawa?? Aya tuache ya jkt hao walim kipnd cha jk walikuwa wanazurura mtaani?? Kipnd cha jk kulikuwa hakuna increment na kupanda vyeo??
Nilikuwa nimeandaa bonge la tusi, Ila nakustahi.
Ikawaje mkawa mnashangilia huyo jk kuondoka na kumtukana matusi yote ikiwa kafanya hayo mazuri?
Tafuta comment yako humu ukimtukana ulinganishe na leo unavyomsifia, alafu sema "Mimi ni mjinga"
 
Acha kuongea kama zuzu mzee. Hata kama unalipwa kwa ku spin lakini kuwa na akili kidogo wapo watu waliomaliza shule miaka hiyo mpaka leo wameajiriwa . Kweli kazi ya serikali siyo kuajiri unategemea mtu aliyemaliza degree ya sociology mwaka jana akajiajiri wapi???
Wakati unaenda kusomea hiyo sociology uliambiwa ukimaliza serikali itakuajiri?
Kila anayemaliza chuo awe anaajiriwa, hiyo itakuwa serikali ya aina gani wewe bogus?
Nchi za ulimwengu wa Kwanza Hadi Leo wameshindwa kutatua tatizo la ajira, ije kuwa huku?
 
Na mtaani biashara ngumu, kufungua vikampuni kupata tenda au kazi nayo ngumu....
Inategemea unafanya biashara gani, sitaki nikupe mifano ya wanaofanya vizuri kwa Sasa na waliopata utajiri miaka ya karibuni kupitia biashara ambazo wewe unasema ngumu.
Endelea kushinda jf kulialia tu, ndio ulichobakia nacho.
 
Wanasoma hadi kwa mikopo taifa lipate wataalamu. Wakihitimu hakuna ajira. Kwani ajira hazipo? Mwaka jana wakati wa kampeni za uchafuzi acha watangaze ajira! Madaktari 1000 kuajiriwa. Waalimu 13000 kuajiriwa kwenye halmashauri. Nani kaajiriwa? Nimekumbuka, ndiyo, yupo mmoja Abdallah kaandikwa mara 196 kwenye orodha ya mzee wa nyungu!
Kazi ya serikali sio kuajiri. Na HAKUNA ambaye anaendaa chuoni kusoma alafu akaambiwa akimaliza serikali itamuajiri
 
Nilikuwa nimeandaa bonge la tusi, Ila nakustahi.
Ikawaje mkawa mnashangilia huyo jk kuondoka na kumtukana matusi yote ikiwa kafanya hayo mazuri?
Tafuta comment yako humu ukimtukana ulinganishe na leo unavyomsifia, alafu sema "Mimi ni mjinga"
Ungesema wewe kuwa ni mpumbavu. Ukisikia mtu anasema afadhali ya jana haina maana kwamba jana ilikuwa nzuri. Humaanisha leo ni hovyo zaidi ya jana. Zote ni shari lakini ya jpm ni balaa tupu!
 
Kazi ya serikali sio kuajiri. Huko vyuoni mnaposoma huwa mnaambiwa mkimaliza mtaajiriwa?
Tatizo la vijana mkishapewa 'vitempo' hapo ofisi za chama basi mnamezeshwa kila aina ya utopolo.
Ina maana wizara zifuatazo nazo hazihitaji nguvukazi..?for almost six years now.
* Wizara ya madini (sekta ya madini kwa ujumla)

*Nishati (Tanesco hawahitaji watu?)

* Kilimo na mifugo, ambako ndio ingemeza vijana wengi sana huko.

Hizi siasa za kipuuzi kwa miaka sita mtajitetea kwa lipi? Very stupidy regime!
 
Hizi akili huwa mnazitoa wapi?hatutaki serikali iajiri per se,kwenye taasisi zake,tunataka iweke sera bora,Sekta binafsi ichangamke,izalishe ajira kibao,Kama wasomi wa vyuo wa korea,japan,china,wanazungumzia ajira,sembuse sie wa ulimwengu wa tatu,hata USA,ajira nyingi zimetengenezwa na sekta binafsi,iliyosaidiwa na sera bora za uchumi zinazosimamiwa na Serikali,
Hatutaki kwenda TRA,Bandari,TBS,TBC,tunataka tukiingia kwenye kilimo,mazao yapate soko,sio serikali ishindane na sisi kwa kuanzisha wakala anayesaga na kukoboa nafaka,
Viwanda vya magari South Afrika,sio mali ya serikali,mashamba makubwa ya kisasa sio ya serikali,ni watu binafsi,
Ukienda Zanzibar,wazungu wote wanaoanzisha mahotel,wengi wao,hawajawahi kuajiliwa serikalini,walifika hapo walipo kutokana na mpango madhubuti ya serikali,

Kampuni inayotengeneza bidhaa ya samsung,kule korea,ni ya mtu binafsi,hatuitaji serikali ijenge nyumba,ilime,serikali hii haiwezi kufanya biashara,iangalie TTCL,hoi,haiwezi hata kushindana na halotel!
Unataka serikali ije ikuambie nenda kaanzishe kilimo?
Haao una iPhone 11, umenunua zaidi ya milioni na kila siku unapata bando la kuingia if, Ila unasubiri serikali ije ikupe mkopo wa mil 2 ili uende kuanzisha kilimo?
Nyie wengime mmezaliwa kuja kulalamika na kuwa ngazi za wengime
Sijawahi na sitakuja kuwahi kusubiri serikali au kampuni ya Mtu binafsi ije iniajiri. Nakukumbusha tu kuwa nna gunia za karanga 360, na gunia moja huku ni 72k kwa wastani wa 12k kwa kila debe
Hakuna hata mmoja aliyewahi kunifuata kuniambia kimbilia kwenye karanga.
Na sio hapo tu, miaka mitatu nyuma nilikuwa kwenye vitunguu swaumu.
Pole Sana, subiri Kuna kulialia humu na kusifia wenzio waliotoboa. au subiri Ontario akuletee forex ukadownload pesa
 
Ungesema wewe kuwa ni mpumbavu. Ukisikia mtu anasema afadhali ya jana haina maana kwamba jana ilikuwa nzuri. Humaanisha leo ni hovyo zaidi ya jana. Zote ni shari lakini ya jpm ni balaa tupu!
Kwa hiyo unasubiri serikali ikuajiri??
Haya subiri au endelea kulialia humu, si ndio kazi unayoiweza?
 
Tatizo la vijana mkishapewa 'vitempo' hapo ofisi za chama basi mnamezeshwa kila aina ya utopolo.
Ina maana wizara zifuatazo nazo hazihitaji nguvukazi..?for almost six years now.
* Wizara ya madini (sekta ya madini kwa ujumla)

*Nishati (Tanesco hawahitaji watu?)

* Kilimo na mifugo, ambako ndio ingemeza vijana wengi sana huko.

Hizi siasa za kipuuzi kwa miaka sita mtajitetea kwa lipi? Very stupidy regime!
Kila siku wanakuwa wanahitaji tu watu? Hizi nafasi hazijai?
Unamaanisha wizara ya madini kila mwaka iwe inaajiri tu? Wawe hata wakurugenzi 100?ili tu ionekane wanaajiri?
 
Mimi na vile nimegundua kuna retention fee na zile interest zinaongezeka. Niko na mpango nikimaliza tu nitembee mambele uko nibebe box. Ajira zenyewe hamna ndio maana hata kusoma huwa nakata tamaa niko bize na mishe za kitaa na kusoma vitu kibao ambavyo sitajibia ila nitaishi navyo.

Kwanza sina imani kama huyu mkemia anaondoka 2025
Huko mbele wao kazi yao ni kukuwekea wewe nafasi ya kwenda kubeba boksi?
 
Wakati unaenda kusomea hiyo sociology uliambiwa ukimaliza serikali itakuajiri?
Kila anayemaliza chuo awe anaajiriwa, hiyo itakuwa serikali ya aina gani wewe bogus?
Nchi za ulimwengu wa Kwanza Hadi Leo wameshindwa kutatua tatizo la ajira, ije kuwa huku?
Aliyekwambia wakimaliza waajiriwe wote nani??? Huko ulimwengu wa kwanza wanamaliza wangapi huku kwako wewe wanamaliza wangapi???
 
Tatizo la mbumbumbu hilo. Anaulizia wanayoambiwa vyuoni. Hutoka wapi hawa mbilikimo wa akili? Kazi ya serkali ni kusomesha tu na sio kuajiri? You must be full blown nuts. You, you nincompoop. Bodi kubwa ya mikopo. Wanaambiwa wataalamu wa hili au lile wanahitajika sana and urgently. Huko vyuo vikuu tena. Vijana wanajipinda. Kwao hakuna jm1 au juma ngapi. Wanachojua ni kitabu. Hadi vitabu vinanung'unika. Na wale wengine utasikia ufaulu umeongezeka. Hayo ndiyo wanayoambiwa we fala! Umeuliza, nimekujibu.
Hiki ndicho mnaweza, kuja jf kulialia.
Kazi ya serikali sio kuajiri.
Hao walioambiwa hizi nafasi zinahitajika urgently wapi huko? Au ndio kujipa moyo?
Wewe ni mmoja wa watu ambao kazi zenu ni humu jf kulialia, HAKUNA kingine mnachojua.
Na mtalia kwelikweli, maisha hayana huruma hata kidogo
Endelea ku-upload list ya mamilionea
 
JK aliweza kufanya hivyo. Kwa Nini iwe kwa JPM, au haelewi maana ya serikali?
Naweza kusema JK alijitahidi sana lakini hata yeye lazima angeshindwa kuajiri kwa kiasi tunachofikiria. Lazma tujue graduate ni zaidi ya laki moja mwaka na pia ujue karbia 50% ya pato la taifa linaishia kwa watumishi kwa ajili ya mishahara na stahiki mbali mbali. Private sector ipewe nafasi zaidi. Hapa ndipo pakupapigia kelele zaidi
 
Aliyekwambia wakimaliza waajiriwe wote nani??? Huko ulimwengu wa kwanza wanamaliza wangapi huku kwako wewe wanamaliza wangapi???
Unataka waajiriwe wangap?
Umejuaje Kama nafasi Bado zipo?
Tukubaliane hapa na ikibidi nikusainishe contract kuwa wewe kazi yako ni kulialia tu
 
Naweza kusema JK alijitahidi sana lakini hata yeye lazima angeshindwa kuajiri kwa kiasi tunachofikiria. Lazma tujue graduate ni zaidi ya laki moja mwaka na pia ujue karbia 50% ya pato la taifa linaishia kwa watumishi kwa ajili ya mishahara na stahiki mbali mbali. Private sector ipewe nafasi zaidi. Hapa ndipo pakupapigia kelele zaidi
Jpm alibugi step from day one pale alipoanza kudharau Marais waliopita na kuwaona hawakufanya kitu wakati ndo walifanya kitu kumzidi yeye anayepuyanga tu. Jk alimaliza wimbi kwa kuajiri walimu kila mwaka na madaktari lakini huyi toka aingia anawarundika mtaani tu
 
Nchi sasa hivi inajiendesha Kama haina Rais. Wafanyakazi sekta zote wengine wanastaafu na wengine wanakufa kila siku lakini jamaa hataki kabisa Wala kusikia kuhusu ajira. Yuko radhi wote mfe ilimradi barabara zijengwe.

Elimu sasa hivi haina value tena Kama kipindi cha JK ambapo kuna vipaumbele vya ajira mpaka wazazi walikuwa wanajivunia kuwasomesha watoto maana ukimaliza tu ajira ipo mkono lakini sasa hivi ukimaliza msisitizo unaotolewa na JPM na viongozi wengine ni kujiajiri hawatwambii kama nchi imeahafilisika haiwezi kuajiri tena.

Kila kitu kimekuwa kugumu hata ukijaribu kuanza kufungua genge TRA wanamwagika unafirisiwa within no time. Uliamua kwenda kulima mazo ya biashara hakuna soko yote serikali imeyavuruga kwa uongozi huuvmbovu kuwahi kutokea.

Vijana salini Sana ndo kilichobakia ili mungu ampende zaidi.
We poti mbona una mawazo ya hovyo. Ugwayiki
 
Back
Top Bottom