ok, Huyu Masauni anafahamu katiba ya Jamhuri ya muungano au anatumia katiba ya Zanzibar?
Mwambieni huku bara katiba inaruhusu watu kuongea wanachotaka bali wasivunje sheria, Mwambieni Zanzibar watu wa huku bara wanatubania ardhi ya kujenga
Mwambie Masauni kuna mambo ya msingi ya kuelimisha watu wake kama PGO, Atumie muda kuwaelekeza watu wake mambo ya PGO na kutenda haki
Mwambieni Masauni awe anasikiliza kauli za Rais kuwa Jeshi la polisi lishughulike na mambo yake ya msingi wasitoke kwenye lengo la kuanzisha Jeshi la polisi
Hivi watu bado hawakujifunza awamu ya sita ya JPM kuwa haya mambo yalitengeneza chuki mpaka kwa mara ya kwanza watanzania wakaanza kufurahia vifo vya viongozi wa kisiasa
Hapa JF tu watu walitoa kauli za kuombea Viongozi wafe kwa korona. Na viongozi waliokufa watu walishangilia
Angekuwa mkristu masauni ningesema kwanini Wagalatia mna roho ngumu na mmeweka pamba masikioni
Sasa huyu ustadh Masauni ameshaanza kupandisha mabega tena, Naona Masauni Mabega yameanza kupanda sasa
Tumkumbushe masauni alikuwepo Kangi Lugola yeye alivaa mpaka bendera ya Taifa na alitembea na ilani mitaani kama anaeneza injili
Hiyo wizara Kangi Lugola alishona suti zenye Rangi ya bendera ya Taifa
Ni muhimu viongozi wakakumbuka nchi imepita wakati gani
Hawa watu mambo yakiwa magumu wanaanza kuwalilia viongozi wa dini wawashauri wananchi
Masauni aache viongozi wa dini wapumzike, Tumechoka na makongamano ya Amani kila wakati na upatanisho wa kisiasa
Rais alishasema watu waongee, Yeye ameshajisahau anaingilia mamlaka ya Rais