Jasusi Mbobezi
Senior Member
- May 17, 2020
- 195
- 851
Kuna wakati nasoma baadhi ya nyuzi natambua 100% zimeandikwa na watu wakiwa na nia ya kudhihaki upinzani au akili zao huenda zina hitilafu.
Naamini hata wewe unajua hakuna mtu anayekubalika kwa wananchi kama Mh Magufuli; narudia hayupo. Nimekutana na watu mbalimbali sehemu mbalimbali na kila unayemgusia kuhusu utendaji wa JPM atakwambia kama ingewezekana tumwongeze miaka hata 20.
Hivi tunajifanya hatujaona ununuzi wa ndege ambazo kwa miaka mingi wapinzani wameitukana nchi kwa kukosa ndege hata moja? Sasa mwamba kanunua ndege 8 kwa cash na ni ndani ya miaka 5 kweli hatujaona?
Tembea nchi nzima uone miradi ya barabara inavyokwenda kwa kasi, hivi kweli tunajifanya hatujaona mpaka tunathubutu kusema JPM hajafanya kitu?
Wakazi wa Dar hivi mfugale Bridge, Ubungo Interchange havina msaada kwenu? Vipi barabara za mitaa nazo hamzitaki? Au zimejengwa na Lissu?
Miradi ya umeme kule kijijini kwenu kupitia REA nayo hamwoni? Miradi ya maji je? Kwanini hamna shukrani?
Huduma za afya mnazionaje? Hamwoni vituo vipya vya afya vilivyo jengwa nchi nzima? Hospitali zilizo jengwa na zilizo boreshwa nazo hamjaona? Vifaa vyakisasa kwenye hospitali hamjaona?
Mara ya mwisho kutembelea bandari za Dar, Tanga na Mtwara mmeona tofauti gani? Ni kweli Mh Rais hajafanya kitu? Viwanja vya ndege je? Vipi kuhusu ununuzi wa rada nalo hamjaona?
Mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa pamoja na mradi wa bwawa la kuzalisha umeme nayo hamjaona? Sio miaka 20 ni ndani ya miaka 5 tu.
Maboresho ya jiji la Dodoma pamoja na ikulu ya Chamwino pia hamjaona? Nikweli JPM hajafanya chochote?
Uhuru wa kujieleza mnaoutaka ni upi? Maana mnamtukana mitandaoni, mna kejeli kwa hisani ya mabeberu na mko huru tu, hivi mmewahi kusikia au kushuhudia uwepo wa watu kama Zitto, Fatma Karume, Maria Sarungi nk ktk serikali za China na North Korea? Unasemaje Tanzania hakuna uhuru?
Hamjaona ujenzi wa meli mpya kule Victoria? Yale si maendeleo? Au hamjaona? Mnasikia tena habari za ufisadi? Nikweli mioyo yenu haiwasuti?
Yapo mengi sana aliyoyafanya JPM ndani ya muda mfupi alio kaa madarakani, kama wewe ni mnafiki unaweza sema hakuna kilicho fanyika lakini kama una akili unajua tu mwaka huu wapinzani wanaambulia patupu.
Mh Magufuli huna hata haja ya kupiga kampeni, mwaka huu ushindi ni wakishindo maana unakubalika sana. Ziara zako ni ushahidi tosha wa jinsi tunavyo kukubali.
Nawasilisha.
Naamini hata wewe unajua hakuna mtu anayekubalika kwa wananchi kama Mh Magufuli; narudia hayupo. Nimekutana na watu mbalimbali sehemu mbalimbali na kila unayemgusia kuhusu utendaji wa JPM atakwambia kama ingewezekana tumwongeze miaka hata 20.
Hivi tunajifanya hatujaona ununuzi wa ndege ambazo kwa miaka mingi wapinzani wameitukana nchi kwa kukosa ndege hata moja? Sasa mwamba kanunua ndege 8 kwa cash na ni ndani ya miaka 5 kweli hatujaona?
Tembea nchi nzima uone miradi ya barabara inavyokwenda kwa kasi, hivi kweli tunajifanya hatujaona mpaka tunathubutu kusema JPM hajafanya kitu?
Wakazi wa Dar hivi mfugale Bridge, Ubungo Interchange havina msaada kwenu? Vipi barabara za mitaa nazo hamzitaki? Au zimejengwa na Lissu?
Miradi ya umeme kule kijijini kwenu kupitia REA nayo hamwoni? Miradi ya maji je? Kwanini hamna shukrani?
Huduma za afya mnazionaje? Hamwoni vituo vipya vya afya vilivyo jengwa nchi nzima? Hospitali zilizo jengwa na zilizo boreshwa nazo hamjaona? Vifaa vyakisasa kwenye hospitali hamjaona?
Mara ya mwisho kutembelea bandari za Dar, Tanga na Mtwara mmeona tofauti gani? Ni kweli Mh Rais hajafanya kitu? Viwanja vya ndege je? Vipi kuhusu ununuzi wa rada nalo hamjaona?
Mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa pamoja na mradi wa bwawa la kuzalisha umeme nayo hamjaona? Sio miaka 20 ni ndani ya miaka 5 tu.
Maboresho ya jiji la Dodoma pamoja na ikulu ya Chamwino pia hamjaona? Nikweli JPM hajafanya chochote?
Uhuru wa kujieleza mnaoutaka ni upi? Maana mnamtukana mitandaoni, mna kejeli kwa hisani ya mabeberu na mko huru tu, hivi mmewahi kusikia au kushuhudia uwepo wa watu kama Zitto, Fatma Karume, Maria Sarungi nk ktk serikali za China na North Korea? Unasemaje Tanzania hakuna uhuru?
Hamjaona ujenzi wa meli mpya kule Victoria? Yale si maendeleo? Au hamjaona? Mnasikia tena habari za ufisadi? Nikweli mioyo yenu haiwasuti?
Yapo mengi sana aliyoyafanya JPM ndani ya muda mfupi alio kaa madarakani, kama wewe ni mnafiki unaweza sema hakuna kilicho fanyika lakini kama una akili unajua tu mwaka huu wapinzani wanaambulia patupu.
Mh Magufuli huna hata haja ya kupiga kampeni, mwaka huu ushindi ni wakishindo maana unakubalika sana. Ziara zako ni ushahidi tosha wa jinsi tunavyo kukubali.
Nawasilisha.