Wanandoa fulani waliendelea kulala chumba kimoja na mtoto mkubwa anayeweza kuongea, labda kwa sababu ya uwezo mdogo wa kupanga chumba cha pili. Huyo mtoto alikuwa na tabia ya kukojoa kitandani kila anapokuwa usingizini. Mama yake alijitahidi kumuonya bila mafanikio. Siku moja mamake aliamua kumuadhibu kwa kosa la kukojoa kitandani. Mama yule alipokuwa anamuadhibu, mtoto yule alilalamika akisema kuwa 'mbona wengine wakikojoa kitandani huwachapi, lakini mimi nikikojoa unanichapa?' Mama yule akamuuliza mwanae kuwa 'ni nani mwingine anayekojoa kitandani simchapi?' Mtoto akajibu akasema 'mbona baba mkilala anakuambia anakojoa na wewe unamwambia kojoa tu mpenzi, halafu humchapi?' Mama yule aliondoka kwa aibu hakumchapa tena.
WanaJF tuwe makini na hali kama hizi!
WanaJF tuwe makini na hali kama hizi!