Hii mbona cha mtoto kaka, kuna Pedeshee mmoja alimpenda mke wa mtu. Jamaa mwenye mke,hakuwa vizuri kifedha. Pedeshee baada ya kuonja nyuki akataka kuchonga mzinga. Akamwambia mwanamke " nataka uachane na mumeo nikuoe kabisa ". Pedeshee akasema ili asitusumbue inabidi tumuue kabisa. Mwanamke akasema kumuua hapana. Wakakubaliana Pedeshee ampe mwanaume hela ili amuache mke wake kwa Pedeshee.
Siku ya siku Pedeshee akamuibukia jamaa (akiwa na mke wake ) na kumwambia mpango wake haramu " NIMEMPENDA MKE WAKO, NATAKA NIMUOE KABISA. NILIKUWA NA UWEZO WA KUMTOROSHA NA KUWA NAE BILA WEWE KUJUA,BUT NIMEONA SI VIZURI..SASA BASI SEMA UNATAKA SH NGAPI, NIKUPE UNIACHIE MKE WAKO...
Jamaa akamwambia Pedeshee, muulize kwanza mwanamke kama yupo tayari. Mwanamke akajibu nipo tayari nilikuwa nasubiria wewe ukubali. Jamaa hakuwa na jinsi,akamwambia Pedeshee nipe siku tatu nifikirie...
Baada ya siku tatu,jamaa akarudi kwa Pedeshee na kumwambia amekubali. Pedeshee akatoa sh milioni tano. Jamaa kachukua milioni tano kisha kaenda kwa mganga ili awatupie uchawi mke wake na pedeshee.....
Kesi nimeikuta kwa sangoma mmoja huko Rufiji wakati nafanya reseach kuhusu uchawi.