Wananchi Tuungane kupinga ongezeko la bei ya umeme

Nimekubali mkuu, tuambie ni wapi na ni lini tuingie barabarani

Nia Tunayo, Sababu tunazo, Uwezo tunao. mambo haya lazima kwanza tujitambue. Lazima tuamue kuchukua maamuzi magumu (?) Nafikiria jinsi ya kufanya mawasiliano humu kwenye jf ili tukutane na kuanza maandamano. Lazima tuwe na kitu cha kutuunganisha, yaweza kuwa wanaharakati au wanasiasa wenye mrengo wa NGUVU YA UMMA. This is serious, na wakati wa kuchukua hatua ndo sasa.
 
Wana JF kwa tabia yao ya kifisadi TANESCO wamezima link yao inayomwezesha mtumiaji wa luku anayetaka kununua luku sasa hivi(saa 3 usiku) asiweze - wa mekata mawasiliano na makampuni ya simu ili tushindwe kununua na kupata units za umeme! Ili kesho ndo tununue/tupate kwa bei yao mpya ya kifisadi - mungu atusaidie!!

Mkuu unadhani kununua umeme mwingi siku ya leo itasaidia? Kuna kitu kinaitwa 'service charge' ambayo ni charge ya @ mwezi. Jaribu kununua umeme mwingi then ukae kama miezi
sita hivi bila kununua umeme. Matokeo utaona!
 
Shirika la umeme Tanzania, Tanesco limekubaliwa ombi lake la kupandisha bei ya umeme kwa 40% kuanzia kesho. Hili ni pigo kubwa kwa wananchi wa kada zote, ingawa wenyewe wametupiga siasa eti ongezeko halitawagusa walalahoi. Ukweli ni kwamba ongezeko la bei ya umeme huchochea pia ongezeko la gharama za huduma mbali mbali ikiwemo afya, Elimu, mawasiliano, nk. kwa kuwa nyingi ya huduma hizo hutegemea nishati ya umeme. Pia huongeza hata bei ya mkaa maana ndo imekua kimbilio kwa kutoshikikika kwa bei ya umeme.

Wakati umefika kwa watanzania kuvaa ujasiri na kupambana na hawa watawala wetu ambao hawana huruma na Wananchi. Tuungane katika hili bila kujali itikadi. Kuna tetesi kwamba deni la dowans limeshalipwa kinyemela ndo maana wanataka kurudisha gharama kupitia kwa wananchi wanyonge. Tulipiga kelele kuhusu kuilipa Dowans, hivi sasa wako kimyaaaaa! Napendekeza maandamano makubwa ya kitaifa kupinga ongezeko hili. Katika hili naomba watanzania tulio wengi tuungane maana sote ni wahanga. Naomba kutoa hoja.

unaongelea wananchi wa wapi? Hawahawa wa tanzania? Acha bei ziendelee kupaa na maisha yawe magumu zaidi labda itasaidia kutuamsha
 
hata ungepanda asilimia 110 sawa tu kwa sababu wote tunatumia kuni na mkaa .ccm oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Umesema kweli tupu.Nani wa kufanya maandamano?Wenzetu Kenya tu wanatushinda kwa ujasiri wa kuandamana.Tatizo la nchi hii ni sisi wenyewe.

acha waongeze hata asilimia elfu moja, kila mtu atakufa na tai yake shingoni! Sioni watz kuungana kutetea haki zao, sana sana tunafikiria jinsi ya kuchakakua
 
Back
Top Bottom