Wananchi Tuunde Kamati Kubaini Uwezo wa Serikali

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,513
41,022
Tanzania haijawahi hata mara moja kukabiliana na majanga kwa namna ya kuridhisha. Ni kwa nini?

Kila wakati likitokea janga, Serikali inakimbilia kuunda kamati ambazo hazijawahi kutatua matatizo.

1. Tuliwahi kupata janga baya kabisa kule Mwanza la kuzama kwa meli, na watanzania wenzetu karibia 1000 waliteketea. Meli ile ikiwa imepulinduka, ilibakia bila kuzama kwa masaa zaidi ya manne lakini tulishindwa kuwaokoa abiria. Wachache waliookolewa, ilikuwa ni kwa msaada wa wavuvi.

2. Tuliwahi kupata ajali ya treni kusombwa na maji. Hata kutoa miili tu ilikuwa shida kiasi cha baadhi kutolewa viungo vikiwa vimenyofoka

3. Kuna lorry liliwahi kuangukia basi dogo pale Kimara, ilichukua zaidi ya masaa matano kulinyanyua lorry lililokuwa limelalia basi dogo likiwa na abiria ndani. Kuna abiria alipona lakini akiwa amekatika miguu, alibanwa chini akiwa analia kwa masaa zaidi ya matano. Hiyo ni Dar es Salaam, sijui ingekuwaje kama ajali ile ingekuwa imetokea Kigoma au Sumbawanga.

4. Kuna basi lilibeba wanakwaya wa Kenya lilipata ajali mkoani Tanga (nilishuhudia kwa macho yangu), ajali ilitokea saa 10 alfajiri lakini mpaka saa 2 majeruhi walikuwa bado hawajafikishwa hospitali. Kenya ilituma ndege kuja kuwachukua majeruhi na miili ya marehemu.

5. Jana limetokea janga la moto kwenye soko la Kariaokoo, katikati ya jiji, imeshindikana kuzima moto. Kama inashindikana kuzima moto uliotokea katikati ya jiji, mahali ambapo ni mita chache kutoka makao makuu ya kikosi cha zimamoto, tunatarajia wataweza kukabiliana na ajali ya moto ajali ikiwa imetokea wapi? Naamini moto hata ukitokea kwenye ofisi za makao makuu ya Zimamoto, matokeo hayatakuwa tofauti.

6. Kuna ajali nyingine nyingi za kuungua shule (watoto wetu wakapoteza maisha kutokana na uzembe wetu, na hasa Serikali), kuungua majengo ya biashara, ajali za barabarani na majini, zilizowahi kutokea, ambazo kwa hakika ukitazama jinsi zilivyoshughulikiwa, unaona kabisa kuwa hakuna uwezo wa Serikali kushughulika na majanga.

Ukifuatilia majanga ambayo yamewahi kutupata na yanayoendelea, hakika hizi kamati zinazoundwa na serikali hazina maana kabisa.

Ajali za mabasi zinapotokea, unashangaa kusikia eti uchunguzi wa Polisi umeonesha kuwa chanzo cha ajali ni kupasuka tairi la mbele. Ah! Ujinga kabisa! Hivi kweli hii ni taarifa ya kiuchunguzi toka kwa chombo kama Polisi? Mtu ungetegemea, taarifa ingekuwa ya kina, kama wanavyofanya wenzetu, kama vile:

1) basi lilikuwa katika mwendo gani. Ulikuwa mwendo sahihi au hapana? Mwendokasi ulichangia kwa kiasi gani kutokea kwa ajali na madhara yake?

2) tairi liliposuka, lilitengenezwa mwaka gani? Lilikuwa bado kwenye kipindi cha matumizi kwa kadiri ya muda ulioneshwa na mtengenezaji? Tairi lilistahili kuendelea kutumika, kwa kuangalia viashiria vya kiwango cha kutumika?

3) tairi lililopasuka, kama lilikuwa bado kwenye muda wake wa matumizi kwa vigezo vya muda wa kutengenezwa na kutokana na kiwango kilichotumika, lilikuwa na ubora unaotakiwa?

4) uchunguzi wa ubora wa matairi ya kampuni hiyo uliofanyika a kwa mtengenezaji au wakala wake, umedhihirisha matairi hayo yana ubora unaotakiwa?

6) kama chanzo cha tairi kupasuka, ni ubora wake, hatua za dharula zilizochukuliwa kuzuia matumizi ya matairi ya kampuni hiyo, ubadilishaji wa matairi ya kampuni hiyo kwa magari yote yanayotumia matairi ya kampuni hiyo.

Lakini kwa bahati mbaya inaonesha Jeshi la Polisi, halina uwezo kabisa wa kufanya uchunguzi wa kina.

Ni vema kwenye Katiba mpya, kila janga/ajali inapotokea, Serikali inapounda Kamati ya uchunguzi, wananchi kwa kupitia taasisi huru, zisizo za kiserikali, na ambazo hazina uhusiano wa moja kwa moja na Serikali, zipewe haki ya kuunda kamati za kuichunguza Serikali, kupima yafuatayo;

1) uwezo wa jumla wa serikali kushughulikia janga lililotokea

2) uwezo wa taasisi husika katika kushughulikia na kupunguza madhara ya janga

3) proactivity ya Serikali na taasisi husika

4) kuwatambua watu ndani ya Serikali wa kuwajibishwa kutokana ama na uwezo mdogo au uzembe.
 
KWAKWELI!
1626005291402.png
 
60% ya viongozi Tanzania hawana uwezo"Prof Assad

Viongozi wetu waambia mambo ya mikutano ambapo wanajua Kuna posho huwezi sikia shida ya pesa ila pesa ya kuwekeza sehemu muhimu kipindi Cha majanga hakuna ndio maana serikali hii hii ilikula Mpaka pesa ya rambirambi.

Leo katikati ya jiji Moto unashika soko muhimu vifaa hakuna hii ni aibu kubwa Sana alafu viongozi wapo wapo tu wanaishia kutoa matamko ya kuunda kamati shameless and hopeless kabisa
 
Hii nchi inaongozwa na watu wa ajabu sana wasioweza kutatua hata matatizo madogo tu ya asprine & ganzi

Ilitakiwa wananchi tuandamane tuwakamate tuwale mattercor
 
Kwa kifupi matukio mengi yakichunguzwa unakuta ni uzembe tu wa serikali yenyewe kwa namna moja ama nyingine.

Hivyo unakuta hakuna hatua stahiki zinazochukuliwa.

Kuna kuzuia majanga

Kuna kuyakabili yanapotokea

Na hatua baada ya hayo majanga.

Kwetu hakuna hata hatua moja tunayoiweza kufanya kwa ufanisi.
 
Kwa kifupi matukio mengi yakichunguzwa unakuta ni uzembe tu wa serikali yenyewe kwa namna moja ama nyingine.

Hivyo unakuta hakuna hatua stahiki zinazochukuliwa.

Kuna kuzuia majanga

Kuna kuyakabili yanapotokea

Na hatua baada ya hayo majanga.

Kwetu hakuna hata hatua moja tunayoiweza kufanya kwa ufanisi.
Ummy tayari ana suluhisho la tatizo la kuungua masoko. Anasema watajenga mavisima makuuuubwa pembezoni mwa masoko ili yatumike masoko yanapoungua. Hii nchi vituko sana kwa kweli.
 
Hata viongozi wa vyama vya upinzani tatizo ni Hilo hilo.

Huwezi amini kiongozi wa upinzani anakaa madarakani for 20 good years halafu anaona ni sawa tu. (Huo ni udikteta).

Kiongozi wa chama Cha upinzani anajipa title ambayo Haina election ( Kiongozi Mkuu wa Chama).

Kiongozi wa upinzani anahamasisha mikutano na sio kudai mambo muhimu ya kijamii.

Ukilaumu CCM pekee unakua unakosea maana yaliyomo huko hamna tofauti na vyama ambavyo vinaweza kuwa mbadala.
 
Uwezo wa serikali itabidi uangaliwe kwenye nyanja kadhaa; uwezo wa vifaa (kama vinaendana na wakati, vipo vya kukidhi mahitaji), uwezo wa watumiaji wa hivyo vifaa (efficiency), na miundombinu yetu kama ni wezeshi kukabiliana na hayo majanga mfano ya moto.

Nikiangalia mengi kati ya matukio uliyoorodhesha, naona uzembe unachukua sehemu kubwa sana, people are very slow to react hata kama upatikanaji wa vifaa sio mgumu, chukulia mfano tukio la hiace kuangukiwa na container Kimara, hili tatizo halistahili kuchukua dakika ishirini halijatatuliwa kwa kuzingatia mazingira ya eneo la ajali, na upatikanaji wa vifaa, uzbe tu wa watendaji.

Sababu nyingine nayoiona hapa ni kuishi kwetu kwa mazoea, tupo tupo tu, kila mara tunasubiri ajali zitokee halafu tuseme ni mapenzi ya Mungu. Matukio kama ya majengo kuungua kwa moto yamekuwa yakitokea mfululizo toka mwaka jana, kuanzia shule za bweni kule Kagera mpaka Dsm shule moja pale Kinondoni, na kwingineko.

Lakini mpaka leo bado hatujachukua madhubuti kukabiliana na haya majanga, tunaangalia tu then yanapita maisha yanaendelea.
 
Hata viongozi wa vyama vya upinzani tatizo ni Hilo hilo.

Huwezi amini kiongozi wa upinzani anakaa madarakani for 20 good years halafu anaona ni sawa tu. (Huo ni udikteta).

Kiongozi wa chama Cha upinzani anajipa title ambayo Haina election ( Kiongozi Mkuu wa Chama).

Kiongozi wa upinzani anahamasisha mikutano na sio kudai mambo muhimu ya kijamii.

Ukilaumu CCM pekee unakua unakosea maana yaliyomo huko hamna tofauti na vyama ambavyo vinaweza kuwa mbadala.
Haya "matatizo" ya viongozi wa upinzani yaligharimu maisha ya wangapi?
 
Haya "matatizo" ya viongozi wa upinzani yaligharimu maisha ya wangapi?
Wengi tu,

Kwa mfano maandamano yasiyo na kibali pale kinondoni yalisababisha kumpoteza binti mdogo kabisa wa chuo.

Vijana wengi wamepata majeraha kutokana na siasa uchwara.

Muulize Dr. Slaa alichokipata.

Mabomu ya Soweto.

Few to mention ila Upinzani umesababishia watu mateso na adha mbali mbali.
 
Wengi tu,

Kwa mfano maandamano yasiyo na kibali pale kinondoni yalisababisha kumpoteza binti mdogo kabisa wa chuo.

Vijana wengi wamepata majeraha kutokana na siasa uchwara.

Muulize Dr. Slaa alichokipata.

Mabomu ya Soweto.

Few to mention ila Upinzani umesababishia watu mateso na adha mbali mbali.
Naona unataka kuleta siasa kwenye maisha ya watu, ngoja nikuache tu nisijeumiza hisia za wengine kwa kile nitachoandika, simply kama tatizo ni wapinzani ndio walisababisha hayo majanga kwa raia kwanini hamkuwapeleka mahakamani?
 
Naona unataka kuleta siasa kwenye maisha ya watu, ngoja nikuache tu nisijeumiza hisia za wengine kwa kile nitachoandika, simply kama tatizo ni wapinzani ndio walisababisha hayo majanga kwa raia kwanini hamkuwapeleka mahakamani?
Hayo ndio matatizo ya kutaka kusikia Yale unayoyapenda kuyasikia.

Nilidhani unataka kujadili logically.
 
Katiba mpya ndio dawa, tume za kuchunguza majanga ziwe huru kutoa mapendekezo ya kuiwajibisha serikali.
 
Back
Top Bottom