Wananchi sasa wamchoka JK

Kwan jamaa haon hali halis ya maisha ya watu wake mpaka aambiwe na wasaidizi wake? Huyo Njaa Kaya aliwahi kuulizwa na ktuo kimoja kikubwa cha television duniani kuwa kwanini nchi yake ni maskini wakati ina raslimali kibao, mjamaa akasema hajui! Sas kama hajui anagombea urais ili afanye nini kama hajui chanzo cha umaskini wetu? Hawez kufanya kitu kwa kuwa hata hajui kazi inayomfanya awe madarakani!

kaka wewe hapo ulipo kila kinachoendelea una kiona? Rais ni kiongozi wa taifa macho yake ni mawili tu hawezi kuona kila linaloendelea nchi nzima, ndio maana anateua watu wa kumsaidia katika kazi. sasa tatizo la msingi hapa ni uadilifu na uzalendo wa mteuliwa mmoja mmoja kitu ambacho JK hawezi kuwajua wote tabia zao, naamini wengine yeye huletewa majina tu huwa siyo rahisi eti JK wote aliowateuwa anawajua tabia zao, majina hayo yeye huletewa na wale anaohisa ni wasafi kumbe siyo na matokeo yake wanapopangiwa majukum hufanya ubadhirifu mkubwa sana na hujitahidi sana kuficha kupitia report zao. na mbaya zaidi na wale waliopewa mamlaka ya kukagua mazingira yanaonesha huhongeka kiurahisi na kuendelea kuuficha ukweli.
 
Katika hali ya kawaida nisingekugongea like, lakini umejaribu kusema jambo fulani pamoja na uwakala wako!

Swala la msingi ni je? Rais anachaguliwa ili awategemee 100% hao wanaosimama pembeni yake na wateule wake? Kama jibu ni ndio...........yeye tunamchagua wa nini sasa!!!

Kama anaowateua wanamfanya katuni, wanakwiba bila woga, wanamkenulia meno nae anasema good job!!...........yeye tulimchagua ili ateue majizi? au tulimchagua asiweze kusimamia hata kitu kimoja???

Kama amechaguliwa na aliowachagua ndo wanamuangusha.................Je, hata wale ambao hajawateua yeye kama wabunge.......wote wa Upinzani na wale wa chama chake wenye nia njema wanapomwambia ....mkuu, wanakudanganya haoooo!!! wezii haooo mkuu!!! kwa nini hasikii??? kwa nini mpaka apate aibu,...aaibishwe na wateule wake ndo anaanza kuhaha kwa kutoa majibu ya vijana wa Form One B shule ya secondary Ilembula?? Rahisi rahisi tu!!

Imagine............eti tatizo la umemem ni la ukame...........Basi, yani tumemchagua na yeye akachagua wasaidizi ile wafanye mambo kwa mzunguko wa dunia na jinsi Mungu na mawingu yatakavyopenda? Mvua za vuli zisiponyesha this year (ofcouse hatutegemei yeye akawe mawingu ili inyeshe!!) TOTAL BLACK OUT!!!

Viongozi wa CCM wanaoipenda nchi hii, ambao hawapo serikalini wako wapi? tuwasikie wakiwakemea wateule wa Kikwete? Wazee wa DSM wakwapi? au kwao umeme unawaka, mafuta ya taa wananua bei gani? Wao hawawezi kumuita Huyu waliyempa kura nyingi na kumwambia......Bwana mkubwa, tunaumia, wanatuumiza, wateule wako wanatukandamiza sisi huku wakineemeka wao!! fanya jambo hima!!
Sio kila siku litokeapo jambo la msingi kwa wananchi, anawaita wazee na kuwapa posho na kuanza kupiga mkwala..........wazee wampige mkwala pia basi!!

Hizi jumuia za wazazi wa CCM, wakina mama ziko wapi? wanafanya nini? au kazi yao ni kukutana kwenye mikutano mikuu na kupeana posho na MIPASHO TU!!!!

Inaniuma sana!!!! this guy need to act.............aanze na kuwa serious kwanza na aache kufikiri WTZ ni mapoyoyo!!!

Kaka nadhani kuna kitu umekisahau au hukijui kuwa Rais ni political figure, pale kuna system ina exist ndio maana maamuzi magumu hayawezi fanyika kibubusa. pale america Obama siye anayeiongoza nchi yeye ni figure tu wanaoiongoza nchi wapo. kama ulikuwa hujui jua kuwa rais hafanyi maamuzi peke yake, kwahiyo kama wale anaoshirikiana nao wameamua kumficha taarifa au wakamwambia taarifa fulani lakini wakampindisha ktk kuitolea maamuzi basi na rais utamuona hivo. Mfano mwepesi kwako siku zile wafanyakazi walivyotaka kugoma rais aliongea na matokeo yake media nyingi zililpoti kuwa rais kadanganywa sasa nijibu nani alimdanganya?
 
Kaka/Dada kweli Jk ni ndugu yako basi bwana kama una ndugu wa hivyo anayewasahau watu wake sijui hata kama ufalme wa mbinguni utaupata pole sana.
 
kama wapambe hawampatii taarifa za hali halisi ya watanzania then atoke aende kwa watanzania azungumze nao, yeye kutwa kucha yuko nje ya nchi atayajuaje ya watanzania sasa!!! mbona alizunguuka karibu TZ nzima kuomba kura na kutoa ahadi hewa, leo kumekua kituo cha polisi?
 
Mkandara,

Hoja nzuri sana umetoa.Kama demokrasia ingekuwa universally beneficial kwa mataifa yote basi tungekuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kunufaika.Kwa hali ilivyo sasa,ni kweli kuna kila Dalili kwamba Demokrasia imetushinda tunaifanyia majaribio tu bado tena kwa mbinu na mikakati ile iliyoshindwa

Kwa kweli hii dhana tuliyoletewa ya Demokrasia,imesababisha sisi kurudi nyuma.Hatuna tofauti na mfumo wa kisultani.Leo hii maamuzi magumu ya hayawezi kuchukuliwa kwa hoja ya kipuuzi kabisa mkuu wa nchi yupo nje ya nchi.Rais akiwa nje kuna VP na wengineo,katiba yenye maono ya demokrasia inasema hivyo.

Ni bora turudi kwenye mfumo wa chama kimoja utakaozuia fikra ili sisi wengine tusiopenda kuburuzwa tutumie nguvu za kimapinduzi kwa kusukumwa na uzalendo wetu tuchukue nchi tuongeze kidikteta lakini kizalendo.Tunahitaji utawala kama wa Gaddaffi,tunahitaji mfumo kama wa kagame na Hugo Chavez.tunahitaji mfumo kama wa Evo morales,kusema kweli na siogopi kusema Democracy does not Suit us.bado hatujajiandaa,hii ni imported vice ! ! !

Kama si kuitikia wito na kukubali kuburuzwa na mfumo wa kibeberu,leo hii ningekuwa kwenye kambi,milima ya mbali na au hata msituni kujiandaa kizalendo.Ningekuwa na sababu za kutosha ! ! ! Huwezi kuwa na demokrasia ya kweli kama wananchi wako ni maskini,wanasumbuliwa na maradhi na Ujinga....Huwezi kuwa na uongozi ambao ni zao la Demokrasia bila kuwa na msingi wa imani ya kisiasa,kiuchumi na kijamii katika kiungo cha uongozi na utawala (namaanisha ideology).

Leadership tuliyo nayo ni hadaa tu,sio kwa serikali tu hata kwa vyama vingine vya siasa.Tunapata pigo kubwa sana kwa ngumi iliyovaa gloves za demokrasia(Pseudo democracy).jaribu kufikiria na kutafakari juu ya mfumo wote wa vyama vya siasa Tanzania,jaribu kufuatilia mfululizo wa matukio kwenye vyama hivyo.Kila siku tunapiga hatua kuwasukuma vijana wazalendo kuingia kambini,milimani au misituni.kila dakika ambayo tunahubiri democracy na vijana wazalendo kweli kweli kwa nchi yao hawaoni uhalisia na matunda yatokanayo na dhana hiyo basi tunawatoa kwenye Demokrasia tunawapeleka misituni.

Haya yana Mwisho,kinachohitajika ni hatua za haraka zichukuliwe ama la basi yatatimia.Carl max,alisema...'A single step in the Revolutionary movement worths a Dozen programmes'
 
Magwanda nanyi hamueleweki yani kashifa ya Jairo ndio mawaziri wa Wizara zote wajiuzuru? Mmmmh magwanda kuweni serious!
Uu kilaza gani kutokuilewa barua ya Jairo "Kama kawaida" yaani ni utamaduni wa bunge la magamba kuhongwa unahitaji nini kuelewa hii ni kashfa ya serikali? Au Jairo ameondoka kusevu majizi mengine mliyoyaficha?! Sasa ndiyo tunaelewa kwa nini hoja zenye maslahi ya taifa zilikuwa zikipingwa bila sababu/ "wanaokubali waseme NDIYOOOOOO!!!!" jamani inatia kinyaa.
 
Nakuunga mkono kwamba rais hana habari na shida za wananchi wake. kama ulimsikiliza jana alipokuwa anahojiwa BBC alijibu maswali kipuuzi sana tena huku akicheka. Hivi kweli miaka hamsini ya uhuru unasema tatizo ni ukame tena sisi hatuwezi kuiambia mvua inyeshe kweli????!!!!!! Karne ya 21 bado unategemea mvua kwa umeme wa taifa mlikuwa wapi miaka yote 50 bila kutafuta njia mbadala haya basi mtasema hela hazikuwepo je mmepoteza shilingi ngapi katika ufisadi na kama mko na nia ya dhati baada ya kupata taarifa za ufisadi mmefanya nini kizurudisha hela hizo kwa faida ya taifa zaidi ya kulindana, wewe mwenyewe rais unahusika sana kwa mambo mengi yaliyohusikia ndio sababu unawalinda kila afanyae maovu hayo . jana unahojiwa unacheka dah inauma sana. mtanzania anataabika wewe unacheka na kuzurura tu ulimwenguni. haukuchaguliwa kwenda kutalii tu mpaka mataifa mengine yakuita mtalii. I HATE U unaongoza kama wewe ndio kizazi cha mwisho tanzania kumbuka utalipwa hapa hapa maandamano ya tunisia yalianzishwa na mmachingakwa kujitolea kufa kwa faida ya wengi angalia fikiria na chukua taadhari.
Ufisadi uliotingisha bunge katika wizara ya Nishati na Madini - Kwa nini hao mawaziri wasijiuzulu?

Inaonekana hawa mawaziri wana nguvu inayowalinda


Licha ya wananchi wa mijini kuchoka migao ya umeme, hali ngumu ya maisha pia Wakulima (wananchi wa vijijini) kutokana na mafuta taa kupanda bei.

Bei kubwa ya mafuta taa imefanya maisha kuwa magumu sana vijijini.

Hata huku mjini, hakuna umeme watu wanategemea mafuta taa, ila bei imepanda maradufu.

Wakati huo huo JK hana habari na shida za watanzania.
 
Back
Top Bottom