Wananchi 7,000 wanufaika na umeme

elivina shambuni

JF-Expert Member
May 31, 2018
461
295
SERIKALI imesema mpaka sasa, idadi ya wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro ambao wamenufaika na punguzo la bei la kuunganishiwa umeme vijijini kwa Sh. 27,000 bila kulipishwa gharama za nguzo wanafikia 7,000.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, alisema jana kuwa mpango huo ulipoanzishwa Mei, mwaka huu, kwa amri ya Rais John Magufuli, watu 5,000 waliunganishiwa huduma hiyo Juni na Julai peke yake. Alikuwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kyeri, wilayani Hai wakati wa uzinduzi wa umeme kwenye kaya zilizonufaika na mpango huo. "Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania kwa kuwa na umeme katika maeneo mengi sawa na asilimia 87. Kilimanjaro ina kata 148 ambazo zote zina umeme, una vijiji 519 ambavyo kati yake 453 vina umeme.

Ukiangalia bado kuna vijiji 66 tu ambavyo viko Hai (vitano), Siha (saba), Rombo (vinane), Mwanga (vinne), Moshi (22) na Same (20) ambavyo vinasubiri huduma hiyo," alisema Mgalu. "Mheshimiwa Rais Magufuli ametuagiza tupunguze gharama za kuunganishia wananchi umeme vijijini kutoka Sh. 177,000 hadi Sh. 27,000," alisema.

Naibu Waziri alisema kati ya vijiji 66 vya mkoa wa Kilimanjaro ambavyo bado havijaunganishiwa umeme, vitakavyobakia hadi Desemba mwaka huu ni 35 na kati ya hivyo, serikali imeliagiza Shirika la Umeme (Tanesco) kuchukua vijiji 18 ili iviunganishe. Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo, mradi wa umeme vijijini awamu ya tatu ya mzunguko wa pili utaunganisha vijiji 17 tu vitakavyokuwa vimesalia.

Akiwa katika kijiji hicho, Naibu Waziri huyo wa Nishati, alitoa namba yake ya simu ya mkononi kwa wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro na kuwaelekeza 'wambipu' ili awapigie na kutatua kero husika endapo wataambiwa na Tanesco au mkandarasi yeyote kwamba walipie nguzo, nyaya au mita wakati wakipeleka maombi ya kuunganishiwa umeme. Aidha, Mgalu alitoa onyo kwa mameneja wa Tanesco ngazi ya wilaya na mkoa ambao watakaidi agizo la serikali linaloelekeza kuwa wananchi wote wa vijijini waunganishiwe umeme kwa gharama ya Sh. 27,000 tu.

source :NIPASHE
 
Wachaga hata kushukuru na kumpongeza JPM kwa upendeleo hamtaki. Kazi yenu kutukana na kuchokonoa mabaya! Mikoa mingi hata maeneo ya manispaa hayana umeme wakati nyie vijiji 87% vina umeme!
 
Wachaga hata kushukuru na kumpongeza JPM kwa upendeleo hamtaki. Kazi yenu kutukana na kuchokonoa mabaya! Mikoa mingi hata maeneo ya manispaa hayana umeme wakati nyie vijiji 87% vina umeme!
Utaambiwa kwamba huyo JPM anatimiza ahadi yake kwa kufanya anacholipwa kukifanya.

Shukrani huwa zinakuja siku na saa tusiyoitegemea, mara nyingi Mungu huwa na njia zake zisizoweza kuelezeka kirahisi.

Unampa ombaomba shilingi mia tano asubuhi saa nne na saa kumi unapata habari ya kufaulu usaili wa kazi, wewe na wengine wawili wakati mlipoomba mlikuwa watu elfu mbili.
 
Jaman tuache kukuza maneno. Mkoa wa Kilimanjaro ulikiwa na umeme vijijini toka enzi za mkoloni. Wilaya ya hai nilikozaliwa umeme uliletwa na wajeruman na tumezaliwa enzi za mwl na umeme ulikuwepo Tena kwenye nyumba za udongo

Tanesco walichofanya Ni kusambaza umeme maeneo machache Sana ambayo wanayatangaza kuliko Yale waloyakuta na umeme
 
Jaman tuache kukuza maneno. Mkoa wa Kilimanjaro ulikiwa na umeme vijijini toka enzi za mkoloni. Wilaya ya hai nilikozaliwa umeme uliletwa na wajeruman na tumezaliwa enzi za mwl na umeme ulikuwepo Tena kwenye nyumba za udongo

Tanesco walichofanya Ni kusambaza umeme maeneo machache Sana ambayo wanayatangaza kuliko Yale waloyakuta na umeme
Acha longolongo wewe? Wakoloni ndo walianzisha umeme wa grid ya taifa? Umeme wa TANESCO ni wa Umma wa Watanzania na mikoa, wilaya, kata, vijiji, na vitongoji vyote vina haki sawa kupata umeme! Huo umeme wa wakololoni unaousemea haukuwa wa umma labda wa maporomoko ya maji au mafuta tena katika makazi pekee ya wakoloni! Tangu lini mkoloni alisambaza umeme vijijini! Nyie wachagga Mungu anawaona! Kila kitu kujifanya wajuaji na mdomo mrefu na kuona makabila mengine wapumbavu! Tangu Baba wa taifa hadi kikwete hamkuwahi kukosa waziri mkuu hata first lady (mama Anna Mkapa). Mkapora nafasi nyeti za ajira (TRA na Wizara ya Fedha, BoT) na kujipendelea katika miradi muhimu ya umeme, maji, elimu, n.k. Ndo maana nasema bora mfunge domo lenu. Tunawashangaa kuona mnaponda serikali pamoja na hayo yoote mliyotendewa wakati mikoa mingine hoi taabani kwa umasikini
 
Acha longolongo wewe? Wakoloni ndo walianzisha umeme wa grid ya taifa? Umeme wa TANESCO ni wa Umma wa Watanzania na mikoa, wilaya, kata, vijiji, na vitongoji vyote vina haki sawa kupata umeme! Huo umeme wa wakololoni unaousemea haukuwa wa umma labda wa maporomoko ya maji au mafuta tena katika makazi pekee ya wakoloni! Tangu lini mkoloni alisambaza umeme vijijini! Nyie wachagga Mungu anawaona! Kila kitu kujifanya wajuaji na mdomo mrefu na kuona makabila mengine wapumbavu! Tangu Baba wa taifa hadi kikwete hamkuwahi kukosa waziri mkuu hata first lady (mama Anna Mkapa). Mkapora nafasi nyeti za ajira (TRA na Wizara ya Fedha, BoT) na kujipendelea katika miradi muhimu ya umeme, maji, elimu, n.k. Ndo maana nasema bora mfunge domo lenu. Tunawashangaa kuona mnaponda serikali pamoja na hayo yoote mliyotendewa wakati mikoa mingine hoi taabani kwa umasikini
Nenda kajifunze kwanza tanesco kama.shirika lilianzishwa lini na umeme ulikuwepo machame mwaka gani. Halafu ndo uje.na porojo zako
 
SERIKALI imesema mpaka sasa, idadi ya wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro ambao wamenufaika na punguzo la bei la kuunganishiwa umeme vijijini kwa Sh. 27,000 bila kulipishwa gharama za nguzo wanafikia 7,000.

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, alisema jana kuwa mpango huo ulipoanzishwa Mei, mwaka huu, kwa amri ya Rais John Magufuli, watu 5,000 waliunganishiwa huduma hiyo Juni na Julai peke yake. Alikuwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kyeri, wilayani Hai wakati wa uzinduzi wa umeme kwenye kaya zilizonufaika na mpango huo. "Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania kwa kuwa na umeme katika maeneo mengi sawa na asilimia 87. Kilimanjaro ina kata 148 ambazo zote zina umeme, una vijiji 519 ambavyo kati yake 453 vina umeme.

Ukiangalia bado kuna vijiji 66 tu ambavyo viko Hai (vitano), Siha (saba), Rombo (vinane), Mwanga (vinne), Moshi (22) na Same (20) ambavyo vinasubiri huduma hiyo," alisema Mgalu. "Mheshimiwa Rais Magufuli ametuagiza tupunguze gharama za kuunganishia wananchi umeme vijijini kutoka Sh. 177,000 hadi Sh. 27,000," alisema.

Naibu Waziri alisema kati ya vijiji 66 vya mkoa wa Kilimanjaro ambavyo bado havijaunganishiwa umeme, vitakavyobakia hadi Desemba mwaka huu ni 35 na kati ya hivyo, serikali imeliagiza Shirika la Umeme (Tanesco) kuchukua vijiji 18 ili iviunganishe. Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo, mradi wa umeme vijijini awamu ya tatu ya mzunguko wa pili utaunganisha vijiji 17 tu vitakavyokuwa vimesalia.

Akiwa katika kijiji hicho, Naibu Waziri huyo wa Nishati, alitoa namba yake ya simu ya mkononi kwa wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro na kuwaelekeza 'wambipu' ili awapigie na kutatua kero husika endapo wataambiwa na Tanesco au mkandarasi yeyote kwamba walipie nguzo, nyaya au mita wakati wakipeleka maombi ya kuunganishiwa umeme. Aidha, Mgalu alitoa onyo kwa mameneja wa Tanesco ngazi ya wilaya na mkoa ambao watakaidi agizo la serikali linaloelekeza kuwa wananchi wote wa vijijini waunganishiwe umeme kwa gharama ya Sh. 27,000 tu.

source :NIPASHE

Kuna mambo hayapaswi kuongelewa karne hii, yan mwaka 2019 bado tunaongea mambo ya watu flan kupata umeme?
 
Back
Top Bottom