Wanamuziki Bora wa Kikongo!nilicheza na kuvua shati...!

Wanamuziki Bora wa Kikongo!nilicheza na kuvua shati...!

Jumong S

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
7,449
Reaction score
10,788
Wadau,
Katika tasnia ya muziki Africa ni vigumu kutoitaja Congo. Nimepata kuishi kambi za wakimbizi wa kikongo na huko nilishuhudia namna muziki ulivyo damuni. Kuna kanisa moja la asili wakati wa kuimba yaani ni bonge la bolingo na hutatamani ibada iishe. Wakati wa udogo wangu kuna mziki wa Azalaki - Ghato(sijui kaishia wapi) tuliucheza sana kwa kuwaiga wa-Zaire huku mshindi akipewa zawadi ya Big G/jojo/bazoka.

Hebu kama umewahi kupenda nyimbo za wakongo tupia walau mmoja na jina la mwanamuziki aliyekukosha enzi za udogo wako na unakumbuka nini.
Twende kazi...!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
kuna wimbo mmoja wa bongo man unaitwa LIZA!!!!ni hatari mpaka leo niusikiapo natoa chozi.Enzi hizo maisha mazuri sio kama sasa mambo yanaendeshwa ki huni huni tu.
 
Nilizaliwa na kuishi uswahilini sana ambako vilabu vya gongo vilirindima muda wote...sitasahau wimbo wa Muchana kanda bongoman.

Ingawaje hatukuwa na fedha, lakini maisha yalikuwa na maana kubwa kwetu. Tulikuwa na furahaa.
 
Kitu Efrakata by Koffi Olomide, wacha kabisa aisee

Nakumbuka nilikua form two miaka hio yaani sie ndio wajanja miaka hio
 
kuna wimbo mmoja wa bongo man unaitwa LIZA!!!!ni hatari mpaka leo niusikiapo natoa chozi.Enzi hizo maisha mazuri sio kama sasa mambo yanaendeshwa ki huni huni tu.

Wewee! MUCHANA ndio wimbo bora zaidi.
 
Aurlus Mabele bado napenda kusikiliza nyimbo zake kama Extra Ball,Zanbel na Canon Scie pamoja na kwamba zilitoka zaidi ya miaka 20 iliyopita.
 
Music Clarification ya marehemu Pepe Kale ulinipagawisha sana hasa rap za Djuma Bumbafu, Fred Nelson ya Extra Musica, Mbongo ya marehemu Mayaula Mayoni hakika nyimbo hizi zilipopigwa ilikuwa raha sana moyoni.
 
Me zaman yangu ni ya Awilo longomba. Dah nilikuwa kichaa na coupe di bamba,mobimba etc etc
 
Kuna collabo moja ya Franco Luambo Makiadi na Rochereau Tabu Ley inaitwa Lisanga ya Baganga, ni hatari sana. Kuna wimbo mwingine wa Madilu System unaitwa Frere Edouard, kwa kweli Congo Kinshasa wana vipaji sana hawa jamaa.
 
Extra Musica lipo songi lao la Danide, aah! Full maraha!kila mmoja alipenda kusikiliza hata kama lugha ilikuwa hatuielewi!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Music Clarification ya marehemu Pepe Kale ulinipagawisha sana hasa rap za Djuma Bumbafu, Fred Nelson ya Extra Musica, Mbongo ya marehemu Mayaula Mayoni hakika nyimbo hizi zilipopigwa ilikuwa raha sana moyoni.
Enzi hizo mtu mwenye radio ya Panasonic ndo tajiri! Vijana tuliembea na Walk man! Tozi bila walkman hujakamilika...! Kweli cha zamani dhahabu!


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Kuna collabo moja ya Franco Luambo Makiadi na Rochereau Tabu Ley inaitwa Lisanga ya Baganga, ni hatari sana. Kuna wimbo mwingine wa Madilu System unaitwa Frere Edouard, kwa kweli Congo Kinshasa wana vipaji sana hawa jamaa.

Mkuu kuna kipindi nilifanya kazi makambi ya hawa wakongo, du jamaa wana vipaji sana! Wanajua kucheza na kuimba sio kawaida! Pia wana upendo na utamaduni wao. Sio hizi bongo fleva zina radha ka jojo/big G muda si mrefu inaisha utamu!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
kuna wimbo mmoja wa bongo man unaitwa LIZA!!!!ni hatari mpaka leo niusikiapo natoa chozi.Enzi hizo maisha mazuri sio kama sasa mambo yanaendeshwa ki huni huni tu.

Yap, hawa jamaa wazuri aisee! Sitasahau sauti tamu za Oliver Ngoma, Kanda Bongo man na Mbilia bell. Huchoki kusikiliza! Tafuteni wimbo wa Sheli!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Samangwana & Franco. Mulongo na Mulozi. Jamani jamani. Kweli muziki unaraha yake.
 
Back
Top Bottom