kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
BAADHI ya wakazi wa Manispaa wametakiwa kuacha imani potofu ya kunywa majivu kabla ya kujamiina kwa madai kuwa kwa kufanya hivyo ni kujikinga na
maambukizi mapya.
Mratibu wa Ukimwi Shinyanga, Dkt. Charles Mashenene amewataka wananchi wa Kata ya Ndala, Manispaa ya Shinyanga kuachana na imani hiyo potofu kuwa wakinywa majivu hawawezi kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa kuwa huo ni upotoshaji mkubwa na unaongeza kasi ya maambukizi.
Dkt. Mashenene alisema hayo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kupambana na ugonjwa wa Ukimwi iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Shinyanga Foundation Fund (SFF) linalojihusisha na masuala ya ukimwi chini ya ufadhiri wa Shirika la Rapid Funding Envelop la jijini Dar es Salaam.
Akitoa mada iliyohusu 'ukweli kuhusu ukimwi' kwenye mkutano wa hadhara ulifanyika viwanja vya viwandani kata ya Ndala mjini hapa na kuhudhuriwa na umati wa wananchi ambapo aliwaeleza umuhimu wa kubadili tabia ili kupunguza kasi ya maambukizi ya vvu pamoja na kupima kwa hiari afya zao.
Kwa upande wa mratibu wa ukimwi manispaa ya Shinyanga Rhobi Gwesso alidai kuwa wananchi kutowanyanyapaa waathirika wa ukimwi na badala yake washirikiane nao katika shughuli za maendelo na kwamba kuugua ukimwi siyo mwisho wa maisha.
Kwa upande wake meneja wa shirika hilo, Bw. Paul Sangija alisema shirika lake limeshaanza kubaini makundi mbalimbali katika jamii yanayojihusisha na biashara ya ngono wakiwemo wanaume sita wanaojihusisha na biashara ya ngono kinyume na maumbile; na wanawake 150 wanaofanyanya biashara ya ngono pamoja na mamalishe wenye uhusiano wa kimapenzi na wateja wao kwa lengo kuwa karibu na watu 1,050.
Alisema kuwa tayari shirika hilo limeanza kujenga vibanda 60 vya maduka
vitakavyotumiwa na makundi hayo ambavyo vitagharimu sh. milioni 300 kupitia kwa wafadhili wao Rapid Funding Envelop.
maambukizi mapya.
Mratibu wa Ukimwi Shinyanga, Dkt. Charles Mashenene amewataka wananchi wa Kata ya Ndala, Manispaa ya Shinyanga kuachana na imani hiyo potofu kuwa wakinywa majivu hawawezi kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa kuwa huo ni upotoshaji mkubwa na unaongeza kasi ya maambukizi.
Dkt. Mashenene alisema hayo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kupambana na ugonjwa wa Ukimwi iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Shinyanga Foundation Fund (SFF) linalojihusisha na masuala ya ukimwi chini ya ufadhiri wa Shirika la Rapid Funding Envelop la jijini Dar es Salaam.
Akitoa mada iliyohusu 'ukweli kuhusu ukimwi' kwenye mkutano wa hadhara ulifanyika viwanja vya viwandani kata ya Ndala mjini hapa na kuhudhuriwa na umati wa wananchi ambapo aliwaeleza umuhimu wa kubadili tabia ili kupunguza kasi ya maambukizi ya vvu pamoja na kupima kwa hiari afya zao.
Kwa upande wa mratibu wa ukimwi manispaa ya Shinyanga Rhobi Gwesso alidai kuwa wananchi kutowanyanyapaa waathirika wa ukimwi na badala yake washirikiane nao katika shughuli za maendelo na kwamba kuugua ukimwi siyo mwisho wa maisha.
Kwa upande wake meneja wa shirika hilo, Bw. Paul Sangija alisema shirika lake limeshaanza kubaini makundi mbalimbali katika jamii yanayojihusisha na biashara ya ngono wakiwemo wanaume sita wanaojihusisha na biashara ya ngono kinyume na maumbile; na wanawake 150 wanaofanyanya biashara ya ngono pamoja na mamalishe wenye uhusiano wa kimapenzi na wateja wao kwa lengo kuwa karibu na watu 1,050.
Alisema kuwa tayari shirika hilo limeanza kujenga vibanda 60 vya maduka
vitakavyotumiwa na makundi hayo ambavyo vitagharimu sh. milioni 300 kupitia kwa wafadhili wao Rapid Funding Envelop.