wanajeshi wa kike na maisha ya uraia

Mkuu tafadhali kwa heshima na taadhima! Usiuchafue huu uzi. Sasa mbona hawa siyo Wanajeshi!!

Hawa si ndiyo wale wenye mafungamano na kile chama gani sijui!! Ika na wenyewe kuna warembo! Cha kushangaza pisi kali zote hupatikana mjini pekee!
yani huyo jamaa sijui ana nia gani na huu uzi. mpaka nishaanza kumkumbuka komandoo wetu Moses lijenge

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Navy S.E.A.Ls (SEa, Air and Land) a.k.a The Frog-men(jina wanalojipa baada ya kuhitimu mafunzo), Tadpoles(jina wanalopewa wale ambao bado wako mafunzoni).

Nay SEALs ni kikosi maalum cha jeshi la majini(Navy) na recruitment ni kipaumbele kwa wanamaji (Navy soldiers) wanaoweza fanya uingiliaji kutoka Baharini(sea), Angani(air) na nchi kavu(land) na ndo jina lao lilipopatikana hapo.

Yasemekana zipo Team 10, ila maarufu zaidi ni SEAL Team 6 (Official name; Navy Special Warfare Development Group (NSWDG), a.k.a DEVGRU), ambayo imegawanyika katika uniti ndogo ziitwazo "Squadron"(mfano; Gold squadron, Red Squadron), ambazo pia zimegawanyika katika uniti ndogo zaidi ziitwazo "Teams"(mfano; Alpha, Bravo, Charlie) ambapo kila team inaweza kuwa na wanakikosi("Operators") kati ya 6 mpaka 10, pamoja na wasaidizi(support structure/personnel) kwa kila "team". Team SIX wanachukua wanavikosi(operators) kutoka Team1, 2, 3, 4, 5, 7, 8, 9 na 10, wanawapeleka mafunzoni tena ndo wanachukuliwa na kupachikwa katika Squadron tofauti tofauti.

Pia Team SIX ipo chini ya United States Special Operations Command (USSOCOM) ambayo inadeal na vikosi vile vilivyonolewa na vikanoleka kweli kweli (mfano SEAL Team 6/DEVDRU, 75th Ranger Regiment, 1st Special Forces Operations Detachment-Delta(1st SFOD-D) a.k.a Delta force etc.)

Navy SEALs wengi wanatoka ndani ya Jeshi la majini(Navy), ni nadra sana kukuta Seal aliyetoka kikosi cha nje ya jeshi la majini.

TV series;
a)SIX
b)SEAL Team

Navy SEALs Motto: The Only Easy Day was Yesterday.


1st Special Forces Operations Detachment-Delta (1st SFOD-D)
a.k.a Delta Force/The Unit
Kikosi chenye siri zaidi katika vikosi maalum vya majeshi ya marekani.

Kikosi hiki ndio kina utaratibu wa kuchukua wanavikosi(operators) kutoka katika kikosi chochote kile katika majeshi ya marekani ambaye wanaona anafaa kuungwa na kikosi hicho.

Delta foce ndio kikosi kinasemekana kilichomuua gaidi Osama Bin Laden, kikiwa kimeundwa na wanavikosi kutoka vikosi maalum mbalimbali ndani ya jeshi la marekani kama team 6, marine raiders, 75th ranger regiment etc., wakibebwa katika "helicopter" maalum za kikosi maalum cha misheni maalum cha jeshi la anga kiitwacho "Night Stalkers'.

TV series;
a)The Unit

Movies:
a)Delta force (imechezwa na Chuck Norris)
b)13 Hours; Secret Soldiers of Benghazi (humu wanaonekana karibia n mwisho wa movie wakiwa wawili katika kwenda kusaidia uokoaji na ulizi wa balozi)

1st Special Forces Operations Detachment-Delta Motto (kwa usiri wao motto yao yasemekana kuwa ni) : Silent Professionals
Utadumu mwamba

Huu msemo wa "Navy SEALs Motto: The Only Easy Day was Yesterday" unatumika na Sf wa kwetu pia pale 92

Utasikia "The only easy day was yesterday, toil boy, toil!"

Pain is my medicine.
 
Mwanajeshi Mwingine uyu apa
images-405.jpg
images-406.jpg
 
US Marine corps ni kikosi maalum kwa ajili ya mambo mengi tu na Wamarekani hujivunia sana hiki kikosi ndo wanalinda balozi karibu zote za Wamarekani, utawaona White house, hata zile helicopter Rais wao hutumia zimepewa majina hayo Marine 1/2.Kikosi kinatumika sana kwenye uvamizi (Assault), Rescue mission na mambo mengine mengi hiki hawa jamaa wanajivunia sana utaskia "Once a marine always a marine"

Navy ni kikosi cha wanamaji hapa tunazungumzia nyambizi zote, manowari, na Meli zote za kivita na hapa Wana command karibia dunia nzima kwenye international water wanazunguka sana Kuna Pacific command base yake ipo Hawaii. Hii ina cover Asia YOTE Japan, Korea (North & South), mpk China kama sijakosea. Mpk kwetu Africa base ipo nafikiri ni Djibouti kama sijakosea. Wataalam wataongezea.

Navy Seal special forces hii ni tofauti hawa ni kikosi maalum kwa kazi maalum wenye mafunzo ya Hali ya juu sana. Recruits wa hiki kikosi anaweza Kuwa raia lakini wengine hujiunga kutoka kwenye Vikosi vingine kama National Guards, Marines, Navy etc. Hawa Wana opperate kwa vikundi vidogo vidogo lkn wanaleta matokeo makubwa hutumwa nyuma kabisa ya mistari ya adui ili kuhujumu, kuokoa mateka,

Hawa wanauwezo wa kuvamia kutokea popote Majini, Ardhini, Angani na wakaleta matokeo chanya kwa nchi. Ingawa misheni zao zipo zilizo feli pia.
Seal team wanaweza pigana in Sea, air na land ndo kirefu Cha seal team
 
Back
Top Bottom