Wanajeshi mbaroni Thailand kwa “dili la sembe”

Wanajeshi mbaroni Thailand kwa “dili la sembe”

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,356
Tatizo la biashara ya dawa za kulevya kuendeshwa na matajiri, viongozi na waajiriwa wa nafasi nyeti serikalini na katika mashirika mbalimbali makubwa, linafanana karibu kila nchi. Habari ifuatayo, japo kwa ufupi, itakupa picha ya jinsi ilivyo ngumu kupambana dhidi ya biashara ya dawa za kulevya.

Nchini Thailand, askari mstaaru wa jeshi la Marekani, Joseph Manuel Hunter (48) maarufu kwa jina la “Rambo”, na washirika wake wawili kutoka jeshi la Ujerumani –Dennis Gogel na Michel Filter -- askari mwingine mmoja kutoka jeshi la Poland, Slawomir Soborski, mtu mwingine kwa jina Timothy Vamvakias pamoja na watu watatu, walikamatwa mjini Phuket siku ya Alhamsi iliyopita, wakiwa katika harakati za kukamilisha njama za kuua watu wawili muhimu waliokuwa kikwazo katika kufanikisha usafirishaji wa dawa za kulevya.

Hunter alikuwa na cheo cha Sergeant daraja la kwanza na “an air-assault and airborne-infantry squad leader, a sniper instructor and a drill sergeant” wakati Vamvakias alipata cheo cha Sergeant baada ya kuhudumu nchini Korea Kusini na Puerto Rico na wote waliacha jeshi mwaka 2004.

Kwa kutumia ujuzi wao, Hunter alifanya kazi kama ‘wakala wa mauaji’ kwa malipo na kufanikisha mauaji ya watu kadhaa. Walipokamatwa Alhamisi iliyopita, alikuwa ameingia mkataba wa kujipatia dola za Kimarekani $700,000 ili kufanikisha mauaji ya watu wawili na angeongezewa $100,000 endapo angeongeza vyema mauaji hayo. Ushirikiano wa askari kutoka mabara manne waliokuwa wakifuatilia nyendo zao ndiyo uliowezesha kukamatwa kwao kabla ya kutekeleza mpango wao huo haramu.

Watu hao wamefunguliwa kesi na mashitaka katika mahakama moja ya jijini Manhattan nchini Marekani na tayari Hunter amesharejeshwa nchini humo ili kukabiliana na kesi hiyo. Kinachosababisha mapambano dhidi ya biashara hii na watu hawa kinatokana na ukweli kuwa, “The charges tell a tale of an international band of mercenary marksmen who enlisted their elite military training to serve as hired guns for evil ends”

Mwishoni mwa mwaka 2012, Hunter kupitia anwani yake ya email, alikusanya CV za watu mbalimbaliwenye ujuzi na masuala ya ulinzi na usalama, wakitka kuajiriwa katika kundi hilo. Wakili mmoja, Preet Bharara anayeshughulikia kesi hiyo ameelezea kuwa ni, "bone chilling… the indictment read like they were ripped from the pages of a Tom Clancy novel."

Source: Vita ngumu! Askari wa Marekani, Ujerumani, Poland mbaroni Thailand kwa
 
Mh....hii vita ni ngumu sana kwa kweli.
Haishangazi kuona Nzowa alipokwenda South Africa akituaminisha kuwa anafuata ushahidi utakaoweza kuufahamu mtandao wa wauza unga, kumbe alienda kutoa Technical support on how kuugeuza ushahidi, yaani ule 'unga' toka illegal drugs to useful one ...(dawa ya pumu).
 
Back
Top Bottom